Yanga kuikosa huduma ya Okwi

Yanga kuikosa huduma ya Okwi

Nahisi kuna utapeli umefanyika kupata ITC ya Okwi kutoka Uganda. ITC halali ilitolewa na TFF kwenda Etoile du Sahel, na bado timu hii inadai Okwi ni mchezaji wao halali, hivyo shirikisho la soka la Algeria halijatoa ITC yoyote kwa kutambua kuwa mgogoro wa mchezaji huyu bado upo FIFA. Hii iliyotolewa na FUFA kwenda Yanga imetoka wapi? Nadhani Yanga wameliwa!
 
Inasemekana TFF wanasubiri jawabu ya ufafanuzi kutoka FIFA kuhusiana na Okwi, anayesemakana kuishtaki Etoile kutomlipa mshahara, Etoile kumshtaki Okwi kwa kutoroka na Simba kuishtaki Etoile kwa kutowalipa hela yao. Atika mantiki ya kawaida, ni lipi kati ya hili linaloweza kumziwia mchezaji kuhamia timu nyengine, ilovyokuwa tayari alishahamishiwa Villa. Jawabu ni kuwa uhamisho wenyewe ulikuwa ni wa muda. Kuna kitu kama hicho FIFA? Na kama kiko, kanuni inasemaje juu ya mchezaji wa aina hiyo kuhama? Na kama kanuni hiyo iko, kwa nini TFF watake ufafanuzi? Mbona FUFA hwakutaka ufafanuzi? Swala la msingi ni vipi FIFA kama kweli kuna kesi hizo imebaki kimya muda wote huo, hata baada ya kuulizwa na TFF? Nadhani kwa hili kuna mawili, kutojiamini kwa TFF au siasa kuendelea ndani ya TFF. Ingawa binafsi siamini iwapo hata kama kuna kesi hizo.
 
umemaanisha Tunisia?
Nahisi kuna utapeli umefanyika kupata ITC ya Okwi kutoka Uganda. ITC halali ilitolewa na TFF kwenda Etoile du Sahel, na bado timu hii inadai Okwi ni mchezaji wao halali, hivyo shirikisho la soka la Algeria halijatoa ITC yoyote kwa kutambua kuwa mgogoro wa mchezaji huyu bado upo FIFA. Hii iliyotolewa na FUFA kwenda Yanga imetoka wapi? Nadhani Yanga wameliwa!
 
Rage aliwaambia kuwa kwenye suala la Okwi Yanga wameimgia chaka,naona kweli maneno yake aymeanza kutimia

Mkuu uende taratibu sana na Aden Rage

  1. Aliapa Twite hatachezea Yanga
  2. Mbele ya Mkutano wa Wanachama akasema "Wallah na saumu yangu Yondani hatachezea Yanga"
  3. Alijinasibu amemsainisha Keneth Asamoah

Rage ni muongo halafu ni msahaulifu
 
kumbe ni ndoto?
Jina la mchezaji Emmanuel Okwi kutoka Uganda halijaorodheshwa katika majina watakaoichezea klabu ya Yanga kwenye mzunguko wa ligi kuu ya Tanzania bara mzunguko wa pili.hii ni kutokana na sakata lake na Etoile du sahel kutokumalizika hivyo kwa mzunguko huu Yanga hawataweza kumtumia Okwi mpaka utata utakapoisha.

Jana Fredrick Mwakalebela kwenye akaunti yake ya facebook aliandika kuwa ameota kuwa sakata la Okwi limeibuka upya,leo hii habari hiyo imekuwa kweli.

Polen sana wana Yanga naona taratibu mnaanza kufuata nyayo za ubabaishaji za ndugu zenu Simba.

Source: shaffihdauda.com
 
Nahisi kuna utapeli umefanyika kupata ITC ya Okwi kutoka Uganda. ITC halali ilitolewa na TFF kwenda Etoile du Sahel, na bado timu hii inadai Okwi ni mchezaji wao halali, hivyo shirikisho la soka la Algeria halijatoa ITC yoyote kwa kutambua kuwa mgogoro wa mchezaji huyu bado upo FIFA. Hii iliyotolewa na FUFA kwenda Yanga imetoka wapi? Nadhani Yanga wameliwa!
Nimeikumbuka Kauli ya Hans Poppe; Okwi atacheza Mechi ya mtani jembe na si ligi kuu!
 
Nimatumaini yangu kama Okwi amebatirishwa Yanga basi na lile goli alilofunga kwenye mechi ya nani mtani jembe limebatirishwa namaanisha Simba alishinda 3:0
 
Nimatumaini yangu kama Okwi amebatirishwa Yanga basi na lile goli alilofunga kwenye mechi ya nani mtani jembe limebatirishwa namaanisha Simba alishinda 3:0

hahaa usije ukafanya wenzako wakakata rufaa
 
Maumivu ya kichwa huanza pole pole ..Mwaka wa tabu umeanza....!!Mzee Pluijm akae mkao wa mguu mmoja ndani mmoja nje!Hans poppe alitahadharisha hayo siku nyingi!!!
 
Nena Mkuu kwa kuwa mtumishi wako anasikia.
Sijaona ukitupia neno kwenye huu uzi toka jana, kulikoni ong'wise, Inaonekana waarabu wa Tunisia wameamua kuwasaidia waarabu wenzao wa Misri maana ndo huyu huyu Okwi alifunga goli la ugenini na kuwatoa waarabu wa Algeria mwaka ule, waarabu wa Tunisia wamepeleka jina lake kwa ajili ya mashindano ya CAF, leta maoni yako kuhusiana na hili sakata.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom