Yas yatoa msaada vifaa tiba Hospitali ya wilaya Chalinze

Yas yatoa msaada vifaa tiba Hospitali ya wilaya Chalinze

News TZ

Senior Member
Joined
Jun 17, 2015
Posts
169
Reaction score
88
chalinze1.jpg


KAMPUNI ya mawasiliano hapa nchini, Yas imeonesha dhamira yake ya dhati katika kuboresha ustawi wa jamii kwa kutoa msaada wa vifaa tiba muhimu katika Hospitali ya Wilaya ya Chalinze, mkoani Pwani.

Mpango huo, uliongozwa na Mkurugenzi wa Kanda ya Pwani Kusini, Fadhila Saidi ambaye alimkabidhi vifaa hivyo, Ramadhan Possi, Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya, kwa niaba ya Mganga Mfawidhi wa hospitali hiyo.
Msaada huo, ulijumuisha vitanda vya wagonjwa 15, mashuka 15, mizani ya watoto 2, kifaa cha kupasha joto watoto wachanga 1, mifuko ya kolostomi 100 na meza za Mayo 5.

Aidha, msaada huo ulitolewa kwa ajili ya Halmashauri ya Wilaya ya Chalinze na kuhudhuriwa na viongozi wa Halmashauri, wafanyakazi wa Yas na Mixx pamoja na wageni waalikwa.
“Kwa Yas, kutoa si tendo tu-ni taswira ya dhamira yetu ya kweli. Tunaamini kuwa kwa kuviwezesha vituo vya afya, tunajenga jamii imara na zenye afya bora.

“Kila mchango ni hatua ya kuanzia tulipo, kuelekea kesho yenye matumaini,”.
 
Back
Top Bottom