Jaji Mfawidhi
JF-Expert Member
- Feb 20, 2016
- 14,047
- 20,412
Jeshi la Zimamoto na Uokoaji nchini Tanzania ni chombo cha serikali kinachohusika na masuala ya kuzima moto, uokoaji, na huduma za kwanza katika maeneo ya dharura.
Kamishna MASUNGA ameleta mabadiliko makubwa sana, ila bado kuna mengine anapaswa kusaidiwa ama na serikali ama
- Kuanzishwa: Jeshi la Zimamoto na Uokoaji la Tanzania lilianzishwa rasmi mnamo mwaka 1963 chini ya Wizara ya Mambo ya Ndani.
- Lengo kuu la kuanzishwa kwake ilikuwa ni kutoa huduma za kuzima moto na uokoaji katika maeneo ya dharura.
- Kuimarika Kwa Miaka: Kupitia miaka, jeshi hili limeimarika na kupanuka kutoa huduma bora zaidi katika kuzuia majanga ya moto na kutoa msaada wakati wa dharura. Pia, limefanya kazi kwa karibu na mashirika mengine ya kutoa huduma za dharura nchini Tanzania.
- Mafunzo na Vifaa: Jeshi la Zimamoto na Uokoaji limekuwa likipokea mafunzo na vifaa vya kisasa kwa lengo la kuboresha uwezo wake wa kushughulikia majanga ya moto na dharura zingine.
- Kukabiliana na Majanga: Jeshi hili limekuwa likishiriki katika kukabiliana na majanga mbalimbali, ikiwa ni pamoja na kuzima moto wa viwanda, misitu, na majumbani, pamoja na kutoa msaada katika dharura kama vile ajali za barabarani na majanga ya asili.
- Kuhamasisha Elimu: Jeshi la Zimamoto na Uokoaji limekuwa likihamasisha elimu kwa umma kuhusu hatari za moto na jinsi ya kujikinga. Wanatoa ushauri kuhusu uokoaji na kuwahimiza watu kuwa na vifaa vya kuzima moto nyumbani.
- Usimamizi wa Majanga ya Asili: Jeshi hili limehusika katika shughuli za kusimamia majanga ya asili kama vile mafuriko na moto wa misituni ambayo yanaweza kutokea nchini Tanzania.
- Usalama Barabarani: Pamoja na majukumu yake mengine, Jeshi la Zimamoto na Uokoaji linashiriki katika shughuli za usalama barabarani kwa kutoa huduma za kwanza na uokoaji kwa waathirika wa ajali za barabarani.
-Kufuatia tukio la moto siku ya 1-10-2023 maeneo ya Kariakoo na msimbazi kwenye kituo cha mafuta cha Big Bon almaarufu kama "sheli ya Big Bon , na kuunguza maduka yasiyo na idadi imegundulika kwamba:-Kinyume cha sheria za nchi na mazingira[NEMC] kibali kilitolewa maduka ya rejareja kujengwa kuzunguka kituo hicho cham mafuta.
-Kama haitoshi, imegundulika kwamba Jiji Limeanzisha kituo rasmi cha Bajaji Kuzunguka "sheli ya Big Bon" kinyume cha seria za Usalama wa Mazingira.
-Imegundulika kuwa vichochoro karibu vyote kati ya jengo na jengo , mitaa ya Big bon vimezibwa na kwekwa maduka[wazaramo wanaita "flem"] isivyo halali na hivyo Kariakoo kujifunga .
- Imegundulika fremu nyingi hazina "fire extinguisher" na hata moto wa jana ulipolipuka hakukuwa na vizimia moto ndio maana wanalaumu zima moto ilhali wao wenyewe hawana, na sababu za kutokuwa nazo ni zile zile za wao kutoa hela kidogo"rushwa" wasinunue fire na hivyo ni tabia ya miaka na mikaka.
- Imegundulika kuwa maduka mengi ya vichochoroni kariakoo ndiyo yanayouza "smuggling" na counterfeited items, bidhaa feki na zisizolipiwa ushuru zipo mitaa ya vichochoroni. TRA na ujanja wao hawajui ama wamefanywa wasijue hili jambo.
- Vigogo wengi wastaafu, wa idara fulani fulani za Manispaa huwa ndio wanajipa vibali visivyo halali vya kujenga vichochoroni na hawalipi kodi.
- Maduka mengi ya vichochoroni hasa ya vipuli yanauza vilivyoibwa kwenye magari na wale wanao uza lubricans/oil ni zile oil zinazochemshwa pale Tabata dampo na kujazwa kwenyee makopo mapya ya makampuni ya mafuta.
Serikali iwaachie wananchi watakacho si mtu anakaa masaki amuamulie mtu anayekaa Tandale.
-JE, hawa wakipigiwa simu 999 huwa wanapokea kwa wakati? Kabla ya kufika na gari lao kubwa lisilo na maji, kwanini wasiwe na watu wanaotumia pikipiki zile kama za polisi zenye vingora waende kuhakikisha MOTO?