Mwiba
JF-Expert Member
- Oct 23, 2007
- 7,607
- 1,744
Tokea ulipoondoka utawala wa kwanza ambao ndio utawala uliopokea uhuru wa Zanzibar ,hali za kitawala zilizofuatia zimekuwa za kibabe ,kuanzia Karume ,Jumbe,Ali hassan Mwinyi,Salmini Komandoo , Karume ,tuwache hawa wapemba wawili Shein na Seif ,siwatii hisabuni kwa sasa ,ila ubabe tumeuona juzi na jana kuhusiana na wale wajiitao uamsho.
Tawala hizo ni tawala za kibabe na kulikuwa hakuna kufurukuta ,ukitofautisha na ile ya Mfalme ambayo ilikuwa na mambo yake lakini si ya kibabe, natumai inafahamika nisemapo mambo ya kibabe,nguvunguvu ujeshijeshi ,kamata weka kolokoloni funga no question or comment n.k.
Sasa nimekuwa nikifikiria sana hawa wanaoshangilia kuvunjika Muungano ,mimi sipo pamoja nao ,langu ni kuwa Muungano uboreshwe na matatizo yatatuliwe kwa amani kabisa na kwa nia safi.Bila ya kuwepo na agenda za siri ,mkubwa kuonekana kumtawala au kummeza mdogo.
Serikali ya Muungano imekuwa ikiangalia mambo ya Zanzibar bila ya kuyaingilia au kuyasemea ,pengine hayahusiki na Muungano ,kuna wakati wa Karume watu kibao ambao walikuwa pamoja walitoweka na hawakujulikana wamezikwa kaburi gani ,kuna wakati wa akina Salmini na Karume mwana,watu walikuwa wakipigwa hovyovyo kusema kweli ilikuwa wakipigwa kwa zamu,yaani leo unakwenda kupigwa mtaa fulani kesho mtaa mwengine ,Serikali haikusema kitu na ikijua ikisikia, inasemekana hata vijana wakitoka Tanganyika ,haya yakitokea zaidi nyakati za uchaguzi ,mtekelezaji mkuu ni mgombea wa wakati huo hivyo hata utawala wake unakuwa wa kuwatia hofu wananchi ,uhuru unakuwa haupo.
Sasa tuchukulie leo hii Muungano unapasuka watu wanagawana mbao ,sioni sababu ambayo itamzuia mtawala wa Zanzibar kuwa mbabe ,tena safari hii kwa kiwango kikubwa ,kama kuliweza kufanyika ubabe wakati wa Muungano itashindwaje leo hakuna muungano ,atakae kamata mpini atajipanga kikweli na majilabu yatakuwa ya kutisha na atakaefurukuta na kutokeza pua atakiona kilichomfanya kuku kishingo kutokuwa na manyoya shingoni.
Serikali ya muungano imewatupa wananchi wa Zanzibar kwa kudharau na kuacha watawala waliopita kuwanyanyasa wananchi bila ya kuingilia kati , tuseme leo hii wananchi wameamua bora jini likujualo kwa maana Muungano uliopo hauwasaidii kitu ni kama haupo ,zaidi unajali maslahi binafsi ,hivyo ni bora ukavunjika ,lakini kama ukivunjika bado suala utakuwa ni kwa faida ya nani ,au itakuwa ni kupinduana kila kukicha ?
Kuvunjika kwa Muungano ni hatari kwa upande wa Zanzibar ,huku Tanganyika hakuna historia ya ubabe iliyowahi kumtia hofu mwananchi wa kawaida ukilinganisha na Zanzibar.Zanzibar kabla ya 1964 ilikuwa shwari ,hayo ya waarabu walikuwa hivi au vile yalikuwepo lakini hakuna historia inayoonyesha kuwa mwananchi alikuwa akiishi kwa hofu na woga kama baadaya 1964 hadi leo.
Nakaribisha hoja na maoni.
Tawala hizo ni tawala za kibabe na kulikuwa hakuna kufurukuta ,ukitofautisha na ile ya Mfalme ambayo ilikuwa na mambo yake lakini si ya kibabe, natumai inafahamika nisemapo mambo ya kibabe,nguvunguvu ujeshijeshi ,kamata weka kolokoloni funga no question or comment n.k.
Sasa nimekuwa nikifikiria sana hawa wanaoshangilia kuvunjika Muungano ,mimi sipo pamoja nao ,langu ni kuwa Muungano uboreshwe na matatizo yatatuliwe kwa amani kabisa na kwa nia safi.Bila ya kuwepo na agenda za siri ,mkubwa kuonekana kumtawala au kummeza mdogo.
Serikali ya Muungano imekuwa ikiangalia mambo ya Zanzibar bila ya kuyaingilia au kuyasemea ,pengine hayahusiki na Muungano ,kuna wakati wa Karume watu kibao ambao walikuwa pamoja walitoweka na hawakujulikana wamezikwa kaburi gani ,kuna wakati wa akina Salmini na Karume mwana,watu walikuwa wakipigwa hovyovyo kusema kweli ilikuwa wakipigwa kwa zamu,yaani leo unakwenda kupigwa mtaa fulani kesho mtaa mwengine ,Serikali haikusema kitu na ikijua ikisikia, inasemekana hata vijana wakitoka Tanganyika ,haya yakitokea zaidi nyakati za uchaguzi ,mtekelezaji mkuu ni mgombea wa wakati huo hivyo hata utawala wake unakuwa wa kuwatia hofu wananchi ,uhuru unakuwa haupo.
Sasa tuchukulie leo hii Muungano unapasuka watu wanagawana mbao ,sioni sababu ambayo itamzuia mtawala wa Zanzibar kuwa mbabe ,tena safari hii kwa kiwango kikubwa ,kama kuliweza kufanyika ubabe wakati wa Muungano itashindwaje leo hakuna muungano ,atakae kamata mpini atajipanga kikweli na majilabu yatakuwa ya kutisha na atakaefurukuta na kutokeza pua atakiona kilichomfanya kuku kishingo kutokuwa na manyoya shingoni.
Serikali ya muungano imewatupa wananchi wa Zanzibar kwa kudharau na kuacha watawala waliopita kuwanyanyasa wananchi bila ya kuingilia kati , tuseme leo hii wananchi wameamua bora jini likujualo kwa maana Muungano uliopo hauwasaidii kitu ni kama haupo ,zaidi unajali maslahi binafsi ,hivyo ni bora ukavunjika ,lakini kama ukivunjika bado suala utakuwa ni kwa faida ya nani ,au itakuwa ni kupinduana kila kukicha ?
Kuvunjika kwa Muungano ni hatari kwa upande wa Zanzibar ,huku Tanganyika hakuna historia ya ubabe iliyowahi kumtia hofu mwananchi wa kawaida ukilinganisha na Zanzibar.Zanzibar kabla ya 1964 ilikuwa shwari ,hayo ya waarabu walikuwa hivi au vile yalikuwepo lakini hakuna historia inayoonyesha kuwa mwananchi alikuwa akiishi kwa hofu na woga kama baadaya 1964 hadi leo.
Nakaribisha hoja na maoni.