Tanganyika unayoiuliza iko wapi? aliiua Nyerere. Kuidai hivi sasa ina maanisha fikra za Nyerere zife na si zidumu tena.
Ni Watanzania wangapi leo hii wanaoweza kupinga fikra za Nyerere kwa makusudi kabisa?
Kuirudisha Tanganyika ni kuzidi kumpeleka mbali na utakatifu mwenyeheri Nyerere.
Muujiza wa kumfikisha Nyerere kuwa mtakatifu unakuwa rahisi sana nchi ikitoka kwenye serikali mbili ikawa moja. Itakuwa ni muujiza wa Nyerere umetimia, kuitawala nchi yenye zaidi ya asilimia 98 Waislaam na kuiingiza kwenye Serikali moja isiyo na dini.
Kumbuka, serikali ya Zanzibar ina dini na dini yake ni Uislaam na kadhi wanae.
Kufanya nchi iwe na Serikali tatu ni kuiuwa ndoto ya wanaompenda Nyerere awe mtakatifu. Linawezekana hilo?
Mimi natamani hata muungano usiwepo kama inawezekana, ikishindikana basi hizo tatu ndio pendeleo langu. Nakuhakikishieni na hilo ndilo pendeleo la Waislaam walio wengi.
duuuh hoja zako zimefungwa na fikra za udini ni kama kile kisa cha watu waliopangoni(an allegory of the cave)..Tanzania itadum daima..huu ni urithi na tnu za taifa,uundwaji wa katiba ni frsa ya kutatua mapungufu ya muungano wetu....tusione haya kuunga mkono fikra sahihi za Nyerere na Karume...hivi kati ya fikra zako za udini na zile za mzee karume na Nyerere zipi zina tija?