Sijaona zembwela alipokosea.Mbunge na diwani kazi yao ni kusimamia serikali.Kama wameshindwa Kusimamia serikali kwa nini wasiwajibishwe?Kuna wabunge na madiwani wanaotimiza wajibu wao huo nakini serikali ikawa kichwa ngumu kwa hao watu wanajua.Watu wajua viongozi wanaowajibika na wale wasiowajibika.
...mkuu si kila wakati wajinga ndo waliwao,wakati mpaka sasa watanzania tunanyonywa tu wote kwa pamoja wajinga na werevu na tumeshindwa kulikomboa taifa,wakati mwingine huwa nadhani waerevu ndo waliwao maana ukiwashawishi 1+1=11 wakaamini basi utawatawala hata miaka 50 ilimradi uwambie kesho utawafundisha ulivyopata jibu la 11,watasubiri kwa matumiani makubwa...
Ni kweli kbs Zembwela anatatizo la kutojua pillars of the gvt na mipaka yake kiutendaji. Kipindi cha Super mix kinachorushwa hewani kuanzia saa 3 hadi 7 mchana EA RADIO kilikuwa more logical akiwepo Michael Baruti kwani yeye aliweza hata kumbishia Zembwela pale alipoona kunaombwe fulani la ufahamu!
Ni vizuri ungeangalia kama alisema Chuo cha uandishi wa habari!Nimefuatilia kwa muda mtazamo wa huyu mwanahabari zembwela na nimegundua kunamambo hafikirii sawa. Kwa mtazamo wake ni kwamba mbunge na diwani ndo mwenye dhamana ya maendeleo ya jimbo. Sitaki kuhoji kiwango chake cha elimu,lakini kwa mtu mwenye ufahamu unajua nani anawajibika kuleta maendeleo na nani anapaswa kupeleka vipaumbele vya wananchi husika. Bwana mdogo zembwela nadhani unapaswa kuwaunganisha vijana kuishinikiza serikali kutimiza yale mliyowatuma wabunge wenu wakayapeleke serikalini kwa kutengewa bajeti na utekelezaji. Lakini ukiendelea kuwaaminisha watu uzembe wa serikali ni wa mbunge unakosea. Sote tunawajua wabunge wawajibikaji na wazembe na lazima tuwawajibishe,lakini hujuma za serikali kwa baadhi ya wabunge kuwafanya hawawajibiki ndo kumezaa mfuko wa jimbo. Sasa wabunge wakiwa watendaji nani ataisimamia serikali ? Mwisho nilistuka na kuogopa zembwela alipowahamasisha wananchi kumng'oa diwani bila uchaguzi eti hawawezi kusubiri uchaguzi wakati anachelewesha maendeleo. Nahisi sheria ya uchaguzi haijui. Amekomaa na azimio la arusha bila kujua kuna azimio la zanzibar wameleta ccm.
sio Clausi fm ni Blauzi fm.
Nitawashangaa sana watakaopitisha hii sera hati mbunge/diwani anaweza kuondolewa katikati ya kipindi chake kwa sababu tu ameshindwa kuleta maendeleo au hata kwa sababu zilizoorodheshwa ndani ya Rasimu ya Katiba! Kama Tunataka vurugu turuhusu kipengele hicho kipite tuone. Wanaotetea hawajafikiri nje ya emotions zao!...that is my point,zembwela nimemsikia marakadhaa anasema mbunge kama hajafanya alichoahidi kuwaletea wampige chini bila kujali kama tatizo lipo kwenye uwajibikaji wa mbunge au serikali ndo mzigo. Mfano kule jimboni kwa marehemu mgimwa miaka yote hawajapata maji si kwakuwa mbunge hakufuatilia bali ni ubovu wa sera na vipaumbele vya serikali. Tukiacha ieleweke hivo serikali inaweza kuhujumu majimbo ya wabunge isiyowataka na kusingizia hawafai....
Kwa maneno mengine ni kuwa kiunganishi cha wananchi na serikali yao ni Mbunge ama Diwani. Hivyo basi iwapo Mbunge ama Diwani anashindwa kuwabana watekelezaji ni nani hapo anayepaswa kulaumiwa?...my point is,mbunge na diwani ndo wanapaswa kuwajibika kama mambo waliyowatuma hayajatimizwa...?je mbunge/diwani ndo mtekelezaji wa vipaumbele vya wananchi ?...
Kwa maneno mengine ni kuwa kiunganishi cha wananchi na serikali yao ni Mbunge ama Diwani. Hivyo basi iwapo Mbunge ama Diwani anashindwa kuwabana watekelezaji ni nani hapo anayepaswa kulaumiwa?
Inajulikana wazi kuwa Mbunge au Diwani sio mtendaji, ila hao watendaji na kurugenzi yake wapo kuwatumikia hao wabunge na madiwani ambao ndio wanawakilisha kero za jamii katika asasi husika! Hivyo kwa namna moja ama nyingine wanapaswa kubeba lawama iwapo watashindwa kuondoa kero katika jamii husika pasipo sababu ya msingi...
mkuu naomba unisaidie,hivi hii sera ya kutoa ahadi pale mtu anapotafuta kuchaguliwa badala ya kueleza Yale aliyokwisha kufanyia nchi au kundi analotaka limchague ilianza lini na wapi ilianzia?...that is my point,zembwela nimemsikia marakadhaa anasema mbunge kama hajafanya alichoahidi kuwaletea wampige chini bila kujali kama tatizo lipo kwenye uwajibikaji wa mbunge au serikali ndo mzigo. Mfano kule jimboni kwa marehemu mgimwa miaka yote hawajapata maji si kwakuwa mbunge hakufuatilia bali ni ubovu wa sera na vipaumbele vya serikali. Tukiacha ieleweke hivo serikali inaweza kuhujumu majimbo ya wabunge isiyowataka na kusingizia hawafai....
Zembwela ndo Nani?
Kila Mtu Ana Mapungufu Yake, Mi Naona Ni Bora Zembwera Kuliko Akina Mchomvu Na Kibonde Wa Blauzi Ya Fm
Hebu twambie kazi ya mbunge na diwani ni nini?!Zembwela no Comedian sasa sijui ya uana habar kaitoa wapi.
No wonder fani ya uana habari ina dharauliwa sana.
Hebu twambie kazi ya mbunge na diwani ni nini?!
Jimbo linapokosa maendeleo nani wa kwanza kuulizwa?
Wabunge na madiwani wanachaguliwa na wananchi ili kusaidia kuimiza serikali kuleta maendeleo na wanapo shindwa wao ndio wa kwanza kulaumiwa ?
Hivi unafikiri wamechaguliwa kuuza sura?
Zembwela yuko sahihi kabisa sema mleta mada ni mvivu?
Hivi unafikiri kwa nini wakazi wa ubunge wana mlaumu John mnyika kwenye swala la maji?
Hivi unafikiri kwanini John Mnyika alitoa ahadi ya kuwapatia Maji akipewa ubunge?
Mkuu umewapa somo zuri! Zembwela is right!Kwa maneno mengine ni kuwa kiunganishi cha wananchi na serikali yao ni Mbunge ama Diwani. Hivyo basi iwapo Mbunge ama Diwani anashindwa kuwabana watekelezaji ni nani hapo anayepaswa kulaumiwa?
Inajulikana wazi kuwa Mbunge au Diwani sio mtendaji, ila hao watendaji na kurugenzi yake wapo kuwatumikia hao wabunge na madiwani ambao ndio wanawakilisha kero za jamii katika asasi husika! Hivyo kwa namna moja ama nyingine wanapaswa kubeba lawama iwapo watashindwa kuondoa kero katika jamii husika pasipo sababu ya msingi...
Ni mwenyekiti wa actZembwela ndo Nani?
ni vizuri ungempigia simu katika kipindi chake na ukatoa ufafanuzi ili uwe umewasaidia na watanzania wengine,pengine haelewi ndio maana anasema hivyo au lah.
Acha kupanic huo Mfano nimeutoa kuoonesha kuwa Zembwela yuko sawa na Kazi ya mbunge ni kuhishinikiza serikali kuahakikisha maendeleo yana patikana na hakishindwa yeye ndiye wa kwanza kupewa lawama!Hiyo ahadi Mnyika alikuahidi wewe.
Sisi wakazi wa Ubungo Mnyika alituahidi kusimamia show suala la upatikanaji wa maji,an thats what exactly the guy is doing.
Ma Intarahamwe yanakwamisha juhudi zake ili kumkosanisha na wana nchi