Return Of Undertaker
JF-Expert Member
- Jun 12, 2012
- 4,572
- 26,868
Baada ya Kenya kuzuia ndege na abiria kutoka Tanzania, na sisi tumejibu mapigo. Mamalaka ya usafiri wa anga TCAA imepiga marufuku ndege zote zinazomilikiwa na shirika la ndege la Kenya Airways kutua katika ardhi ya Tanzania. Hii ina maana abiria wanaosafiri na Kenya Airways kutoka mataifa mengine kuja Tanzania watalazimika kuishia Nairobi, na kuunganisha ndege nyingine.
#MyTake:
Kwanza nadhani kuna mgogoro wa kidiplomasia ambao mamlaka hazitaki kuuweka wazi. Sidhani kama tatizo ni Covid19 kama inavyoelezwa. Nahisi kuna mengine yanaendelea ambayo wananchi hatuyajui. Ukiangalia trend ya matukio baina ya Kenya na Tanzania ni kama Korea Kaskazini na kusini. Hakuna kuaminiana, hakuna kuheshimiana, hakuna tena ujirani mwema. Kila mmoja anaonesha ubabe wake.
Pili, ukweli ni kwamba bado tunahitajiana sana. Kwenye biashara, kijamii, na kisiasa. Kuna watanzania wameoa Kenya and the vice versa. Wakenya wanategemea mazao ya chakula kutoka Tanzania. Zaidi ya 60% ya mazao ya nafaka (mahindi, mchele) yanayoliwa Kenya yanatoka Tanzania.
Na Tanzania inatumia sana bidhaa za viwanda kutoka Kenya. Takwimu zinaonesha kuwa Kenya ni nchi ya pili tunayofanya nayo biashara zaidi duniani. Yani tunafanya biashara zaidi na Kenya kuliko tunavyofanya na China, Marekani, au mataifa mengine makubwa.
Kwahiyo tunahitajiana sana. Hatua hii ya kutumishiana misuli inaathiri zaidi wananchi kuliko viongozi. Atakayeumia si Raila Odinga au Kassim Majaliwa. Ni kijana wa Sirari ambaye anategemea kuvusha mazao Kenya kujipatia riziki. Ni kijana wa pale Taveta mwenye kampuni ya utalii anayetegemea mlima Kilimanjaro.
Hii approach ya kutunishiana misuli si sahihi hata kidogo. Tukumbuke hata Jumuiya ya kwanza ya Afrika Mashariki ilivunjika mwaka 1977 baada ya chokochoko kama hizi.
Hivi tumekosa wanadiplomasia wazuri wa kusawazisha hizi tofauti hadi kufikia kutunushiana misuli hadharani? Kwanini Corona itusababishie uhasama?
Kama kila nchi imeamua kutafuta njia yake ya kupambana na Corona basi kila mmoja aheshimu maamuzi ya mwenzie na maisha yaendelee. Sio kuzozana na kutengeneza migogoro isiyo na sababu. Athari za kuwekeana uhasama na kuharibu undugu wetu ni kubwa kuliko athari za corona yenyewe.!
Na: Malissa GJ
#MyTake:
Kwanza nadhani kuna mgogoro wa kidiplomasia ambao mamlaka hazitaki kuuweka wazi. Sidhani kama tatizo ni Covid19 kama inavyoelezwa. Nahisi kuna mengine yanaendelea ambayo wananchi hatuyajui. Ukiangalia trend ya matukio baina ya Kenya na Tanzania ni kama Korea Kaskazini na kusini. Hakuna kuaminiana, hakuna kuheshimiana, hakuna tena ujirani mwema. Kila mmoja anaonesha ubabe wake.
Pili, ukweli ni kwamba bado tunahitajiana sana. Kwenye biashara, kijamii, na kisiasa. Kuna watanzania wameoa Kenya and the vice versa. Wakenya wanategemea mazao ya chakula kutoka Tanzania. Zaidi ya 60% ya mazao ya nafaka (mahindi, mchele) yanayoliwa Kenya yanatoka Tanzania.
Na Tanzania inatumia sana bidhaa za viwanda kutoka Kenya. Takwimu zinaonesha kuwa Kenya ni nchi ya pili tunayofanya nayo biashara zaidi duniani. Yani tunafanya biashara zaidi na Kenya kuliko tunavyofanya na China, Marekani, au mataifa mengine makubwa.
Kwahiyo tunahitajiana sana. Hatua hii ya kutumishiana misuli inaathiri zaidi wananchi kuliko viongozi. Atakayeumia si Raila Odinga au Kassim Majaliwa. Ni kijana wa Sirari ambaye anategemea kuvusha mazao Kenya kujipatia riziki. Ni kijana wa pale Taveta mwenye kampuni ya utalii anayetegemea mlima Kilimanjaro.
Hii approach ya kutunishiana misuli si sahihi hata kidogo. Tukumbuke hata Jumuiya ya kwanza ya Afrika Mashariki ilivunjika mwaka 1977 baada ya chokochoko kama hizi.
Hivi tumekosa wanadiplomasia wazuri wa kusawazisha hizi tofauti hadi kufikia kutunushiana misuli hadharani? Kwanini Corona itusababishie uhasama?
Kama kila nchi imeamua kutafuta njia yake ya kupambana na Corona basi kila mmoja aheshimu maamuzi ya mwenzie na maisha yaendelee. Sio kuzozana na kutengeneza migogoro isiyo na sababu. Athari za kuwekeana uhasama na kuharibu undugu wetu ni kubwa kuliko athari za corona yenyewe.!
Na: Malissa GJ