Yanga: Mashabiki komeni kuukurubia zaidi uongozi na wachezaji wenu.

kavulata

JF-Expert Member
Aug 2, 2012
12,319
12,622
Shabiki wa timu ni mhimili laini wa timu ambao kazi Yake kwenye timu ni kusimamia furaha yao isipotezwe na wachezaji, viongozi, wafadhili na wadhamini wa timu yao. Yaani malipo ya shabiki wa timu ni furaha TU ya ushindi wa timu. Mashabiki ndio mjeredi (whip) imara wa timu kuwafanya wachezaji, viongozi, na wadau wengine wasipotee kwenye malengo yao.

Kama Shabiki wa timu anapokuwa karibu zaidi na rafiki mkubwa wa uongozi, wachezaji na mfadhili wa timu ni sawa na Mbunge anapokuwa karibu zaidi na rafiki mkubwa wa serikali, atashindwa kuisimamia na kuikosoa serikali kikamilifu pale ubadhilifu na wizi ndani ya serikali utakapotokea.

Mashabiki wa timu kazi yetu ni kushangalia timu viwanjani na kununua brands za timu na wafadhili na kusubiri kulipwa furaha na wachezaji, uongozi na mfadhili. Kama shabiki atakuwa karibu mno na uongozi ni mbaya sana kwakuwa itampunguzia shabiki uwezo wake na nguvu zake za kumkosoa kiongozi, mchezaji, kocha au mfadhili pale timu itakapofanya vibaya; Utaona aibu kufanya hivyo.

Kuwa karibu zaidi na uongozi, kuitwa kunywa supu pamoja na uongozi na kuvaa misuri sikuungi mkono kwakuwa ni kama rushwa na pombe, inayolegeza nguvu za shabiki, kufunga mdomo, kupofua macho na masikio dhidi ya uongozi na mchezaji pale mambo yatakapokwenda vibaya. Kifupi ni rushwa ya mazingira ambayo itamlazimisha shabiki akae kimya milele na kusababisha migogoro miongoni mwa mashabiki wanaokunywa supu na wasiokunywa supu kama itatokea changamoto.
 
Acha kutupangia cha kufanya wewe Makolo. Mnatamani sana na sisi tuwe mbumbumbu kama nyinyi, jambo ambalo haliwezakani kamwe.

Mashabiki wengi wa Yanga, nikiwemo mimi! Bado tuna imani kubwa na timu yetu. Kwa juhudi wanazozionesha uwanjani, hatuna sababu ya kubweka bweka hovyo kama mbwa koko.

Wakati wa dirisha dogo, naamini benchi letu la ufundi litajazia mapengo yaliyopo.
 
Watasema wewe ni mnyama kisa umewaambia ukweli washabiki wenzio wa utopolo mlioshani huku klabu bingwa ni kwepesi kama kule kwa akina Zalan, Marumo na Bamako.
Huku ni kugumu sana, tokea msimu umeana hatujashinda hata mechi moja ni mwendo wa sare sare tu hata kwa timu zilizochini kabisa kwenye rank za CAF zimetutoa jasho na kuambulia sare tu.
 
ààll
Acha kutupangia cha kufanya wewe Makolo. Mnatamani sana na sisi tuwe mbumbumbu kama nyinyi, jambo ambalo haliwezakani kamwe.

Mashabiki wengi wa Yanga, nikiwemo mimi! Bado tuna imani kubwa na timu yetu. Kwa juhudi wanazozionesha uwanjani, hatuna sababu ya kubweka bweka hovyo kama mbwa koko.


Wakati wa dirisha dogo, naamini benchi letu la ufundi litajazia mapengo yaliyopo.
Sijasema timu yenu ni mbovu, bali checks and balance haiepukiki ili kila pande isibweteke, iwe na hofu ya kufanya kazi kwa mazoea. Barcelona, real Madrid, man City, man united ya Ferguson sikuhi kusikia mashabiki na uongozi wanakunywa mvinyo pamoja na kugongeana bilauri. Uongozi na Mashabiki wanakutanishwa kwenye meza moja siku ya kukabidhiwa makombe TU, kabla ya hapo viongozi na Mashabiki wanakutana viwanjani TU kwenye majukwaa tofauti.

Sasa hivi mtu kama god Yanga, Mwl Yanga au kigelegele anaweza kumlaumu hadharani BACCA akikosea uwanjani?
 
Shabiki wa timu ni mhimili laini wa timu ambao kazi Yake kwenye timu ni kusimamia furaha yao isipotezwe na wachezaji, uongozi na wafadhili wa timu yao. Yaani malipo ya shabiki wa timu ni furaha TU ya ushindi wa timu.

Shabiki wa timu anapokuwa karibu na rafiki wa uongozi, wachezaji na mfadhili wa timu ni sawa na Mbunge anapokuwa karibu zaidi na rafiki mkubwa wa serikali, atashindwa kuisimamia na kuikosoa serikali kikamilifu pale ubadhilifu na wizi ndani ya serikali utakapotokea.

Mashabiki wa timu kazi yetu ni kushangalia viwanjani na kununua brands za timu na wafadhili na kusubiri kuliowa furaha na wachezaji, uongozi na mfadhili. Kama shabiki atakuwa karibu mno na uongozi ni mbaya sana kwakuwa utampunguzia uwezo wake na nguvu zake za kumkosoa kiongozi, mchezaji, kocha au mfadhili timu itakapofanya vibaya; Utaona aibu kufanya hivyo.

Kuwa karibu zaidi na uongozi, kuitwa kunywa supu pamoja na uongozi na kuvaa misuri sikuungi mkono kwakuwa ni kama rushwa na pombe, inayolegeza nguvu za shabiki dhidi ya uongozi na mchezaji pale mambo yatakapokwenda vibaya.
Siyo kweli Tanzania tumefika hapa tulipo kwasababu ya kutokuhoji hili tatizo la kuhoji limeanzia ngazi ya familia familia nyingi huziruhusiwi kuhoji
 
Acha kutupangia cha kufanya wewe Makolo. Mnatamani sana na sisi tuwe mbumbumbu kama nyinyi, jambo ambalo haliwezakani kamwe.

Mashabiki wengi wa Yanga, nikiwemo mimi! Bado tuna imani kubwa na timu yetu. Kwa juhudi wanazozionesha uwanjani, hatuna sababu ya kubweka bweka hovyo kama mbwa koko.

Wakati wa dirisha dogo, naamini benchi letu la ufundi litajazia mapengo yaliyopo.
Wewe mbwiga huyo ni gongowazi mwenzako pimbi wewe
 
Acha kutupangia cha kufanya wewe Makolo. Mnatamani sana na sisi tuwe mbumbumbu kama nyinyi, jambo ambalo haliwezakani kamwe.

Mashabiki wengi wa Yanga, nikiwemo mimi! Bado tuna imani kubwa na timu yetu. Kwa juhudi wanazozionesha uwanjani, hatuna sababu ya kubweka bweka hovyo kama mbwa koko.


Wakati wa dirisha dogo, naamini benchi letu la ufundi litajazia mapengo yaliyopo.
Huyo utopolo mwenzenu
 
ààll

Sijasema timu yenu ni mbovu, bali checks and balance haiepukiki ili kila pande isibweteke, iwe na hofu ya kufanya kazi kwa mazoea. Barcelona, real Madrid, man City, man united ya Ferguson sikuhi kusikia mashabiki na uongozi wanakunywa mvinyo pamoja na kugongeana bilauri. Uongozi na Mashabiki wanakutanishwa kwenye meza moja siku ya kukabidhiwa makombe TU, kabla ya hapo viongozi na Mashabiki wanakutana viwanjani TU kwenye majukwaa tofauti.

Sasa hivi mtu kama god Yanga, Mwl Yanga au kigelegele anaweza kumlaumu hadharani BACCA akikosea uwanjani?
Mpira siyo vita, mpira siyo uadui, mpira siyo ugomvi, mpira siyo malumbano, na pia mpira siyo uhasama.

Na ndiyo maana nimekuambia timu yetu kwa sasa udhaifu wake mkubwa ni kwenye namba 9. Hivyo sioni sababu ya mashabiki kuanzisha taharuki isiyo na ulazima. Bado mashabiki wengi tuna imani na timu yetu.
 
Mpira siyo vita, mpira siyo uadui, mpira siyo ugomvi, mpira siyo malumbano, na pia mpira siyo uhasama.

Na ndiyo maana nimekuambia timu yetu kwa sasa udhaifu wake mkubwa ni kwenye namba 9. Hivyo sioni sababu ya mashabiki kuanzisha taharuki isiyo na ulazima. Bado mashabiki wengi tuna imani na timu yetu.
Kwasasa timu ni nzuri ndio maana watu wanaweza kukubali kuvaa misuli bila kuogoga kutabarukiwa. Lakini nguvu zenu za kuhoji mambo kama uwanja, mabadiliko yatamalizika lini, thanani ya mikataba kama Haier, whizom kwa timu zinadhoofishwa kwa kupewa supu,
 
Kwasasa timu ni nzuri ndio maana watu wanaweza kukubali kuvaa misuli bila kuogoga kutabarukiwa. Lakini nguvu zenu za kuhoji mambo kama uwanja, mabadiliko yatamalizika lini, thanani ya mikataba kama Haier, whizom kwa timu zinadhoofishwa kwa kupewa supu,
Mimi nadhani tuwape muda. Haya madhaifu ya timu hata wenyewe wanayaona.

Walimuuza Fiston Mayele, na kumleta Hafiz Konkoni, aliye prove failure!
Wameshindwa kumsajili namba 6 halisi, na badala yake wakatuletea Skudu ambaye kimsingi siyo namba 6!

Rais wa klabu aliahidi kwenye kampeni zake kuendeleza ule mradi wa Kigamboni kwa kujenga uwanja na hostel ya kisasa ya wachezaji! Lakini mpaka leo, bado hakuna kinachofanyika!!

So, i think time will tell.
 
Mimi nadhani tuwape muda. Haya madhaifu ya timu hata wenyewe wanayaona.

Walimuuza Fiston Mayele, na kumleta Hafiz Konkoni, aliye prove failure!
Wameshindwa kumsajili namba 6 halisi, na badala yake wakatuletea Skudu ambaye kimsingi siyo namba 6!

Rais wa klabu aliahidi kwenye kampeni zake kuendeleza ule mradi wa Kigamboni kwa kujenga uwanja na hostel ya kisasa ya wachezaji! Lakini mpaka leo, bado hakuna kinachofanyika!!

So, i think time will tell.
Wakati wa Nabi wachezaji wote walikuwa wana uwezekano wa kuanza au kuingia baadae, lakini Gamondi wachezaji ni haohao inyeshe mvua litoke jua, hii sio sahihi. Wakati wa Nabi hakukuwa na mchezaji mkubwa sana, lakini sasa wako wachezaji wakubwa sana, pangapangua watacheza. Hali hii inasababisha wachezaji wafiche maumivu yao na kuchezaja chini ya kiwango. Haiwezekani wachezaji kama Fred, Konkoni, skudu, nkane, farid, sure boy ghafla kwa Nabi wasiwe na uhakika wa kugusa mpira kiwanjani. Fresh legs ni muhimu sana kwenye mechi kaka.
 
Watasema wewe ni mnyama kisa umewaambia ukweli washabiki wenzio wa utopolo mlioshani huku klabu bingwa ni kwepesi kama kule kwa akina Zalan, Marumo na Bamako.
wasubiri pale watakapolitia tembo maji. Wahenga walifanyab utafiti wao miaka mingi sana kuwa mgema (mchezaji) ukimsifu sana atalitia maji tembo na kuiharibu pombe. Mashabiki kazi zao ni mbili tatu kushangilia (hamasa), kunuanua jezi na mambo yake na kukosoa wachezaji, uongozi na mwalimu baaasi. Shabiki hahitaji kufuatwa mtaani ili kuhamisishwa kwenda uwanjani, noooo!! Shabiki wa kweli apatie wachezaji wazuri, mwalimu mzuri, kandanda safi na matokeo mazuri kila wakati (consistently), atafurika mwenyewe uwanjani na kununua jezi. Shabiki ni kichocheo (whip) kwa viongozi, wachezaji na kocha, Hii ya kukaa meza moja na viongozi kunywa supu haipo, itamlemaza shabiki kuichochea timu yake kufanya vizuri, wataoneana haya kusemana ukweli pale mambo yatakapokuwa hayaendi sawa.
 
  • Thanks
Reactions: K11
Mind your own business, unajua ni kwann ikaitwa timu ya wananchi?
Kiongozi kuzunguuka mitaani na kispika kwenda kuita watu waende uwanjani ni njia nyingine safi ya kula fedha za klabu ambazo zinahitajika pia kwenye maendeleo ya timu kama ujenzi wa viwanja na hostel za wachezaji. Wananchi wanajazwa uwanjani kwa matokeo mazuri ya timu, sio kwenda kuwaita.

Timu imesajili kihalali wachezaji halali 27, Kwanini mashabiki waambiwe wamsifu mchezaji mmoja tu kwenye mechi? atacheza peke yake?, Ni njia ipi (sampling method) inatumika kumchagua mchezaji wa kusifiwa kwenye mechi husika? je, hiyo njia inayotumika iko wazi (unbiased) kwa kiasi gani? Je, wachezaji wote wanafahamu vigezo vya kuchaguliwa kuwa mchezaji wa mechi? njia na Vigezo hivyo haviwasumbui wachezaji wengine ambao hawajachaguliwa na ambao hawatachaguliwa hadi mwisho wa msimu?
 
Kiongozi kuzunguuka mitaani na kispika kwenda kuita watu waende uwanjani ni njia nyingine safi ya kula fedha za klabu ambazo zinahitajika pia kwenye maendeleo ya timu kama ujenzi wa viwanja na hostel za wachezaji. Wananchi wanajazwa uwanjani kwa matokeo mazuri ya timu, sio kwenda kuwaita.
Huo ni mtazamo wako, siyo lazima mtazamo wako ufanane na wangu, amini unachoamini na mimi niamini ninachoamini
 
Wakati wa Nabi wachezaji wote walikuwa wana uwezekano wa kuanza au kuingia baadae, lakini Gamondi wachezaji ni haohao inyeshe mvua litoke jua, hii sio sahihi. Wakati wa Nabi hakukuwa na mchezaji mkubwa sana, lakini sasa wako wachezaji wakubwa sana, pangapangua watacheza. Hali hii inasababisha wachezaji wafiche maumivu yao na kuchezaja chini ya kiwango. Haiwezekani wachezaji kama Fred, Konkoni, skudu, nkane, farid, sure boy ghafla kwa Nabi wasiwe na uhakika wa kugusa mpira kiwanjani. Fresh legs ni muhimu sana kwenye mechi kaka.
Unakumbaka nini kuhusu mechi dhidi ya Ihefu? Mashabiki mnaongoza kwa kugeuka geuka, Gamond alikuwa muumini sana wa kufanya rotation lakini hao hao wachezaji wakamuangusha akapata somo mawili. La kwanza kuhusu viwango vya wachezaji havifanani katika ubora na la pili mashabiki wakaanza kuonesha udhaifu wa kufungwa kumetokana na kocha kufanya rotation (kadharau mechi) hapo ndipo kocha alipojifunza kuwa kila mechi kwake ni fainali hivyo anapaswa kuweka kikosi chake cha uhakika.
 
Back
Top Bottom