M-bongotz
JF-Expert Member
- Jan 7, 2010
- 1,734
- 405
Nionavyo mie kumpa mama huyu mapokezi na heshima zote hizo ni si sahihi,yeye ni nani?, tulimchagua mume wake na wala sio yeye sasa hili la kupewa heshima kama mungu mtu linatoka wapi, nae eti anatuweka barabarani kwenye foleni kumsubiri apite jamani nchi hii maskini hivi badala ya watu kuwahi kwenye vibarua vyao tunapotezewa muda kusubiri eti "first lady apite", first lady wa nani?, kila mtu ana first lady wake nyumbani yule ambae walikula kiapo cha "kwa shida na raha", nashangaa sana ingawaje ni utaratibu kwenye nchi nyingi kuwaheshimu wamama hawa lakini hiyo haitunyimi nafasi ya kutafakari uhalali wa cheo hiki na benefits zake, unaweza kujiuliza kwanini alipwe, kwanini safari zake zigharamiwe na kodi za wavuja jasho, wakati hakuna sheria inayoestablish hiki cheo wala kumfanya mwenye cheo hiki kuwa mmoja wa viongozi wa nchi hii..sisi tuliwachagua Rais na Makamu wa Rais, mbona Bi. Mwanamwema Shein yeye hapati privileges kama hizi?