Yatokanayo na lockdown ya mtandao na maandamano

Yatokanayo na lockdown ya mtandao na maandamano

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
359,899
Reaction score
828,507
Niliyogundua katika zoezi hili la maandamano ni mengi sana, lakini haya machache tunaweza kujadiliana.

1. Hivi wale wanaotuma meseji za tuma kwenye namba hii walikuwa wapi? Maana sijapata meseji hiyo mpaka nimeihamu.

2. Wakina baba ni wapishi wazuri sana tatizo la kujua vipaji vyao ndio ilikuwa changamoto.

3. Watoto wengi wamepata fursa ya kujadiliana na wakina baba hasa masuala yahusuyo shule. ( wamefanikiwa kuwafahamu sura zao)

4. Kumbe tunaweza kulala saa 1 bila kupata konyagi, haya mazowea ni uongo tu usingizi upo.

5. Kanisa halihitajiki kwenye kupatanisha ndoa, just maandamano kikinuka familia zinaelewana.

6. Inawezekana kuamka na elfu kumi na ukalala ukiwa nayo.

7. Nyumba nyingi zinamjua Mungu hasa kwenye kusifu na kuabudu usiku mkubwa.

8. Biashara nzuri ni ya vyakula zingine mbwembwe tu za msimu.

9. Kufua na Saluni ni masuala ya kujitakia, dela linaweza kuvaliwa mwezi na kunyoa ndevu ni anasa.

10. Simba na Yanga ni vitu vinavyosahaulika kwa usiku mmoja tu, hata ikipigwa Derby unaweza usijue
1761567746037.jpg
 
11. Nimegundua mitaa ina watu ni vile tulikuwa hatufahamiani au kuonana. Kuna apartments zilifurika wapangaji wote wapo 24/7

12. Mabeki tatu tuwaangalie kwa jicho la tatu wanapiga sana kazi tukiwaacha majumbani

13. Maisha bila mtandao yanawezekana

14. Uchaguzi ujao 2030 ndani tuwe na food stocking ya kutosha, nishati kama gesi, mkaa hata kuni, madawa, cash, mifugo kama kuku na vibustani vya mboga za majani.

Hii iwe sehemu ya maisha haijalishi ni uchaguzi au pindi zingine
 
11. Nimegundua mitaa ina watu ni vile tulikuwa hatufahamiani au kuonana. Kuna apartments zilifurika wapangaji wote wapo 24/7

12. Mabeki tatu tuwaangalie kwa jicho la tatu wanapiga sana kazi tukiwaacha majumbani

13. Maisha bila mtandao yanawezekana

14. Uchaguzi ujao 2030 ndani tuwe na food stocking ya kutosha, nishati kama gesi, mkaa hata kuni, madawa, cash, mifugo kama kuku na vibustani vya mboga za majani.

Hii iwe sehemu ya maisha haijalishi ni uchaguzi au pindi zingine
Naendelea

11. Mboga zote ni tamu tatizo unakula katika mazingira gani.
12. Viazi na mihogo ni mbadala mzuri wa mkate, kununua mkate ni kuchezea hela tu.
13. Maisha bila mtandao yanawezekana ni mazowea mabaya tu.
14. Kumbe majirani wapo na ni watu wazuri sana kuongea nao na kuombeana kwa Mola.
15. Mji ni mtulivu kabisa na hauna foleni, sema tunapenda kuzurura sana.
16. Kumbe watu wana namba zetu za simu ila walikuwa hawawezi kupiga tu.
17. Aliyesema hatuwezi kufuata sheria tumlaani kabisa.
18. Sasa tumejua vitu vya msingi ndani ya nyumba kama akiba ya chakula, dawa, mishumaa na cash.
19. Nimegundua vipimo kama nusu na robo au robo havijatumika kabisa.
20. Kumbe kila mtu mjini anapo pa kulala sema huwa tunazembea kurudi home tu.

Mengine niliyogundua ni siri yangu na wewe iwe siri yako, muhimu tumegundua.
 
Back
Top Bottom