ZILIPENDWA: Wanamuziki, nyimbo na mitindo yao

Mimi natafuata jina la wimbo mmoja nadhan ni wenge bcbg, unaimbwa "baswahili batakingalaba titi, eliiiiii mamaaaa eliiii maamaaa
Aysee ninaujua vizuri mkuu mpaka video yake wamevaa kijeshi jeshi.nadhani ulikuwa unahamasisha mambo ya amani,tatizo jina la wimbo sasa!! Ngoja nifukue fukue nikiupata nitakujuza
 
HOT CLUB BANGERS VOL 1 - By Dj Times9
Screenshot_20210201-183307.jpg
 

Marquiz du zaire - Mama Maria Nyerere


Field Marshal Nguza Chimbwiza Vicking na Maestro Ndalla Kasheba wakiongoza kundi zima la Maquiz Du Zaire kumtakia Mama Maria Nyerere maisha ya marefu na mema ya ustaafu kijijini Butiama baada ya kazi ngumu za majukumu ya kama First Lady.
Source: zamani leo


nitaicheki hii
 
February 2021
Paris , France

SAM MAGWANA - FESTIVAL AU FIL DES VOIX - ÈDITION NUMÈRIQUE


CONCERT DIGITAL FILMÈ AU 360 PARIS MISIC FACTORY

Source : Festival Au Fil des Voix
 
Babloom Kisauji : song : "Uya kaya" (official audio)


Mwanamuziki mkongwe Seif Kisauji akionesha jinsi Tanzania ilivyojaliwa mirindimo ya kila aina ya muziki
Source : Babloom Kisauji
 
Kwema huku, nataka kujua kwa kuhusu wimbo wenye maneno haya,
Naenda Ilula kwa wakwe zangu wakanielezee, na maneno tele tele ya kwamba yeye anauwezoo,,
Leo isiwe sababu ya kunidanganya mimi Ooh na kuniharibia jina langu ehee, to tundu..
Penzi langu la kusuasua..
Nikipata jina aliyeimba na bendi pilizziiii
 
VULI YENI'S MUSIC JOURNEY FROM DAR ES SALAAM TANZANIA TO THE WIDER WORLD

INTERVIEW AT MABOPANE COMMUNITY RADIO STATION


Source : Vuli Yeni
 
10 Mar 2020

NOFA NA NZALA - THE SPARKS

Dedicated to The Sparks of Dar es Salaam Tanzania Traditional Zaramo song arranged by Omari Mgogo with Eddy Sykes, Huluku Mkwela, Salum 'Choggy Sly' Mrisho, , Ibun, Madi, Mwalami, Lameck Ubwe, Jagger, the Sabuni Brothers, Alice Mhuto, Vuli Yeni, Adam Kingui, Mohammed Mdoe, Charlie, Plamba, Lindi Yeni, The Rifters,The Heroes, Nguza & co

Source : Vuli Yeni
 

Twende Afrika Rebelljo


Tanzanian native Joseph Rebello and the Rebelljo Band All the way from Toronto, Canada performing live at the Daressalaam Institute December 31, 2014

Joseph Rebello was born and raised in Tanga, Tanzania where he started his music career. He is the founder of the well-known music group “The Revolution Band” now know as “The Kilimanjaro (Njenje) Band”.

Source : Rebelljo Band
 
13 Jan 2020

ORCHESTRA MKWAWA - WIKIENDI IRINGA MPIGA TUMBA KAKOBE


Mkwawa Jazz Band katika mtindo wao wa Ligija.Bendi hii ilikuwa moja ya bendi mbili za wanafunzi waliokuwa wakisoma Mkwawa High School mkoani Iringa kati ya mwaka 1969 na 1971.

Kila Jumapili mchana bendi hizi mbili ziliporomosha muziki katika mfumo uliojulikana kama bugi, katika ukumbi wa Community Center pale Iringa.

Bugi lilikuwa dansi lililoruhusu wanafunzi na watoto wadogo kufaidi dansi. Dansi lilianza saa nane mchana na kibali cha bugi kiliisha saa kumi na mbili kamili, pombe zilikuwa marufuku wakati wa bugi.

Katika miaka hiyo shule za sekondari nyingi zilikuwa na bendi na bendi hizi nyingine zilikuja kuwa maarufu na hata kuja kutoa wanamuziki maarufu sana. Na kwa kuwa kulikuwa na utaratibu mzuri wanafunzi wengi waliokuwa wanamuziki wakati huo walikuja kuendelea na kuwa watu muhimu katika nyanja mbalimbali kitaifa.

Kwa mfano katika bendi hiyo ya Mkwawa iliyoimba na hata baadae kurekodi wimbo wangu wa leo, wanamuziki wake wote walikuja kuwa watu wenye nafasi muhimu Kitaifa.

Mpiga solo Sewando alikuja kuwa mwalimu wa ‘electronics’ chuo kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) na pia ndie alikuja kuwa mwanzilishi wa bendi ya TZ Brothers.

Sewando ambaye mwanae sasa ni producer maarufu wa muziki wa ‘kizazi kipya’, alianza muziki akiwa Kwiro Secondary ambako nako kulikuwa na bendi iliyowahi kurekodi nyimbo maarufu wakati huo, na hata kuwa chanzo cha baadhi ya mitindo iliyotumiwa na Morogoro Jazz band.

Sewando alianza kupenda electronics wakati huo, na kuwa fundi wa vyombo vya bendi yake ya shule kiasi cha kupata jina la ‘The Mad Scientist’.

Masanja alikuwa mpiga rhythm wakati huo na hatimae alikuja kuwa rubani wa ndege. John Mkama aliyepiga bezi alikuja kuwa mwandishi wa habari mahiri.

Manji aliyepiga rhythm pia alikuja kuwa mhandisi wa ndege, na miaka mchache iliyopita alianzisha bendi iliyoitwa Chikoike Sound, na kwa sasa ana shule nzuri ya muziki Tabata, Dar es Salaam wakati muimbaji Danford Mpumilwa ni mwandishi maarufu, nae pia ndie alikuwa mwanzilishi wa bendi ya Serengeti ya Arusha.

Mpiga tumba katika wimbo huo ni kiongozi maarufu wa dini mwenye wadhifa wa Askofu Mkuu. Hivyo kushiriki katika muziki hakukuwafanya wanamuziki hawa waishie kuwa wahuni au walevi walioharibikiwa kimaisha au kushindwa kuendelea ma masomo.

Bendi ya pili ya Mkwawa Secondary ilikuwa ikipiga muziki wa kizungu na hasa wa mtindo wa soul. Bendi hii iliitwa ‘The Midnight Movers’ ikiwa na wanamuziki kama Kafumba, Martin Mhando. Hans Poppe, Deo Ishengoma, ambao waliohai ni watu wenye nyadhifa muhimu katika jamii. Kuwa mwanamuziki hakukuwa tiketi ya kuwa muhuni.

Kama nilivyosema shule nyingi za sekondari zilikuwa na bendi, pale Dodoma Secondary kulikuwa na bendi kiongozi wa bendi hii alikuwa Patrick Balisidya aliyekuja kuwa mwanamuziki maarufu alipokuja kuanzisha Afro 70.
Source : Habari Trends
 
26 Mar 2021

Tanzania Songa Mbele {Tribute to Magufuli} - UMOJAH BROTHERS GROUP (Official Video)


Tanzania Songa Mbele {Tribute to Magufuli} - UMOJAH BROTHERS GROUP (Official Video) Artists: Innocent Galinoma, Ras Gwandumi, Ras Inno, Ras Mizizi na Pampi Judah Wimbo Maalum Wa Kumbukumbu Ya Rais Wa Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Mh. John Pombe Magufuli (RIP).
Source : Boomshot media
 
Pia kuna Washirika Tanzania Stars Band.....

Bendi hii ilikuwa ikimilikiwa na Jumuiya ya Washirika Tanzania na iliundwa na wanamuziki wengi waliojiengua kutoka Orchestra Vijana Jazz,iliundwa mwaka 1989 na ilikuwa ikitumia mtindo wa Watunjatanjata(Watanzania tuondoe njaa Tanzania) na baadae wakajiita Njata one....

Bendi hii ilikuwa ikifanya maonesho yake katika ukumbi wa 92 Hotel pale Sinza Shekilango...Ilikuwa ni bendi kali hasa na ilikuwa ni tishio kwa bendi zilizotamba enzi zake hasa Vijana Jazz...

Bendi hii ilitamba na nyimbo kama Yaliyopita si ndwele(Nimekusamehe lakini sitokusahau),Washirika,Nelson Mandela,Julie,Penzi la ulaghai,Nimebaki nashangaa,Spare tyre,Maeliza,Gubu la wifi zako,Zuhura,Umbea,Watoto wamekuja juu,Masumanda,Kissa,Kayumba na nyingine kali....

Bendi hii iliundwa na wanamuziki wengi waliojiondo Vijana Jazz kama Hamza Kalala 'Komando',Eddy Sheggy,Mhina Panduka 'Toto Tundu',Adam Bakari 'Sauti ya Zege' bila kuwasahau Abdul Salvador 'Father Kidevu',Emma Mkelo 'Lady Champion',Robert Mabrish,Zahir Ally Zorro,Madaraka Morris 'Kiwembe' ,

Baadae mwaka 1991 baadhi ya wanamuziki wakiongozwa na Hamza Kalala na Eddy Sheggy na kwenda kuunda bendi mbili tofauti za Bantu Group Band(wana Kasimbagu Kahabuka) na MCA International(wana Munisandesa) na wengine(Eddy Sheggy na wenzake) walihamia Bima Lee Orch. wana Magnet Tingisha.....Hiii iliifanya Watunjatanjata itetereke kidogo hadi mwaka 1992 ilipompata mtaalam Zahir Ally Zorry ambaye aliifanya ikabaki imara na mtindo wa Watunjatanjata waliouboresha na kuwa Njata One wakiwa na nyimbo kama Gubu la Wifi zako,Maeliza,Zuhura na Umbea
Mkuu Balantanda nahitaji sana wimbo mmoja wa zamani chorus yake inaimbwa hivi
"Kifo cha baba jamaniii,hakitatutoka moyonii,kwa kumpata hatumuonii tutakaye muuliza ni nani eeh...." nijulishe hao walikuwa bendi gani,na wimbo nautaka sana! Yamenikuta
 
9 Jan 2021

Karama Regesu - " L'amour "



Mwanamuziki huyo mkongwe alisema kwamba yeye ni mwanamuziki wa siku nyingi, kaanza sanaa ya muziki mwaka 1985.

Karama Regesu kwa mara nyingine tena mwaka 2021 anakuja na "L'amour". Hiki ni kibao chake kingine kipya kilichopo kwenye mtindo wa Runbas. Ni mategemeo yetu kuwa kibao hiki kitakuburudisha na kukidhi kiu yako.
Source: Karama Regesu
 

KASHEBA AND ZAITA MUSICA (live): NIMPENDE NANI NDALA


Tanzania music WAS LIVE AND GREAT DURING THIS ERA. KASHEBA AND HIS MUSICIANS CALLED THEIR BAND ZAITA MUSICA, ZAITA stood for ZAIRE TANZANIA
Source : zama zilie
 
LUCKY DUBE LIVE



Lead vocal : Lucky Dube
Keyboards: Thuthukani Cele
Keyboards: Eugene Mthethwa
Percussion : Chris Dlamini
Saxophone: Vulindela (Vuli) Yeni
Trombone: Robert Jabu Mdluli
Trumpet: Ndumiso Nyovane
Guitar Bass: Jabulani Sibumbe
Lead Guitar: Sandile Dhlamini
Drums: Isaac Mtshali
Backing Vocalsa: Nolusindiso Gaeza, Cynthia Malope, Kabanina Ntsele
Manager: Richard Siluma
 
Back
Top Bottom