Zanzibar na hatima ya Muungano ni hatari...

na uvunjike tu hakuna namna sasa, mana wanaonewa sana wananchi kule.

Naona CHADEMA tanzania bara toka Lowasa ashindwe mko frustrated sana.Ndio mmekuwa vinara wa kuanzisha humu maada nyingi za Zanzibar na kuzichangia wenyewe.Mnatumia Zanzibar KU-STEAM OUT FRUSTRATION zenu za Lowasa kubwagwa.Poleni
 
muungano hauwezi kuvunjika ng'o! Hata wazanzibar wakimbie wote au wafe wote. Bara haiwezi kuiacha Zanzibar hata kwa nukta. Sababu kubwa ni uislam wao tu,rejea maneno ya lukuvi aliyoyasema kanisani mwakajana utakubaliana namimi na huo ndio ushahidi. Ingekuwa population ya Zanzibar ni wakristo ulimwengu ungesimama na haki ikapatikana na Zanzibar ingekuwa huru kama southsudan. Lakn Zanzibar imekuwa kama palestina kutoka Israel japo hazfanani mojakwa moja. Southsudan ilikuwa rahisi kujitenga lkn kwa Zanzibar haiwezekani kwasababu tu ya uislam wao
 
Mwenye uwezo wa kuvunja muungano ni serikali ya muungano na ya SMZ lakini kwa kuwa zote zote zinaongozwa na CCM usitarajie kuvunjika muungano bali kuimarishwa kwa nguvu zote na kudhibitiwa waleta fyokofyoko.
 
Awawezi kuvunja. muungano kwa sababu wazanzibar wanategemea tz kwa %sema kwa hili lilivyo inaonekana znzb awana meno katika hili
 
Kila nikifikiri kwa yalio tokea zanzibar na yanayo endelea huko sintasita kusema muungano uko mbion kuvunjika.
Kwa wale wenye kuona mbali hebu tutafakar kidogo!

SUK na katiba mpya ilipatikana baada ya mgogoro uliosababisha wakimbiz kwa mara ya kwanza visiwan humo.
Tukumbuke cuf walisusia baraza la wawakilishi, kwa wenye mtizamo wa karibu waliojua ndio mwisho wa cuf kumbe ndio mwanzo wa kudai usawa.

Kwa sasa cuf na vyama vingine hawajashiriki uchaguz, nn hatma yao na zanzibar kwa ujumla? Kwa mtizamo wangu huu ni muda wa kudai zanzibar huru! hakuna asiye jua zanzibar inatawaliwa kisiasa na Tanganyika. Shen peke yake hana ubavu wa kufanya haya yaliotokea kule zanzibar ila ni kwa mkono wa chuma kutoka bara!!
Tanganyika hatujitambui na tulishazoea kukandamizwa tangu tunaanza vyama vingi lakn kwa zanzibar walishaamka tangu 95. Yaan kungekua na tume huru wangeshinda cuf mwaka huo na chaguz zilizoendelea.

Tunaoshangilia yanayoendelea huko tukumbuke kuna watu wengi sana wamekaa kimya ila wakijiuliza kwann zanzibar iko hivi kisiasa??
nan anasababisha!?
nn suruhu yake ??

Kwa muono wangu safari iliyopita walitengeneza katiba mpya na SUK haijasaidia kuleta usawa wa kisiasa kifuatacho ni kuvunja MUUNGANO.

Jeuri hizi zinazo endelea huko zinatoka bara na bara wakifikiri ndio kulinda muungano kumbe ndio mwanzo wa Tanganyika kudai katiba mpya na Tanganyika yao wazanzibar kudai zanzibar huru!!
Nawakaribisha wenye kutafakari mbali!!
Sio taarifa mbaya.
 
Sitatizo kwangu, mimi na Watanganyika wengi hatuupendi huu Muungano (unatunyonya na kutuumiza wabara), WaUnguja wengi hawaupendi huu Muungano (wanahisi unawanyima haki zao especial za kupewa vya bure na mataifa ya kiarabu na western, Wapo ili walindwe)
Wapemba hawataki hata sikia (wanahisi unawanyima haki ya kuongoza visiwa vya Zanzibar na kulipa visasi kwa waunguja waliowapindua)
Muungano usioeleweka ndo huu, wasepe tu
 
Ni vema ukasoma sheria na katiba za Nchi kuliko kusoma magazeti yaliyojaa propaganda za wanasiasa
Sijui ni Dr. wanini, lakini sheria si zinatungwa na hao hao wanasiasa na wanao kiuka na kutuharibia katiba si hao hao? ila wanapo sema kwenye magazeti ndio tusiwasome? yaelekea chuki yako ni magazeti ila si yote yenye kupotosha ina tegemea unasoma magazeti gani na si wanasiasa wote ni watu wa propaganda wapo japo wachache walio wakweli na wenye uchungu na nchi yao na wanaeleweka,chagua vizuri tu.
 
Jadilianeni huko zenj mkimaliza nlete hoja zenu mezani. Kama muungano umewachosha mpige kura ya kuukataa. Malalamiko yenu yametuchosha wakati hakuna chochote cha maana tukipatacho kwenu kuwa sehemu ya muungano zaidi ya kuwalipia bili kibao
Tena tumechoka nao kweli kweli wame jazana huku bara wanafanya shughuli zao bila bugudha wanachukua ardhi wanalima wanajenga lakini tizama watu hawa kulalamika,kunungunika ndio shukrani yao.
 
Kutafuta maridhiano kuhusu maswala ya muunguno na kuboresha muungano ni jambo litakalowatafuna CCM milele, hadi hapo watakapokubali kufuata siasa za kisataarabu. Siasa zenye kushirikisha wananchi katika maamuzi muhimu kama haya. Kinyume chake kila Raisi atakaye chaguliwa kuongoza nchi ataonekana wazi ameshakula kiapo cha kufanya mauaji huko Zanzibar. Maana ni apende au asiepende. Na viongozi wa Zanzibar wanatakiwa kukomaa kisiasa zaidi inashangaza wanalambishwa asali midomoni wanaendelea kulamba wanashindwa kabisa kutoa hoja ya wanachokitaka, Wazanzibari wanaye raisi, watanganyika hatuna, wanayo katiba yao, watanganyika hatuna, wanalo bunge lao watangganyika hatuna, wanayo nchi yao watanganyika hatuna. Kilichopo ni serikali ya muungano, Bunge la muungano, Katiba ya muungano, nchi ya muungano nk. Tuliodhoofika zaidi katika hili ni watanganyika.
 
Tatizo la Zanzibar ni kuwa watawala wa kule watawala kwa nguvu ya muunga hasa bara. upande wa pili hata ufurukute hauambui kitu.
kwa hiyo kuvunjika kwa muungano kutaleta maafa. laba pande zete zianze kuja pamoja kabla ya kuvunja Muungano
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom