Ziito Kabwe ameongea ukweli mchungu

Binafsi simkubali kabisa huyu bwana na ni bora tu muda wake uishe aondoke madarakani na ikiwezekana aondoke yeye na CCM yake yote waje watu wengine watuongoze.
 
Wia ini ze raiti traki.

Hamjajua tu jinsi watumishi wanamhujumu huyu Pogba Kwa kuwakandamiza haki zao.Wapo kimya kama wameridhika vile
 
Mi nilishasema ni danganya toto haiwezeakani kwa muda mchache kodi ipande ghafla gafla alafu eti uje kusema kuna mlolongo ni mwingi wa ulipaji kodi inabidi tukae tuupunguze alafu kodi ishuke tena wakati anasema hivyo ni yule anaesisitiza watu walipe kodi ili tufanye maendeleo ya nchi uchumi ukue
 
BIASHARA ndio njia pekee ya kukufanya ulinde na kuongeza mtaji wako. Mara nyingi Kufunga Biashara sio kulinda mtaji bali kuupunguza kupitia matumizi.
Wengi hawafungi bali wanabadili na wapo wachache wanaohamisha biashara zao.
Dhana ya wapiga deal ni sahihi kwa zaidi ya 50%..
Hakuna mfanyabiadhara mwaminifu..
Wenyewe wamekiri kutoa rushwa japo wanasababu..
Rais amekuja na ushahid wa makampuni 17000 ya kitapeli.
Wako wenye mauzo bilion wao huonyesha milion 20.
Wako kina Kaluwa wazee wa ganji la bilion 4
Hawa wakifunga kwa nini tusiseme ni wapiga deal
 
Ndiyo matatizo ya kumsukumizia mwendawazimu Ikulu. Na kama ulivyosema na bado, kwani hali ya uchumi ni mbaya sana na mapato ya kodi yanazidi kushuka. Fagio la chuma kwa wafanyakazi wa Serikali liko njiani na sijui kama kutakuwa na pesa za kugharamia uchaguzi mwakani.

 
Duh hilo la kodi za wafanyakazi kushuka hadi kwa kiwango cha 500bilion ni hatari sana, maana yake tumepoteza watu wengi sana kutoka ajira rasmini. Kwa hali tuwe makini sana na data zetu za makusanyo pale TRA..

Kuna viashiria vinaonyesha mambo hayako sawa, lakini tatizo la watanzania wengi ni kuwa wapenzi wa vyama na si kuishi kwa uhalisia, Unawezaje kusema unakusanya kodi ya kutosha huku kila siku tunabadirisha makamishina wa TRA, unawezaje kujisifia kwenye makusanyo huku mamia ya watu wametoka kwenye ajira rasmi na hakuna ajira mpya zilizozarishwa? Unawezaje kujisifia kwenye makusanyo huku kumbe kuna matatizo makubwa na watu wanafunga biashara??
 
Swaga ya "wapiga deal iko wapi"?
Eti nini Zitto anasema? Anasema ''Njia ya uhakika kurejesha Uchumi wetu kwenye Reli sahihi ni kufanya MABADILIKO''. Hivi jamani uchumi wetu ulishakuwa kwenye reli sahihi ili tuurejeshe? Anakumbuka kipindi cha Kikwete alichokuwa anafaidi ndiyo anakiita ''uchumi ulikuwa kwenye reli sahihi''. Huu ni upumbavu na ubinafsi wa hali ya juu. Wanasiasa wa aina hii walaaniwe kwani wanajifikiria wao tu! Kweli kile kipindi cha Kikwete ambacho kila mtu alikuwa anaachiwa kuiba na kufanya hujuma atakavyo ndiyo anasema tulikuwa kwenye reli sahihi?
 
Mbona ndugu migebuka ameshindwa kutwambie kama tusipo muongezea Magufuli siku ikulu nani tumpe?
MKEO AU MMEO AKIKUSHINDA KTK NDOA UTACHUKUA HATUA MBALIMBALI IKIWAMO KUMUONYA , KUMKUMBUSHA WAJIBU WAKE N.K NA IKITOKEA AKASHINDIKANA BASI JIBU NI KUMPIGA CHINI, HIVYO ZITO YUPO SAHIHI LAZIMA NDULI AKAE BENCHI
 
KWANI AMETAJA KIPINDI CHA KIKWETE KTK HOJA YAKE? KWANI NI KIPINDI KIPI UCHUMI ULIWAHI KUWA MCHAFU KAMA AWAU HII?
 
Hayo ya wizi umeyatoa wapi?Kichwani kwako ila sio kwenye maneno ya Zitto!Anazungumzia wastani mzuri wa kukua kwa uchumi,kwa sasa tumeanguka vibaya mno!Ni suala la namba tu ambazo zinareflect uhalisia!
Hayo ya wizi yakwako!
 
We
We akili yako iko tenge ntakuuliza swali la ki layman kwani wewe unataka usifaidi uchumi ukinawili? Mbona unaongea kama mlozi?
 
Zito Kabwe njoo na ngonjera zako za bandari ya bagamoyo.

Mnahongwa pesa mtetee ujinga na ufisadi
Watanzania tumerogwa, siyo bure!
Zito Kabwe atahongwa na nani kutetea Bandari ya Bagamoyo? Haiingii kwenye kikao chochote cha maamuzi. Wanaoingia ni MAKADA WA CCM, ambao ndiyo wameingia mikataba yote ya hovyo tangia awamu ya pili.
Kwa hiyo kama yupo wa kumhonga Zito Kabwe, basi ni wale MAKADA WA CCM, walioingia makubaliano ya kifisadi kuhusu Bandari ya Bagamoyo.
Ukweli mchungu ndiyo huu: CCM NI JANGA LA KITAIFA.
Wanaoitetea wote ni WASALITI Wa Taifa letu!
 
Hayo ya wizi umeyatoa wapi?Kichwani kwako ila sio kwenye maneno ya Zitto!Anazungumzia wastani mzuri wa kukua kwa uchumi,kwa sasa tumeanguka vibaya mno!Ni suala la namba tu ambazo zinareflect uhalisia!
Hayo ya wizi yakwako!
Afu cha ajabu yaani awa jamaa wa awamu hii sijui wanamdanganya nani kwamba hawaibi,kwa taarifa yako wizi ni kama wote hivi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…