Nundu_Tanzania
JF-Expert Member
- Apr 19, 2019
- 811
- 349
Adamu na Hawa ni wazazi wetu wa mwanzo, mababu zetu.Hao adam na hawa unahakika gani kwamba walikuwepo mzee?
Pasipo Yesu hakuna chochote kilichofanyika. Kwa Kifo chake kile kilichoharibu hali ya kimungu ya mtu yaani akili kiliondolewa.Uhusiano wa kifo cha yesu na akili ya binadamu unaunganishwa na point ipi?
Tuanzie kwanza hapa; nini maana ya akili?Pasipo Yesu hakuna chochote kilichofanyika. Kwa Kifo chake kile kilichoharibu hali ya kimungu ya mtu yaani akili kiliondolewa.
Akili ya binadamu ili iwezekuwa na nguvu au hali ya kimungu ni pekee katika na kwa njia ya Yesu Kristo, Kifo chake.
Habari ya hekima ya Suleimani kwa vipi inaweza kutenganishwa na uwepo wa Yesu ?Suleimani alipewa maarifa makuu ya kujenga hekalu ambalo mpka Leo linaheshimiwa, Yesu alikuwepo?
Ni uwezo wa kutambua, kuona, kufikiri na kuhukumu.Tuanzie kwanza hapa; nini maana ya akili?
Jina lako tu lina-reflect ulichoandika.mtoa mada jichunge, utapigwa vibao .. najua sio kosa lako kuandika blah blah !
Swali la kujiuliza ni "Nafsi ni nini ?Hii mada haina usahihi wa kushabihisha Kristo na akili ya Maarifa ya kidunia, kristo hakuja kuokoa 'nguvu ya uhai' bali kuokoa nafsi.
Mwanzo 3:7 hapo utaona 'nguvu ya uhai' inaposhindwa kumudu nafsi, hawa alishindwa kumudu na baadaye unaona walijua wako uchi, why?
Kwa sababu ile nafsi ya k
Pia usiache kuwashukuru wale waliofanya juhudi ya kumkimbiza hadi wakamkamata Yesu na kumpeleka msalabani ili wewe upate akili ya kiunguKwa kosa la Adam na Hawa, mtu aliondelewa uwezo wa akili, hali ya kimungu.
Mtu aliumbwa kwa mfano na sura ya Mungu. Ndiyo kusema mtu ni mwili na roho aliyeumbwa kushiriki uumbaji wa muumba wake, Mungu.
Roho au wakati mwingine huitwa akili pia moyo ndiyo maarifa yote.
Pasipo akili au roho, mtu anakuwa sawa na mnyama au mimea, hakuna maendeleo yoyote.
Kwa kosa la Adam na Hawa, wazazi wetu wa kwanza lilijeruhi roho au akili.
Kwasababu hiyo uwezo wa mtu kutenda kiakili yaani kimungu uliondoka akawa sawa na wanyama.
Binadamu kwa muda mrefu sana ameishi kama mnyama. Hakuwa na maarifa yoyote.
Kwa karne na karne mtu aliishi kwa kutumia akili ya ufahamu. Hakuweza kuendeleza mazingira.
Kwa ujio wa Yesu Kristo, kwa Kifo chake alimrejeshea binadamu hali ya sura na mfano wa Mungu yaani akili.
Yesu Kristo ndiyo chanzo cha maarifa yote. Ndiyo kwa njia yake binadamu anaweza kupata maarifa.
Maarifa tuliyonayo hii leo, maendeleo tulionayo hii leo ni kwasababu na kwa njia ya Yesu Kristo, Kifo chake.
Kabla ya Yesu Kristo mambo hayakuwa hivi yalivyo hii leo. Hakukuwa na maarifa pia maendeeleo kama haya baada ya Kristo.
Historia kabla ya Kristo haifahamiki kama ilivyo baada ya Kristo.
Hali ya mambo kabla ya Kristo ni ya kukanganya hivi kwamba inategemea maarifa baada ya Kristo kuitafiti.
Binadamu kabla ya Kristo, hata licha ya Mungu Mwenyewe kuwasaidia na wao wenyewe kumwomba Mungu kwa ajili ya ujio wa Kristo, bado hatahivyo, hali yao ya akili haikuwa imerejeshewa hadhi ile ya mwanzo ya kimungu tuliokuwa nayo kabla ya kosa la Adamu na Hawa.
Kwa ujio wa Kristo, kwa Kifo chake, tumerejeshewa hali ya kimungu yaani akili.
Pasipo Yesu Kristo, Kifo chake, mtu asingeweza kuwa na maarifa haya tuliyonayo nyakati hizi, maendeleo. Angebaki kama walivyo wanyama.
Hivyo, mtu anaekataa yale Yesu Kristo aliamuru kwa njia ya Kanisa lake yaani mitume hawezi kupata manufaa ya akili.
Kama lilivyo jua chanzo kikuu cha nishati duniani. Yesu Kristo ndiye chanzo cha maarifa na maarifa yenyewe. Yeye ndiye mwanga. Pasipo Yeye hakuna maarifa, wala maendeleo.
Haya nipe uthibitisho wa kipi umeona watu waliokuwa kabla ya yesu wamekitenda au kukifanya hadi kuwaona kuwa hawana uwezo wa kutambua, kuona, kufikiri na kuhukumu?Ni uwezo wa kutambua, kuona, kufikiri na kuhukumu.
Unafafanuaje uwezo wa kutambua ?Haya nipe uthibitisho wa kipi umeona watu waliokuwa kabla ya yesu wamekitenda au kukifanya hadi kuwaona kuwa hawana uwezo wa kutambua, kuona, kufikiri na kuhukumu
Kuna tofauti ya kuwa Mungu na hali ya kimungu.Kifo cha Yesu pale msalabani hakikumaanisha Mwanadamu kurejeshewa hali ya Kiungu huu ndio uongo shetani aliowadanganyia Adam na hawa pale Bustanini kwamba wakila tunda watakuwa kama Mungu!