Zanzibar Wants Union Constitution Overhauled

HEbu gonga hapa. MZALENDO.NET-Zanzibar na zama za ukweli na uwazi!
Wazanzibar asilimia kubwa hawapendi muungano, harafu wanawachukia watanganyika sana. Pili kufanya hiyo patisheni ni rahisi. Tatizo liko kwa viongozi wetu ukifanya hiyo kitu kwa upande wa bara unaitwa MHAINI. Na ndicho hasa wazanzibar wanakua na nguvu ya kusema kwa nini twa ng'ang'ania kama hatufaidiki na visiwa vile.?

Hiyo Mzalendo-Net takriban watu hamsini ( sasa hivi wako 28,wageni 26 na wanachama 2!) ndiyo wanaochangia, wengi wao kutoka ughaibuni! Kama unadhani sentiments zilizomo mle ndiyo zinazo-reflect hisia za wazanzibari wote utakuwa umekosea sana. Bara tatizo letu ni self-sensorship. Hakuna mtu atakayefungwa kwa kudai mjadala juu ya Muungano. Humo ndipo iingizwe hoja ya umuhimu na ulazima wake. Kitu ambacho wazanzibari wanatupatia ni kuwa hakuna kiongozi wa bara ambaye yuko tayari kusimamia haki za watu wa bara ndani ya Muungano. Hakuna anayesema wazi kuhusu kero zinazoipata bara kutokana na Muungano. Wameachia mjadala mzima utekwe na watu wachache kutoka Zanzibar kiasi cha kuwaaminisha kuwa wanawaogopa! Kwa hali hiyo wataendelea kutingisha kiberiti mpaka tutakapojikuta watupu, haki zote wamechukua wazanzibari!

Amandla.......
 
Hiyo Mzalendo-Net takriban watu hamsini ( sasa hivi wako 28,wageni 26 na wanachama 2!) ndiyo wanaochangia, wengi wao kutoka ughaibuni! Kama unadhani sentiments zilizomo mle ndiyo zinazo-reflect hisia za wazanzibari wote utakuwa umekosea sana. Bara tatizo letu ni self-sensorship. Hakuna mtu atakayefungwa kwa kudai mjadala juu ya Muungano. Humo ndipo iingizwe hoja ya umuhimu na ulazima wake. Kitu ambacho wazanzibari wanatupatia ni kuwa hakuna kiongozi wa bara ambaye yuko tayari kusimamia haki za watu wa bara ndani ya Muungano. Hakuna anayesema wazi kuhusu kero zinazoipata bara kutokana na Muungano. Wameachia mjadala mzima utekwe na watu wachache kutoka Zanzibar kiasi cha kuwaaminisha kuwa wanawaogopa! Kwa hali hiyo wataendelea kutingisha kiberiti mpaka tutakapojikuta watupu, haki zote wamechukua wazanzibari!

Amandla.......


Ni kweli unachoongea
Lakini wazanzibar hawautaki muungano, nimekua nao wengi ktk zile biashara za mashua kule bagamoyo, tena ni watu ambao wa chini kabisa. Naamini kule kura ya maoni ikipigwa kuhusu muungano ile ya wasiotaka muungano itapita kwa kishindo.

Tatizo linalowasumbua sana kuona kama Zanzibar ndo inaibeba bara, kwanini wabara wanang'ang'ania sana muungano? kwa mtu mwenye akili ya kawida akiwa upande wa zanzibar lazima hisia kama waliyonayo itamgusa.

Mimi ninavyoelewa na ninavyofikiri WABARA hawazungumzi sana kuhusu muungano kwa sababu impact ya Zanzibar kwa watanganyika ni ndogo sana ama haipo kabisa nikiwa na maana iwemo ktk muungano na isiwemo ktk muungano yote ni sawa. Ninachofikiri kwa upande mwingine WABARA hasa watanganyika wanapenda sana jina TANZANIA na ndilo pekee wanahofu ya kulipoteza.
 
Mkamap,
Tunaweza kuendelea na jina la Tanzania hata baada ya Zanzibar kujitenga. It has a nice ring to it.
 
Mkamap,
Tunaweza kuendelea na jina la Tanzania hata baada ya Zanzibar kujitenga. It has a nice ring to it.

Ninavyofikiri nami ni hivyo ni kuondoa neno muungano tu. Lakini ninavyofikiri, pia wazanzibari bado watapinga hilo. Watawalazimisha muitwe Watanganyika maana bila kuitwa watanganyika hawatarizika.
 
Ninavyofikiri nami ni hivyo ni kuondoa neno muungano tu. Lakini ninavyofikiri, pia wazanzibari bado watapinga hilo. Watawalazimisha muitwe Watanganyika maana bila kuitwa watanganyika hawatarizika.
Kwani wao ndio waliotubatiza? Watatuamulia mpaka na chupi tunazovaa?
 
Mnaposema WaZanzibari hawautaki Muungano hapo mtakuwa mnakosea na kwa lugha ya kileo mtakuwa mnapoteza dira. Zanzibar wamefanya mabadiliko makubwa sana na hawakuogopa mtu ,au chama chochote kile.

Bunge la tanzania haswa hawa WaTanganyika wanakuwa na matatizo ya kiuamuzi na wanakuwa na jazba ,aidha wanakuwa na chuki za kidini au kibinafsi au wanakuwa na choyo flaniflani ,hivi ni wangapi wamedai uwepo wa Serikali tatu ? Je ni WaZanzibari ndio walio kuja na tume ya Nyalali na kutoa maamuzi ya serikali tatu ? Msiwe dhaifu wa kujadili muungano kiume ,kila siku tunasema Muungano unamatatizo ,mmebadili msamiati na kuziita kero !! Kero hizi hebu jiulizeni zimeanza lini na zitakwisha lini ,mbona mpaka leo kunaundwa tume na vigogo kukutana na hakuna la maana hata moja linaloamuliwa kiume ! Nani anamuogopa nani ? Hatimae Zanzibar wameamua kivyaovyao kama nilivyowahi kusema kuwa sasa Zanzibaer itajiendesha kivyakevyake ?

Tatizo kubwa ambalo linautikisa Muungano ni hili la ufisadi mkubwa sana ambao haujawahi kutokea unaofanywa ndani ya serikali ya Muungano ukiwahusisha wabara watupu na hakuna sheria zinazochukuliwa ?!!? Zanzibar kama nchi inayofanya muungano huu kidamu kabisa inaona hali hii haiwezi kuendelea ikiwa nayo ni sehemu ya Muungano maana hasara inayopatikana pia inaiathiri Zanzibar kwa upande fulani kimaendeleo.Wizi wa matrilioni ya shilingi unafanyika waziwazi ,huku hazina za Taifa zikipotea ,sasa kama Zanzibar wana mafuta na yananyemelewa na Muungano ,hamuoni kama faida haitapatikana na hawa wezi waliomo ndani ya serikali ya Muungano ambao sheria haziwagusi wataweza kuifikia kirahisi hazina ya Zanzibar na kuitafuna bila ya woga kama wanavyoitafuna hazina ya Tanganyika ? Hivi kutakuwa na Muungano au kutakuwa na wezi waliojificha ndani ya Muungano huu ?

Tunaposema Wazanzibari inabidi mufahamu kuwa panazungumziwa wananchi wa Zanzibar ambao ndio wanaoounda serikali ya Zanzibar ,hawa wameshaona hatari inayosogea katika nchi yao ,iweje WaTanganyika wanakaa kimya hawawezi hata kuandamana kuishinikiza serikali iwachukulie hatua wezi wa matrilioni ya shilingi ? Kama waTanagayika waliomo ndani ya serikali ya Muungano ambao ni 99% hawawezi kukemea na kuwatia hatiani wezi ,hivi kutakuwa na faida gani yakuwepo kwa serikali hii isiyo na meno au tuseme iliyojaa makumbatiano,kulindana wakati nchi inadidimia na hakuna sababu za kudidimia ikiwa kutakuwa na hatua madhubuti ? Zanzibar imeamua kuchukua hatua za dharura ili kukabiliana na hali hii ambayo inavunja matumaini ya mwananchi.

Sasa WaZanzibar wameingiwa na tamaa kuwa mambo yao yatakuwa super kwa kuweka serikali itakayojali hali ya mwananchi, ,serikali ambayo itawajibika kwa wananchi. Na ikiwezekana serikali hiyo itakuwa na meno ya kuidhibiti serikali ya Muungano ,kwani serikali kuu ni serikali za Zanzibar na Tanganyika ,(Serikali ya Tanganyika haipo)hili nalo ndio tatizo sugu ambalo inabidi lishughulikiwe ili serikali hii ya Tanganyika iweze kurudishwa.

Serikali ya Zanzibar ni mdau wa serikali ya Muungano hivyo ni lazima iwe na nguvu kamili za kuihoji serikali ya Muungano kisheria bila ya kuwepo kizingiti chochote kile ,cha wabunge au wawakilishi.Serikali ndio itayokuwa ya mwisho kukubali au kukataa jambo lolote lile lisilokuwa na maslahi kwa Zanzibar na kuamrisha wawakilishi wake kuamua kwa kuweka veto ndani ya baraza la wawakilishi kuzuia hujuma zozote zinazolenga uhujumu wa Zanzibar ,karibuni mtaelewa kuwa Zanzibar ni nchi ndani na nje ya mipaka hii ,mmambo ya kuburuzwa kwa kisingizio cha kivuli cha Muungano yatafikishwa mwisho ,kisheria na kiuzalendo.

Kama hamna kikwazo basi irudisheni serikali ya Tanganyika kwa haraka sana ili uwepo uwiano ndani ya serikali ya Muungano ,mambu mengi sana yanapotua ndani ya serikali ya muungano hayafiki Zanzibar ,jamani tumeungana kama nchi mbili zilizohuru ,kwa ridhaa za viongozi wakuu wa nchi hizi ,sasa mnapoanza kusema Zanzibar ni kanchi kadogo hakistahili kupata 50% ya msaada unaopewa Tanzania ,mtakuwa hamuitendei haki Zanzibar.
 
Mnaposema WaZanzibari hawautaki Muungano hapo mtakuwa mnakosea na kwa lugha ya kileo mtakuwa mnapoteza dira. Zanzibar wamefanya mabadiliko makubwa sana na hawakuogopa mtu ,au chama chochote kile.

Bunge la tanzania haswa hawa WaTanganyika wanakuwa na matatizo ya kiuamuzi na wanakuwa na jazba ,aidha wanakuwa na chuki za kidini au kibinafsi au wanakuwa na choyo flaniflani ,hivi ni wangapi wamedai uwepo wa Serikali tatu ? Je ni WaZanzibari ndio walio kuja na tume ya Nyalali na kutoa maamuzi ya serikali tatu ? Msiwe dhaifu wa kujadili muungano kiume ,kila siku tunasema Muungano unamatatizo ,mmebadili msamiati na kuziita kero !! Kero hizi hebu jiulizeni zimeanza lini na zitakwisha lini ,mbona mpaka leo kunaundwa tume na vigogo kukutana na hakuna la maana hata moja linaloamuliwa kiume ! Nani anamuogopa nani ? Hatimae Zanzibar wameamua kivyaovyao kama nilivyowahi kusema kuwa sasa Zanzibaer itajiendesha kivyakevyake ?

Tatizo kubwa ambalo linautikisa Muungano ni hili la ufisadi mkubwa sana ambao haujawahi kutokea unaofanywa ndani ya serikali ya Muungano ukiwahusisha wabara watupu na hakuna sheria zinazochukuliwa ?!!? Zanzibar kama nchi inayofanya muungano huu kidamu kabisa inaona hali hii haiwezi kuendelea ikiwa nayo ni sehemu ya Muungano maana hasara inayopatikana pia inaiathiri Zanzibar kwa upande fulani kimaendeleo.Wizi wa matrilioni ya shilingi unafanyika waziwazi ,huku hazina za Taifa zikipotea ,sasa kama Zanzibar wana mafuta na yananyemelewa na Muungano ,hamuoni kama faida haitapatikana na hawa wezi waliomo ndani ya serikali ya Muungano ambao sheria haziwagusi wataweza kuifikia kirahisi hazina ya Zanzibar na kuitafuna bila ya woga kama wanavyoitafuna hazina ya Tanganyika ? Hivi kutakuwa na Muungano au kutakuwa na wezi waliojificha ndani ya Muungano huu ?

Tunaposema Wazanzibari inabidi mufahamu kuwa panazungumziwa wananchi wa Zanzibar ambao ndio wanaoounda serikali ya Zanzibar ,hawa wameshaona hatari inayosogea katika nchi yao ,iweje WaTanganyika wanakaa kimya hawawezi hata kuandamana kuishinikiza serikali iwachukulie hatua wezi wa matrilioni ya shilingi ? Kama waTanagayika waliomo ndani ya serikali ya Muungano ambao ni 99% hawawezi kukemea na kuwatia hatiani wezi ,hivi kutakuwa na faida gani yakuwepo kwa serikali hii isiyo na meno au tuseme iliyojaa makumbatiano,kulindana wakati nchi inadidimia na hakuna sababu za kudidimia ikiwa kutakuwa na hatua madhubuti ? Zanzibar imeamua kuchukua hatua za dharura ili kukabiliana na hali hii ambayo inavunja matumaini ya mwananchi.

Sasa WaZanzibar wameingiwa na tamaa kuwa mambo yao yatakuwa super kwa kuweka serikali itakayojali hali ya mwananchi, ,serikali ambayo itawajibika kwa wananchi. Na ikiwezekana serikali hiyo itakuwa na meno ya kuidhibiti serikali ya Muungano ,kwani serikali kuu ni serikali za Zanzibar na Tanganyika ,(Serikali ya Tanganyika haipo)hili nalo ndio tatizo sugu ambalo inabidi lishughulikiwe ili serikali hii ya Tanganyika iweze kurudishwa.

Serikali ya Zanzibar ni mdau wa serikali ya Muungano hivyo ni lazima iwe na nguvu kamili za kuihoji serikali ya Muungano kisheria bila ya kuwepo kizingiti chochote kile ,cha wabunge au wawakilishi.Serikali ndio itayokuwa ya mwisho kukubali au kukataa jambo lolote lile lisilokuwa na maslahi kwa Zanzibar na kuamrisha wawakilishi wake kuamua kwa kuweka veto ndani ya baraza la wawakilishi kuzuia hujuma zozote zinazolenga uhujumu wa Zanzibar ,karibuni mtaelewa kuwa Zanzibar ni nchi ndani na nje ya mipaka hii ,mmambo ya kuburuzwa kwa kisingizio cha kivuli cha Muungano yatafikishwa mwisho ,kisheria na kiuzalendo.

Kama hamna kikwazo basi irudisheni serikali ya Tanganyika kwa haraka sana ili uwepo uwiano ndani ya serikali ya Muungano ,mambu mengi sana yanapotua ndani ya serikali ya muungano hayafiki Zanzibar ,jamani tumeungana kama nchi mbili zilizohuru ,kwa ridhaa za viongozi wakuu wa nchi hizi ,sasa mnapoanza kusema Zanzibar ni kanchi kadogo hakistahili kupata 50% ya msaada unaopewa Tanzania ,mtakuwa hamuitendei haki Zanzibar.


Bravo Mwiba i likeyour points keep it
 
Mnaposema WaZanzibari hawautaki Muungano hapo mtakuwa mnakosea na kwa lugha ya kileo mtakuwa mnapoteza dira. Zanzibar wamefanya mabadiliko makubwa sana na hawakuogopa mtu ,au chama chochote kile.

Bunge la tanzania haswa hawa WaTanganyika wanakuwa na matatizo ya kiuamuzi na wanakuwa na jazba ,aidha wanakuwa na chuki za kidini au kibinafsi au wanakuwa na choyo flaniflani ,hivi ni wangapi wamedai uwepo wa Serikali tatu ? Je ni WaZanzibari ndio walio kuja na tume ya Nyalali na kutoa maamuzi ya serikali tatu ? Msiwe dhaifu wa kujadili muungano kiume ,kila siku tunasema Muungano unamatatizo ,mmebadili msamiati na kuziita kero !! Kero hizi hebu jiulizeni zimeanza lini na zitakwisha lini ,mbona mpaka leo kunaundwa tume na vigogo kukutana na hakuna la maana hata moja linaloamuliwa kiume ! Nani anamuogopa nani ? Hatimae Zanzibar wameamua kivyaovyao kama nilivyowahi kusema kuwa sasa Zanzibaer itajiendesha kivyakevyake ?

Mambo ya dini yametoka wapi? Si ndio unafik tunaouzungumzia! Humu kutoka bara wako wakina Mkandara na wakina Fundi Mchundo halafu wewe unataka kuingiza dini. Hauna aibu, Mkuu?

Hata ikiwa serikali tatu mambo yatabaki hivi hivi. Hamtaisha kulalamika. Ndio maana sisi wengine kutoka bara ndio maana tunasema, ili kukata mzizi wa fitna, basi huo Muungano uvunjwe. Watu wa bara wabaki na mafisadi wao na nyie waungwana wa Zanzibar mchangamkie misaada ambayo hamtalazimika kugawana na bara. Kigugumizi cha nini?

Amandla.......
 
kwa sababu mabadiliko ya katiba ya Zanzibar hivi sasa hayana nguvu bila kukubalika na Bunge la Muungano; sasa Bunge la Muungano litatakiwa kuridhia au kukataa. Likikataa Zanzibar watasema nini?

Hawana sababu ya kujali.
Z'bar imeshakuwa nchi. Ina serikali, SMZ. wana wimbo wa Taifa. Wana bendera.
Bado wanahitaji vitu vichache sana! Kama watarudisha pasipoti zao, itakuwa hatua nzuri zaidi!
 
Hawana sababu ya kujali.
Z'bar imeshakuwa nchi. Ina serikali, SMZ. wana wimbo wa Taifa. Wana bendera.
Bado wanahitaji vitu vichache sana! Kama watarudisha pasipoti zao, itakuwa hatua nzuri zaidi!

Unajua Seif Sharifu Hamad ndiye hapendi muungano, ni tofauti sana na wazanzibari wenye asili ya bara. Na mabadiliko ya katiba ya Zanzibar ni seif ameyafanya inagawa watu wanasema ni baraza la wawakilishi. Anataka kuendelea polepole na ambtion zake ya kuitenga zanzibar kutoka kwenye jamhuri ya muungano, then kuigawa na kuwe na Unguja na pemba, kisha arudishe usultani Pemba. Hatua ya kwanza amefanikiwa, sasa atajaribu kubadilisha katiba ya jamhuri ya muungano lakini hapo atashindwa.
 
Wazanzibari lao kubwa ni kumaliza ndoa yao na Tanganyika,wanataka talaka,hata kama mtaleta serikali ya mseto huko visiwani.Cha muhimu kwa upande wa bara ni kurudisha serikali ya Tanganyika na kufanya kazi kwa juhudi na maarifa.Tuachane na visingizio vya Wazanzibari ati wanaonewa.Watamalizana wenyewe baada ya muda mfupi tu.
 
mr. Ag shame on you ! if JK is depending on you for advise then he should look for somebody else.You knew in advance this crap was coming so how much time do you need to defend constitution? This is a serious matter affecting millions of Tanzanians; we Tanzanians demand answers as soon as possible .
 
kwa sababu mabadiliko ya katiba ya Zanzibar hivi sasa hayana nguvu bila kukubalika na Bunge la Muungano; sasa Bunge la Muungano litatakiwa kuridhia au kukataa. Likikataa Zanzibar watasema nini?

Inawezekana wakajitenga, maana sasa wamekuwa wamoja (CUF & CCM), nadhani kuna siri kubwa sana behind this
 
Mwiba,
Tatizo kubwa ambalo linautikisa Muungano ni hili la ufisadi mkubwa sana ambao haujawahi kutokea unaofanywa ndani ya serikali ya Muungano ukiwahusisha wabara watupu na hakuna sheria zinazochukuliwa ?!!? Zanzibar kama nchi inayofanya muungano huu kidamu kabisa inaona hali hii haiwezi kuendelea ikiwa nayo ni sehemu ya Muungano maana hasara inayopatikana pia inaathiri Zanzibar kwa upande fulani kimaendeleo.Wizi wa matrilioni ya shilingi unafanyika waziwazi ,huku hazina za Taifa zikipotea ,sasa kama Zanzibar wana mafuta na yananyemelewa na Muungano ,hamuoni kama faida haitapatikana na hawa wezi waliomo ndani ya serikali ya Muungano ambao sheria haziwagusi wataweza kuifikia kirahisi hazina ya Zanzibar na kuitafuna bila ya woga kama wanavyoitafuna hazina ya Tanganyika ? Hivi kutakuwa na Muungano au kutakuwa na wezi waliojificha ndani ya Muungano huu ?
Mkuu wangu acha kutuzuga. Viongozi wa serikali ya Muungano ndio MAFISADI wenyewe halijalishi nafasi ya mtu katoka sehemu gani ya Muungano.. hawa wote kwa pamoja wanachelewesha maendeleo ya sehemu zote mbili. Hivyo kama kweli kungekuwa na mwamko huo Wazanzibar tungewasikia Bungeni wakilaani Ufisadi na hata wangetaka mabadiliko ya Katiba ya Muungano kuhusiana na miiko na maadili ambayo Yalivunjwa na Mh. Mwinyi rais wa jamhuri na mwakilishi wa Zanzibar.

Ukisema ati Zanzibar wanaona Ufisadi ulivyo bara, hali uongozi wake unawashirikisha viongozi toka Zanzibar ktk kila nafasi ndani ya serikali ya Muungano ni kutafuta uongo unaokubalika ili mradi mnakipaka tu... Nenda wizarani, mashirika ya Umma, taasisi za serikali wamejaa Wazanzibar wengi tu na Mafisadi pia tena ktk miradi ya Bara na sijawahi sikia Wabara tukizungumzia watu hao kuwa Mafisadi kutokana na Uzanzibar wao.

Na unapofikiria kwamba kuwepo kwa Mafuta huko visiwani ndio kunapelekea Zanzibar kufikiria maslahi yake ni jambo ambalo linanipa wasiwasi na mtazamo wako ktk mahusiano ya Muungano wetu.. Yaani unanikumbusha kisa cha mshiakaji wangu hapa aliyekwenda kuoa mke Bongo miaka kibao tukidhania wakipendana ajabu.. Na MaashaLlah Mnyazi Mungu kawajaalia watoto baada ya kuishi ktk ndoa miaka 10 pamoja, wakati huo huo wa ndoa mke alichukua masomo ya U nurse na muda wote huyu mshikaji akiingia gharama zote.

Siku mkewe alipomaliza masomo na kuanza kazi ndipo siku tuloanza kusikia mke akidai Talaka yake kwa madai kwamba hakuwa akimpenda jamaa toka zamani. Ndipo tuliposikia hadithi zote za jinsi alivyokuja poswa na kulazimika kuolewa kutokana na mazingira alokuwa nayo wakati ule lakini hakuwa na mapenzi na huyu jamaa. yaani mke aliolewa kwa sababu ya kuvuta karatasi za kuishi Ulaya lakini hapakuwa na mapenzi..eeeh ngoma nzito hiyo baabu!

Sasa kwetu sisi tunajiuliza hivi, kama huyu mke angeomba talaka yake na kudai hana mapenzi naye tena na amechoka kuishi ktk ndoa hiyo. Bila shaka ingeeleweka vizuri na kwa uzito mkubwa zaidi kuliko kusiribia kinyesi kwa karatasi unayotawadhia..
Tatizo kubwa ni pale huyu mwanamke anapoweka madai ya kumshusha hadhi jamaa, abuse za maneno sijui ya kwamba hakuwa na mapenzi naye kwa miaka yote 10 isipokuwa ilibidi tu.. Na zaidi ya hapo tulisikia hadi mambo ya ndani chumbani yaani ilikuwa mwanamke anasiriba sio kupaka tena..

Mkuu wangu siku zote tujaribu sana kuepusha maamuzi yatokanayo na vitu viwili:-
1.Ushawishi wa fedha au mali na 2. Ushawishi utokanao na Ulimbukeni.

Kauli zozote zinazoweza tafsirika kutokana na hayo hapo juu ndizo huondoa ladha na uzito wa hoja ya mtu kama huyu binti yetu kufikia sisi kumwona yeye ndiye asokuwa na akili. Hakuwa na sababu ya kuzungmza yoote haya ya toka ampigie mahesabu jamaa Bongo hadi maswala ya ndani ya unyumba ili kuleta uhalali wa kuomba Talaka tu. Unapotaka talaka hulazimishwi kutaja sababu kubwa au kuonyuesha ujanja wa akili kumzunguka alolala ili kuhalalisha madai yako,kwani - Haihusu!
Ukisema umechoka kuishi maisha ya ndoa inatosha kabisa kupata sheria ya kuachika -No means NO!.

Sasa kichekesho ni kwamba mshikaji pia kwa miaka mingi alikuwa akitafuta njia ya kumtoka mkewe isipokuwa alishindwa kutokana na wajibu aloji commit kuingia ktk ndoa kulingana na imani yake ya dini kisha tayari walikuwa wamezaa watoto. Kifupi kila mmoja wao alikuwa akitafuta njia ya kumtoka mwenzake kumbe hawa jamaa kwa miaka yote waliyoishi ndani ya ndoa hawakuwa na mapenzi ya haki. Kwa upungufu kila mmoja wao aliingiza tu asilimi 50 ya nguvu ya kimapenzi hivyo kila mmoja wao alimuona mwenza kuwa mchovu wa Mapenzi.

Hatuwahitaji Zanzibar hata kidogo zaidi ya kiapo, but for sure najua fika Zanzibar inawahitaji Bara..ndio inachofanya tunahitajiana.. Hiyo Greencard waliyokuwa nayo Zanzibar haitoshi kuweka guarantee usalama wa visiwa hivyo. I 'm 100 sure baada ya kujitenga tu basi Pemba watatumia sababu hizi hizi za leo Zanzibar nao kujitenga. wataanza na kuomba madaraka zaidi, ku share leadership na mwsiho ya yote hawautaki Muungano wa visiwa vya Zanzibar. Uhasama wa Kiutawala Zanzibar upo baina ya Wazanzibar wenyewe toka enzi za kutawaliwa. Hawa jamaa wamejificha ktk makundi ya vyama hivi lakini Uadui wao upo palepale na Bara inatumiwa tu kuamsha cheche za upinzani wao.

Hakuna Mzamzibar kiongozi asiyependa Muungano (ndio baba zenu hawa) na kama mmeozeshwa pasipo mapenzi wekeni maombi ya talaka mtapewa na sio kutukandya Bara mkifikiria ndio mnajenga hoja zenu.. Tumebebana vya kutosha mkuu wangu na nadhani ni vizuri sana mkiweka wazi ombi la kuvunja Muungano..sii lazima kututukana kana vile sisi ni Washenzi, Mashetani watu wasiokuwa na ustaarabu hali mmekuwa ktk ushirika huu kwa zaidi ya miaka 40 inawafanya nyie kuonekana wapumbavu au vichaa.. Na kibaya zaidi ni kwamba mnazugumzia sana hisia zenu nyie katika Muungano huu pasipo kuelewa kwamba hata sisi Bara tulishachoka isipokuwa tumebakia ktk Muungano huu kutokana na kiapo na watoto tulokwisha zaa ndani ya Muungano huu.
 
Mkuu Mkandara,

Kweli tupu uliyonena. Watu wanataka kuandika historia upya wakati Bara ilikuwa ndiyo kimbilio lao walipokuwa wakitendewa matendo ya kidhalimu na viongozi wao! Kuanzia Sultani wao ambaye alipewa hifadhi bara baada ya Kenya kukataa kupokea meli yake. Mpaka wakina Babu na wengine siasa chafu za chuki na kisasi zingewatoa roho. hadi hao walioukataa Muungano wakiwa madarakani, leo wana sehemu la kujidai bara. Bandari zao, viwanja vyao, vya ndege, viwanda vyao vya ndege wameviua lakini bado bila aibu wanadai kuwa hawana mafisadi nchini mwao. Kiwanja cha ndege unguja kinanuka rushwa, watalii wanaibiwa wazi wazi. Watoto wao wamekuwa mateja wakitegemea hela za ankal lakini hawataki kutambua kuwa teja yuko tayari kufanya lolote ili apate hicho anachotumia. Nako watasema watu wa bara ndio wanaingiza madawa hayo ya kulevya? Maovu yako kila mahali, lakini wenzetu wanataka kutunyooshea kidole wakisahau vinne wanajinyooshea wenyewe.

Amandla........
 
Back
Top Bottom