Yemenikuta Mwenzenu

Yemenikuta Mwenzenu

kila siku kunaibuka mbinu mpya ya kuibiwa.
pole sana. tumejifunza kupitia yaliyokukuta.
 
Asanteni jamani, nashukuru Mungu hakunifanya kitu chochote zaidi ya kuchukua hizo pesa simu na kadi za benki ambazo napo by the time asubuhi nareport amekwisha toa hela zote kabakiza elfu kumi tu kwenye kila kadi.
Gari ilikuwa ni Verosa nyeupe namba T116 BGH nimejaribu kutrace na TRA wanasema imesajiliwa kwa jina la kampuni inaitwa African king cars ambao wao huagiza magari from abroad na kudistribute kwa dealers,wananisaidia kuangalia chasis number wajue waliziuza kwa dealer gani then dealer atasema alimuuzia nani then from there huyo mmiliki wa gari kama ndo yeye tapeli mwenyewe au si yeye atajua..nina hakika nitampata tu hata baada ya miaka mia saba na kama anasoma ajue kabisa.kwa kweli sijawahi kukasirika kama hivi loooh,nimejifunza..
 
hii kitu ina kozi zake bahati mbaya vitabu vyake viko mbali na hapa nilipo ila hapa nina dvd yake yenye koz hizo..lakini kozi zake ni kama hizi:

1. The Confident Hypnotist

This is a good course for beginners who want to gain confidence their voice tone, body language, gestures, breathing rate, timing etc. It contains valuable information if you want to eliminate failure while hypnotizing someone.

2. The Power Of Conversational Hypnosis

This was created by one of the greatest hypnotic minds of our century, Igor Ledochowski. The course is the most comprehensive, powerful and detailed conversational hypnosis course in the hypnosis world. Highly recommended!

3. The Art of Covert Hypnosis (iliyotumika kumlaghai huyu bidada)

This is a new course on covert hypnosis. this one is real course. The course teaches powerful hypnosis, NLP and mentalism techniques to guide you on how to hypnotize others covertly..

So kwa hiyo haihusishi uchawi wala mazingaombwe
 
Kwa kuwa una police report ya kuibiwa nenda TRA kaulizie details za mwenye hiyo gari zinaweza kukusaidia kujua pa kuanzia katika kumsaka huyo tapeli. Pole sana.
 
hakuna uchawi mkuu ni namna ya kucheza na akili ya mtu tu na kuzifata hatua kwa mikini bila kupoteza mwelekeo

Thanks.........kimsingi mtu wa aina hiyo ni lazima awe na confidence na akili yenye kufikiri kwa haraka. Na labda utujuze mtu anayetapeliwa ni lazima anayemtapeli awe na details zake au anamvaa mtu yeyote anayehisi ana mkwanja?

Hebu tupe step kwa step angalau kwa ufupi inavyofanyika:
 
Thanks.........kimsingi mtu wa aina hiyo ni lazima awe na confidence na akili yenye kufikiri kwa haraka. Na labda utujuze mtu anayetapeliwa ni lazima anayemtapeli awe na details zake au anamvaa mtu yeyote anayehisi ana mkwanja?

Hebu tupe step kwa step angalau kwa ufupi inavyofanyika:


ni lazima awe anajiamini sana na kama amesoma haya makitu lazima awe ameyaelewa vizuri na pia awe na uwelewa wa kutosha juu ya psychology....so haihitaji mpaka uwe na uhakika mtu flani ana pesa ndio umfanyie haya makitu..kwa aliyefuzi vizuri hii kitu anaweza kuyasoma mawazo ya mtu yeyote anayekutana nae na kujua nini kinaendelea katika kichwa chake na kwa haraka akaweza hypnotize...

kikubwa n kwamba katika hili yule anayefanyiwa huwa ana submit akili yake pasip kujua kwa huyu hypnotist na hypnotist akaikontroo akili ya mtendwa huku mtendwa akiwa na ufahamu kamili katika kichwa chake...

sasa inategemeana na njia anayoitumia huyo mtu maana zipo nyingi tu mfano:

1. Influence And Persuade People(Without Them Being Aware Of It) In Everyday Situations...

2 .How To Instantly DevelopA Deep Connection With People So You Can Almost "Read" Their Minds!

3.How To Alter Anyone's StateOf Mind On The Spot And Lead Them Into A Mesmerizing Hypnotic Trance!

4,Secrets Of Getting People To Follow Your Suggestions Without Giving It A Second Thought!

5.The Key To Changing Another Person's Behavior And Getting Them To Act Now On Your Specific Commands!


na nyingine nyingi...so kila moja ya hizo hapo juu ina hatua zake za kufata kulingana na mazingira na mtu unayetaka kum-hypnotize... i
 
shit happens,lamsingi samehe na sahau maisha yasonge mbele.

pole sana,kwa kweli hawa watu wanakera sana na wanarudisha nyuma maendeleo ya watu, hata mi nimejifunza not to talk with just anybody,especially strangers... unakuta mwingine from nowhere eti anakuuliza saa ngapi..!!? khaaa.. tena ukimjibu tu ndo kosa linapoanzia....
:A S cry:
 
ni lazima awe anajiamini sana na kama amesoma haya makitu lazima awe ameyaelewa vizuri na pia awe na uwelewa wa kutosha juu ya psychology....so haihitaji mpaka uwe na uhakika mtu flani ana pesa ndio umfanyie haya makitu..kwa aliyefuzi vizuri hii kitu anaweza kuyasoma mawazo ya mtu yeyote anayekutana nae na kujua nini kinaendelea katika kichwa chake na kwa haraka akaweza hypnotize...

kikubwa n kwamba katika hili yule anayefanyiwa huwa ana submit akili yake pasip kujua kwa huyu hypnotist na hypnotist akaikontroo akili ya mtendwa huku mtendwa akiwa na ufahamu kamili katika kichwa chake...

sasa inategemeana na njia anayoitumia huyo mtu maana zipo nyingi tu mfano:

1. Influence And Persuade People(Without Them Being Aware Of It) In Everyday Situations...

2 .How To Instantly DevelopA Deep Connection With People So You Can Almost "Read" Their Minds!

3.How To Alter Anyone's StateOf Mind On The Spot And Lead Them Into A Mesmerizing Hypnotic Trance!

4,Secrets Of Getting People To Follow Your Suggestions Without Giving It A Second Thought!

5.The Key To Changing Another Person's Behavior And Getting Them To Act Now On Your Specific Commands!


na nyingine nyingi...so kila moja ya hizo hapo juu ina hatua zake za kufata kulingana na mazingira na mtu unayetaka kum-hypnotize... i

kwenye purple kama nimekusoma vizuri huyu jamaa hana kesi ya kujibu
 
Kosa Ni ulipomsikiliza, usikae kumaikiliza mtu sentence ya pili Kama ya kwanza hukuelewa.


yamenikuta mwenzenu.

Ilikuwa ni siku ya jumatano saa tano asubuhi, nikiwa ndani ya quality centre nikaingia kwenye cash point kutoa pesa.pembeni kulikuwa na kijana anaongea na simu kwa nguvu.mimi nilikuwa na mwenzangu ambaye ndo alinifanya nikatoe pesa mana alikuwa ananidai, basi nilivyokwisha kuchukua pesa nikampa rafiki yangu za kwake zilizobaki nikaweka kwenye pulse haoo tukaondoka.

Tulipofika kwenye gari tukasikia mtu anaita kwa nguvu ''dadaa dadaa" yule mwenzangu akamwona akamwambia aniite, kumwangalia alikuwa ni yule kijana tuliomwona pale kwenye ATMs,akaomba kuongea nami nikatoka kwenye gari nikamsikiliza,kwakuwa nilikuwa naendesha gari la kampuni ambalo ni branded nadhani ndipo alipopatia mwanya wa kuanzia akasema anataka kufanya business na blabla kibao nikamwambia kwa wakati ule nipo busy itabidi nimschedule kwa kesho yake akasema yuko serious anataka akamilishe procedures zote za kufanya biashara na kampuni yetu, basi tukapanga tuonane jioni, kwa kuwa mimi sina usafiri binafsi nikachagua tuonane karibu na kazini ambapo ni quality centre lemon tree(msinijudge nature ya kazi yangu nafanya awkward hours),ikafika mida ya miadi nikaenda, yule jamaa alikuwepo akajitambulisha kwa jina la Paul Eric Shayo anafanya kazi Prime Minister's Office akanionyesha na ID yake,basi tukakaa kidogo tukaongea mara mwenzangu akasema twende peacock hotel kuna sehemu nzuri imetulia kwa juu,ila from the minute nimeongea nae mimi sikuwa normal nikawa najihisi kama nimekunywa pombe wakati niliagiza tu maji, na kila alichosema mi nilitii,basi tukaenda peacock hotel kuna kachilling place kule juu sijui kanaitwaje,cha kushangaza yule jamaa akawa haongei business tena akaanza kunambia kuwa amekuwa akifunga ili apate mke na Mungu kamuonyesha ni mimi,huyo mume niliyenae ni muigizaji tu,kwa kweli aliongea maneno mengi ya kutisha mpaka nikahisi sio binadamu yule kijana.akija muhudumu atamwambia "huyu mchumab wangu" akiongea na simu atasema "niko na mchumba wangu",nilistaajabu sana.wakati naondoka akaomba anipe lift nikakubali,kitendo cha mimi kuingia kwenye gari lake nilihisi kuishiwa na nguvu nikajikuta nipo pale shoprite pugu road kwenye ATM machine nakumbuka kumsikia ananiambia toa laki mbili na mimi nikatoa akasema lete kadi nikampa akachukua na pesa zote nilizokuwa nazo kwenye pochi..wakati huo wote nilikuwa kama mlevi fulani.nilikuwa nina mfuko una nguo na viatu vipya tukatoka hapo shoprite akaenda kwa speed mpaka mwenge pale bamaga kuna hotel pale kuna kagarden akasimamisha gari akanambia shuka haraka nikashuka akatoa gari kwa speed na mizigo yangu ikiwa mule ila pochi nilibeba,nilistuka baada ya dakika tano nikawa nimeshila wallet yangu nikaangalia hela hakuna kadi zote hakuna na niilmtajia mpaka pin.nikarudi nyumbani ila bado nilikuwa nayumbayumba.

Jamani kuna uwizi wa ajabu sana, jana nikaamua kumtafuta huyu mtu nikaenda polisi afu nikaenda kuulizia prime minister's office,waliulizana ofisi nzima mpaka HR wote waliangali majina ya watu wao lakini hakukuwa na jina hilo.NILITAPELIWA kwa kupumbazwa.ssa sijui ni dawa gani alitumia vipi mi sijui mana sikunyanyuka kwenda chooni tuseme ameweka kwenye kinywaji.nimekoma mie kuongea na strangers jamani nimekomaaaaa,hapa nilipo sina kadi naanza kuzunguka mapolisi na benki,kaniharibia financial situation yangu yote pumbavu zake nina hasira na nilishika namba yake ya gari kabla sijaingia kwa gari ni T 116 BGH.ninampango wa kumtafuta huyu mtu hata miaka mia nne ijayo lakini nitampata tuuu,nina hasira sana kama gari si lake basi mwenye gari atamtaja.

Wheeew jamani yamenikuta mwenzenu.
 
Pole sana mkuu.next time uwe makini na stragers.hii kitu ishamtoke dada mmoja mwanza.
 
Aisee pole sana, na asante kwa kuleta taarifa, wengine yasiwafikie
 
Watu wenye hasira kama wewe wanahitaji msaada wa FP.
 
Hiyo namba ya gari itakuwa ya uongo.

Wadada siku hizi wanatapeliwa sana kwa staili maana wengi wapo desperate na mambo ya mahusiano.
 
Utapeli!!

samehe tu dada!! Je ukupata utamfanya nini??

Mungu amekupa mikono na ubongo utapata tu vingine!
 
Shukuru hajakufanya kitu mbaya.We jipange upya,fedha ni matokeo.

Sent from my BlackBerry 9380 using JamiiForums
 
mhhh mbona dunia imebadilika binadamu hatuaminiani hee jamani mimi ndo maana hata simsalimiagi wala kumsikiliza mtu nisiyemjua khaaa simwamini banadamu yeyote jamani keeleeuuuwiii poel sana kua makini
 
Back
Top Bottom