Young Africans Sports Club (Yanga) | Special Thread

:p :p
Hahaha unajua mtani kiuhalisia yanga ndo mlimkosea sana morrison kumpanga na yikpe na molinga.

Nyie ndo Inabidi mumuombe radhi
Khaaaa!!! Haiwezi kutokea hiyo Mtani, tunaanzaje kumuomba radhi. Lol

Hamna alichokosewa zaidi ya kuwa mtu mwenye tamaa yaani yupo huku ila maisha wanayoishi majirani yanamzuzua.

Si ajabu hata huko Kimataifa pia na nyie akawafanyia mbwembwe hasa pale atakapokutana na klabu iliyo bora zaidi ya Simba na kuitamani.
 
Khaaaa!!! Haiwezi kutokea hiyo Mtani, tunaanzaje kumuomba radhi. Lol

Hamna alichokosewa zaidi ya kuwa mtu mwenye tamaa yaani yupo huku ila maisha wanayoishi majirani yanamzuzua.

Si ajabu hata huko Kimataifa pia na nyie akawafanyia mbwembwe hasa pale atakapokutana na klabu iliyo bora zaidi ya Simba na kuitamani.
Hahaha mtani dua la kuku hili ujue.

Sema poleni sana naelewa huzuni mnayopitia, I feel what you feel

Ama kweli ukiwa masikini manyanyaso yanakuja bila hata kujua ili mradi tu uchanganyikiwe uuze timu :D :p
 
20200809_075805.jpg
WAZIRI JUNIOR AITAKA JEZI NAMBA 10

MSHAMBULIAJI mpya wa timu ya Yanga, Wazir Junior, amesema atajisikia faraja iwapo atapewa jezi namba 10 iliyokuwa inavaliwa na Tariq Seif.

Wazir amesajiliwa na Yanga kwa mkataba wa miaka miwili akitokea Mbao FC, kwa ajili ya msimu ujao wa Ligi Kuu Tanzania Bara, utakaoanza Septemba 6, mwaka huu.

Tariq aliyesajiliwa na Yanga kipindi cha dirisha dogo la msimu uliopita alikuwa anavaa jezi hiyo,kabla ya hivi karibuni kutemwa katika kikosi hicho.

Alizungumza na BINGWA jana, Tariq alisema anapenda kuvaa jezi namba 10 kwa kuwa ina historia kubwa katika maisha yake, lakini pia inavaliwa na nyota wengi duniani.

“Jezi hii ni ya heshima sana kwa sababu inavaliwa na mchezaji mwenye mafanikio makubwa katika soka kimataifa, lakini pia kwangu inahistoria ya kipekee ndio maana nimewaomba viongozi wa Yanga wanipe jezi namba 10,” alisema Waziri.
 
Khaaaa!!! Haiwezi kutokea hiyo Mtani, tunaanzaje kumuomba radhi. Lol

Hamna alichokosewa zaidi ya kuwa mtu mwenye tamaa yaani yupo huku ila maisha wanayoishi majirani yanamzuzua.
Unajua wee Shadeeya mashabiki wenzako wa vyura dizaini ya Sibonike wanakumandi kwa kutoa ushirikiano kwa mashabiki wa upande wa pili kwa kuwajibu 'kistaarabu'!?
 
Back
Top Bottom