Fundi Mchundo
Platinum Member
- Nov 9, 2007
- 8,940
- 6,854
HEbu gonga hapa. MZALENDO.NET-Zanzibar na zama za ukweli na uwazi!
Wazanzibar asilimia kubwa hawapendi muungano, harafu wanawachukia watanganyika sana. Pili kufanya hiyo patisheni ni rahisi. Tatizo liko kwa viongozi wetu ukifanya hiyo kitu kwa upande wa bara unaitwa MHAINI. Na ndicho hasa wazanzibar wanakua na nguvu ya kusema kwa nini twa ng'ang'ania kama hatufaidiki na visiwa vile.?
Hiyo Mzalendo-Net takriban watu hamsini ( sasa hivi wako 28,wageni 26 na wanachama 2!) ndiyo wanaochangia, wengi wao kutoka ughaibuni! Kama unadhani sentiments zilizomo mle ndiyo zinazo-reflect hisia za wazanzibari wote utakuwa umekosea sana. Bara tatizo letu ni self-sensorship. Hakuna mtu atakayefungwa kwa kudai mjadala juu ya Muungano. Humo ndipo iingizwe hoja ya umuhimu na ulazima wake. Kitu ambacho wazanzibari wanatupatia ni kuwa hakuna kiongozi wa bara ambaye yuko tayari kusimamia haki za watu wa bara ndani ya Muungano. Hakuna anayesema wazi kuhusu kero zinazoipata bara kutokana na Muungano. Wameachia mjadala mzima utekwe na watu wachache kutoka Zanzibar kiasi cha kuwaaminisha kuwa wanawaogopa! Kwa hali hiyo wataendelea kutingisha kiberiti mpaka tutakapojikuta watupu, haki zote wamechukua wazanzibari!
Amandla.......