Ziara ya Ghafla ya Boss wa Vodacom Kipindi cha Michezo EFM chamfanya Mtangazaji Maulid Kitenge 'ajing'ateng'ate' katika kuongea Kiingereza

MINOCYCLINE

JF-Expert Member
Apr 2, 2015
8,011
16,748
Picha lilianza pale Boss huyo alipoingia Studioni ghafla baada ya Kupendezwa na Majadiliano ya Kiswahili yaliyokuwa yakiendelea baina ya Wachambuzi na Watangazaji.

Kabla Boss huyo hajaingia Mtangazaji Maulid Kitenge alikuwa ni Mchangamfu sana ila alipoingia Boss huyo wa Vodacom na kugundua hazungumzi Kiswahili na anazungumza Kiiingereza Pumzi ya Kitenge ilishuka ghafla, akawa hana Raha na anajiumauma pengine hata akitaka Ardhi ipasuke akajifiche Kwanza.

Pongezi nyingi sana ziende kwa Mtangazaji na sasa Mchambuzi Ibrahim Masoud 'Maestro' na Mchambuzi Bora kwa sasa wa Michezo nchini Jemedari Said ambao walikuwa Comfortable katika Kukizungumza Kiiingereza na Mgeni Boss huyo wa Vodacom huku Maulid Kitenge akiendelea Kujiumauma tu na Kutetemeka.

Kiingereza pekee alichokimudu Mtangazaji Maulid Kitenge ambacho nacho alikitafuta mno ni Kumuuliza tu Mgeni (Boss huyo wa Vodacom) kuwa are you Simba or Yanga huku akitetemeka na Jasho la mbali Kumtoka japo Studioni Kwao 24/7 ni Full AC.

Hakika waliosema kuwa Kukaa karibia na Mahakama siyo Kujua Sheria na hivyo hivyo Kusafiri kila Siku Ulaya na Marekani siyo Kujua/ Kujijua Kiingereza.

Uchangamfu wa Mtangazaji Maulid Kitenge ulirejea rasmi pale Boss huyo wa Vodacom alipoaga (alipowaaga) ambapo Muoga wa Taifa wa Lugha ya Kiingereza ambacho pia hakijui Mtangazaji Maulid Kitenge alimuaga kwa haraka huku akifurahia na huenda hata Kimoyomoyo alikuwa anaomba Jamaa aondoke kwani angemchoresha kwa Wasikilizaji kuwa ni kweli hakijui Kiingereza japo Kutwa anaenda kwa Wanaokijua.
 
Mauldi Baraka wa Kitenge hana elimu ya utangazaji hajui kbs kbs kiingereza, kuna bandiko liliwekwa humu kuhoji na kudadisi elimu ya Kitenge.

Maulid ni sungura mjanja hana elimu kbs na kiingereza ndio hajui kbs. Ni vigumu kumtenganisha kitenge na Mbwiga.
 
Lugha ni kipaji,ufundi na uelewa.Lugha hasa kiingereza inataka utundu.Usimcheke.😂😂😂😂
Ni Uwendawazimu na Aibu kutwa uko Marekani na Ulaya na bado Kiingereza kinakupiga Chenga na unaogopa hata Kukiongea ukikutana Wanaokijua na Waliozaliwa nacho.

Mwambieni aache Sifa za Kijinga na Ushamba wake mwingi ambao Sometimes huwa Unamchoresha na Watu Wanamsanifu tu huku Yeye akidhani Wanamkubali.
 
Ni Uwendawazimu na Aibu kutwa uko Marekani na Ulaya na bado Kiingereza kinakupiga Chenga na unaogopa hata Kukiongea ukikutana Wanaokijua na Waliozaliwa nacho.

Mwambieni aache Sifa za Kijinga na Ushamba wake mwingi ambao Sometimes huwa Unamchoresha na Watu Wanamsanifu tu huku Yeye akidhani Wanamkubali.
Kashindwa hata kumtafuta RAS SIMBA kweli amfundishe Kiingereza? Asilimia 80 ya watangazaji hawa wa mpira ni weupe sana kuhoji kwa Kiingereza fuatilia sana mahojiano ya watangazaji wa Azam kwa kocha wa kigeni utajionea vumbi tu. Weupe sana.
 
Back
Top Bottom