Zimamoto sasa imefeli, Irudishwe Halmashauri, Hakuna Moto umewahi kuzimwa na ZT!

Jaji Mfawidhi

JF-Expert Member
Feb 20, 2016
14,047
20,411
Baada ya Magufuli kuingia madarakani, aliwapa hadhi idara ambazo ni idara tu na kuongeza matumizi yasiyo ya Lazma. Hili jeshi la zimamoto ni mzigo kwaTaifa na sasa tunaomba mh Samia Suluhu alirudishe kama zamani, fikiria halmashauri ya Moshi ilikuwa na magari matatu ya kuzima moto na ndiyo yanahudumia mkoa mzima, huyu kamishna alipoteuliwa nakuagiza magari yakabidhiwe kwake haujulikani mengine yalipopelekwa ila mkoa ukabakiziwa gari moja. hilo garo nalo ni bovu siku zote na moto ukitokea kilimanjaro inatumika FIRE ya TPC au KIA na si hii ya serikali. Ina maana kuna dereva anakula mshahara wakati gari halifanyi kazi

Aliwapa uhamiaji kuwa inajitegemea na kumteua anna Makakala kuwa kamishanmkuu.
Akawapa Zimamoto kuwa idara na kuteua kamishana mkuu.
Idara nyingine sizigusi , wachangiaji mtazitaja wenyewe.
Zimamoto ilipopewa mamlaka yake, kamishana wake ana hahdi kama IGP, the same na uhamiaji.

Wakachukua magari yote na mali ambazo zamani zilikuwa zinaendeshwa na halmashauri zikawa za zimamoto.
Zimamoto wao kazi kubwa , tangu iundwe ni kugombanie kwendsa kwenye maofisi na sehemu za biashara kukagua mitungi za FIRE EXTINGUISHER.

Zimamoto wao, kumetokea moto Moshi soko la mbuyuni mara mbili, meimoria, nyumba soweto, Kaloleni zote ziliteketea kwakuwa hakuna anayejishughulisha zaidi wao wanataka hela ya kufutia viatu pale wanapokagua na kukuta huna mtungi.

Msikilize Mbunge wa Moshi Mjini ambaye hajawahi kufanya kitu chochote tangu aingie bungeni, haulizi swali, hajibu hoja, ila inasemekana anaopngoza kwa kupiga meza, ambaye pia ni classmte na mtoto wa raisi flani mstaafu na kura za maoni aliangukia pua sema akabebbwa na Bwana yule ndugu PRISCUS TARIMO.


 
Back
Top Bottom