Zembwela acha upotoshaji...!

Zembwela acha upotoshaji...!

Nimefuatilia kwa muda mtazamo wa huyu mwanahabari zembwela na nimegundua kunamambo hafikirii sawa. Kwa mtazamo wake ni kwamba mbunge na diwani ndo mwenye dhamana ya maendeleo ya jimbo. Sitaki kuhoji kiwango chake cha elimu,lakini kwa mtu mwenye ufahamu unajua nani anawajibika kuleta maendeleo na nani anapaswa kupeleka vipaumbele vya wananchi husika. Bwana mdogo zembwela nadhani unapaswa kuwaunganisha vijana kuishinikiza serikali kutimiza yale mliyowatuma wabunge wenu wakayapeleke serikalini kwa kutengewa bajeti na utekelezaji. Lakini ukiendelea kuwaaminisha watu uzembe wa serikali ni wa mbunge unakosea. Sote tunawajua wabunge wawajibikaji na wazembe na lazima tuwawajibishe,lakini hujuma za serikali kwa baadhi ya wabunge kuwafanya hawawajibiki ndo kumezaa mfuko wa jimbo. Sasa wabunge wakiwa watendaji nani ataisimamia serikali ? Mwisho nilistuka na kuogopa zembwela alipowahamasisha wananchi kumng'oa diwani bila uchaguzi eti hawawezi kusubiri uchaguzi wakati anachelewesha maendeleo. Nahisi sheria ya uchaguzi haijui. Amekomaa na azimio la arusha bila kujua kuna azimio la zanzibar wameleta ccm.
Kumbe wewe ni mshabiki wa Azimio lá Zanzibar, lilioua Azimio la Arusha?

Hivi una maana wewe hujui kuwa hata ufisadi mbalimbali unaoendelea nchini, kama vile EPA, Escrow account, skandali ya rada, ufichwaji wa matrilioni, kwenye mabenki ya Uswisi, ni matokeo ya kuliua Azimio la Arusha.

Bila shaka wewe unaolipigia debe Azimio la Zanzibar, utakuwa miongoni wa beneficiaries, wa mfumo wa nchi yetu wa kulea mafisadi, na ndiyo maana hata Presidaa wako, alitoa 'msamaha' kwa majambazi yalioiba mabilioni ya EPA, na kuwaambia, warejeshe tu hayo mapesa waliyokwapua, ili soo iishe!!
 
Eti Hutaki Kuhoji Elimu Yake Wakati Ndo Umeshahoji Tayari

...hahahaa mkuu mahoro nilimaanisha huenda kiwango cha elimu kinachangia lakini sidhani kama ni sababu ya poor analytical skill to that level...
 
Lakini Katiba Si Inamruhusu?? Hongera Wewe Unaejua Kila Kitu, Mbna Hata Rais Wako Huwa Anaongea Kama Leyman

sina tatizo na uhuru wa kuongea ila kwenye redio na unasikilizwa na watu wengi ni vema ukaongea unachokijua. kuliko usichojua usipotoshe umma nao wakaamini maelezo yasiyo sahihi
 
Usijifanye Huelewi? Kaandika Hivo Makusudi Na Nafahamu Hata Wewe Ushaelewa Labda Kama Kichwa Chako Kimejaa Makamasi Tu
Kuwasaidia tu, yeye anasikia clausi fm! Ila ni Clouds fm. Punguza jazba mkuu.
 
Kumbe wewe ni mshabiki wa Azimio lá Zanzibar, lilioua Azimio la Arusha?

Hivi una maana wewe hujui kuwa hata ufisadi mbalimbali unaoendelea nchini, kama vile EPA, Escrow account, skandali ya rada, ufichwaji wa matrilioni, kwenye mabenki ya Uswisi, ni matokeo ya kuliua Azimio la Arusha.

Bila shaka wewe unaolipigia debe Azimio la Zanzibar, utakuwa miongoni wa beneficiaries, wa mfumo wa nchi yetu wa kulea mafisadi, na ndiyo maana hata Presidaa wako, alitoa 'msamaha' kwa majambazi yalioiba mabilioni ya EPA, na kuwaambia, warejeshe tu hayo mapesa waliyokwapua, ili soo iishe!!

...mkuu hukunielewa kwanini nimetaja azimio la zenj,ni kwamba huwezi kutumia sheria ya mwaka 1977 wakati imeshafanyiwa amendments mwaka 2000. Huwezi kuwambia wanasiasa waishi kwa azimio la arusha wakati la zanzibar limewapa uhuru wa kuvunja azimio la arusha. My point is zembwe achambue mambo katika uhalisia wake na si ktk kufikirika...
 
"MKINICHAGUA MIMI" Nitahakikisha zahanati inajengwa na tunapata dawa.
Wazazi hamtatozwa michango ya madawati.
Soko la kahawa litapatikana nje ya nchi.
Tatizo la maji litakwisha. Nisisahau umeme.
Kwa kauli hii nani anastahili kuleta maendeleo kwa wananchi. Mr Politician anaona ahadi alizotoa hazijatekelezeka anataka kutuaminisha kuwa sio yeye aliyetoa ahadi.
WAJINGA NDIO WALIWAO
 
Lakini Zembwela taaluma yake ni mchekeshaji na hivyo mengi huwa anaongea radioni nafikiri kwa lengo la kuwavunja watu mbavu..
 
Nimefuatilia kwa muda mtazamo wa huyu mwanahabari zembwela na nimegundua kunamambo hafikirii sawa. Kwa mtazamo wake ni kwamba mbunge na diwani ndo mwenye dhamana ya maendeleo ya jimbo. Sitaki kuhoji kiwango chake cha elimu,lakini kwa mtu mwenye ufahamu unajua nani anawajibika kuleta maendeleo na nani anapaswa kupeleka vipaumbele vya wananchi husika. Bwana mdogo zembwela nadhani unapaswa kuwaunganisha vijana kuishinikiza serikali kutimiza yale mliyowatuma wabunge wenu wakayapeleke serikalini kwa kutengewa bajeti na utekelezaji. Lakini ukiendelea kuwaaminisha watu uzembe wa serikali ni wa mbunge unakosea. Sote tunawajua wabunge wawajibikaji na wazembe na lazima tuwawajibishe,lakini hujuma za serikali kwa baadhi ya wabunge kuwafanya hawawajibiki ndo kumezaa mfuko wa jimbo. Sasa wabunge wakiwa watendaji nani ataisimamia serikali ? Mwisho nilistuka na kuogopa zembwela alipowahamasisha wananchi kumng'oa diwani bila uchaguzi eti hawawezi kusubiri uchaguzi wakati anachelewesha maendeleo. Nahisi sheria ya uchaguzi haijui. Amekomaa na azimio la arusha bila kujua kuna azimio la zanzibar wameleta ccm.
Mkuu huyu futilia mbali kwanza siyo mwandishi bali unprofessional comedian,uwezo wake wa kufikiri ndo umefikia kikomo au beyond repair.Kuendelea kumjadili ni sawa na kujadili kitendo cha mtoto wa mwezi mmoja kukojoa kitandani.Kingine mmbovu zaidi ni mwajiri wake kwani hata waandishio wa magazeti wanakuwa na mhariri anayepitia habari kabla hawajairusha.Au labda anatokea kile chama cha siasa ambacho takwimu inaonesha wamesheheni wenye elimu na uelewa duni.

 
halafu anajifanya hajihusishi na vyama vya siasa lakini kauli na mwenendo wake unamuonyesha wazi kwamba anaunga mkono c ic.em , naomba kuchukua nafasi hii kumuonya ndugu zembwera aache kutumia redio ya watu kupotosha jamii , hasa kwenye masuala ya siasa , hayajui .
 
vijana wengi mtu akiwa mlengo wa kati hatumpendi kwasababu hapendelei yoyote.mnapenda zembwela awasifu madiwani weni waliofeli kuibana serikali ili wananchi wapate maendeleo.mnaanza kumlaumu.au mnapenda zembwela aseme madiwani wa ccm wazuri na madiwani wa cdm wabaya?au unapenda aseme madiwani wa cdm wanafanya kazi vizuri wakati nao wameingia madarakani hawana wanalofanya katika kata zao
 
...kweli mkuu wale wa claus ni utumbo,ila zembwe hawezi kutofautisha majukumu ya mbunge na serikali,na hayuko huru kusema kweli serikali inapoboronga...

Nakuelewesha tu, siyo Claus ni Clouds fm.
 
...mkuu hukunielewa kwanini nimetaja azimio la zenj,ni kwamba huwezi kutumia sheria ya mwaka 1977 wakati imeshafanyiwa amendments mwaka 2000. Huwezi kuwambia wanasiasa waishi kwa azimio la arusha wakati la zanzibar limewapa uhuru wa kuvunja azimio la arusha. My point is zembwe achambue mambo katika uhalisia wake na si ktk kufikirika...

samahini, hivi azimio la arusha lilikuwa kwa ajili ya tanganika au tanzania? Na azimio la zanzibar ni kwa ajili ya zanzibar au? Maana zanzibar ni nchi inayojiendesha kwa katiba yake na serikali yake
 
Hata mimi nilikuwa mfuatiliaji sana wa vipindi vya super mix ila sasa hivi nlishaacha kama nlivyoacha kusikiliza clouds. Mimi ni RFA nikibadili ni radio one. Jamaa ni mweupe sana kichwani
 
Umetumwa na mawingu fm

...mkuu hoja zote nilizogusa ni juu ya namna na upeo wa uchambuzi wa mambo ya siasa. Hata angekuwa anafanyakazi uhuru media,itv au tanzania daima bado ningemkosoa tu.infact mawingu fm kama ulivyoita ni among the stations ambazo hata kuzisikiliza naona aibu kwa utumbo wao....
 
Back
Top Bottom