Yu Wapi Askari Mkama Sharp?

Mambo ya Daslam, nimekumbuka wauza minazi pale ubungo mataa pamoja na soko kubwa tu la bidhaa mbalimbali(ilipo stendi ya daladala), kulikuwa na hoteli opposite na Olicom pale Tanesco wale Wapemba walikuwa wanauza Kashata na kalimati balaa.
Hapa wanamuongelea askari lakini.

Ila kitambo ng'ambo ya minazi kulikuwa na hospitali inaitwa Barukta nadhani kwa ndani kidogo.
 
sawa sawa mkuu,nakumbuka maeneo ya kariakoo alikuwa hakosekani katika michiriku.


alikua anaishi kariakoo mkuu mtaa wa kibambawe ndio maana alikua hakosekani mwanzoni mwa miaka ya 90s enzi hizo nipo nursery
 
Siku hizi pale Kituo cha Polisi Magomeni kuna Mdada mmoja anaitwa Cynthia anatembea na Difenda za doria, nae anajitahidi sana.
 
hahahahaha......dar ilikuwa tam ingawa nilikuwa mdogo na hata ustaarabu bado ulikuwepo....
ILIKUWA FULL MIZENGWE KWA WALE TULIYOKUWA TUNAISHI KIMAZABE...
 
Siku hizi pale Kituo cha Polisi Magomeni kuna Mdada mmoja anaitwa Cynthia anatembea na Difenda za doria, nae anajitahidi sana.
Yule dada nuksi.....wanamuita Cynthia rothrock
 
Very interesting. Kuna somo kubwa hapa. Uchapakazi, Je huku tulipo nasi tutakumbukwa kwa yapi?
 
Huyu jamaa alishafariki dunia miaka mingi tu iliyopita baada ya kuugua kwa muda mrefu. Ila ukweli alikuwa sharp
 
Saba Sita na Saddam Hawa nao walikuwa Morogoro
 
Kwa wale wahenga wenzangu waliokuwa wapenzi wa kuhudhuria michezo kama mpira wa miguu na ngumi Bila Shaka si wageni wa jina hili

Mkama sharp alikuwa polisi mwenye mbwembwe za Aina yake huku akiwa na sifa ya ubabe na uwezo mkubwa wa kutuliza fujo

Ilikuwa ukimuona tu lazma uvutiwe kumuangalia maana anatembea kibabe,kiunoni Ana bastora mbili,pingu,kirungu nk.

Ilikuwa akionekana tu watu wenyewe wanatulia na alikuwa na uwezo WA kutuliza uwanja mzima.kwa wanaofahamu alipo huyu polisi wanijuze
 
Duuuh! safi sana watu kama hao ndio ambao wanatakiwa kwasababu wanakua wamefit kwenye career zoo.
 
Daah, I wish ningemuona enzi za uhai wake.
 
mara ya mwisho alikua temeke huku alinyoosha sana,sijui walimkodi maana alipoingia tu uhalifu ukaisha.aliondoka na jamaa kadhaa pale mtaani hawakurudi.ndio adabu ikawekwa
 
Wewe kqma hujui kaa kimya. Eti alikuwa hahongeki. Ni miongoni mwa wala rushwa wakubwa waliopata kutokezea . Tuulize sisi tuliokuwa tunaishi nae mitaa ya Kibambawe, kariakoo DSM.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…