Yanayojiri: Kwa SMS Hivi Sasa

Yanayojiri: Kwa SMS Hivi Sasa

Pole na Majukumu ya kila siku Mtanzania Mwenzangu, vipi Umeshapata MAISHA BORA kama walivyokuahidi CCM Mwaka 2005 Na 2010? Anayekuuliza sio Mwanasiasa! Yaani, Mwanaharakati!! Hebu jiulize
wanaotoa Ahadi Wanakuonaje Wewe?
1.Ni -----
2.Ni Mjinga
3.Mpumbavu
4.Mwehu
5.Mwendawazimu
6.Una Ubongo wa kuku Yaani, Msahaulifu.
Mbona Wenyewe wana Maisha Bora! Kwanini wewe huna au Wenzetu sio Watanzania? Kazi Kwako Mwaka 2015 Nikutakie Tafakari Njema MATUMAINI NA JIoni NJEMA

Vipi zile ambulance alizopewa msaada Lema pale Arachuga ameshazipeleka kwa wananchi au bado zimebadilishiwa matumizi?
 
Maisha bora hayaletwi na serikali mkuu. Ukisubiri serikali utajikuta unazeeka na mawazo kama wazee wa EA

kweli nakuunga mkono ila nilitegemea kuwa maisha bora yangekuwa nikienda hospital ya uma nipate matibabu na dawa,maji safi,elimu nzuri na nimsomeshe mtoto shule ya umma...
haya mambo yamekuwa kinyume ndio maana maisha bora hayajatimia
 
Maisha bora hayaletwi na serikali mkuu. Ukisubiri serikali utajikuta unazeeka na mawazo kama wazee wa EA

kwa io nikienda hospitak niende na dawa zangu? niwe na kampuni yangu ya kuniletea maji nyumbani? tatizo lenu mna jua maisha bora ni kua na nyumba na spacio,msiwe wabinafsi nyie watu njoo kijijin huku uone watu wanavyo teseka kwa kukosa huduma muhimu za kibinadamu....huyo mwenyekiti wenu anajua alicho kua ana maanisha alivyo kua anasema "maisha bora kwa kila mtanzania"
 
Sikuhitaji ahadi za CCM au chama chochote kujitengenezea maisha bora... yes nina maisha bora ukilinganisha na 2005, 2010 lakini kwa juhudi zangu... Na ukweli utaendelea kuwa hivyo daima.

Maisha bora ni mipango na jitihada zako.

Maisha bora hayaletwi na serikali mkuu. Ukisubiri serikali utajikuta unazeeka na mawazo kama wazee wa EA

Kama mlijua hivyo kwa nini hamkuwapiga wanafik walipowadanganya watanzania kuwa watawaletea maisha bora? Au nyie wenyewe ni vipofu kisiasa?
 
Lema, Mbowe na Slaa hawakuahidi mtu yeyote maisha bora kwa kila mtanzania.. Msiwe wanafiki kwa kukwepa hoja kijinga jinga. Kikwete na wafuasi wake walikiri wenyewe kuwa wana uwezo kuwafanya watanzania waishi maisha bora. Je, wametimiza ahadi yao? Msilete longo longo.

Vipi zile ambulance alizopewa msaada Lema pale Arachuga ameshazipeleka kwa wananchi au bado zimebadilishiwa matumizi?

Kwani anayoahidi Slaa na Mbowe lipo hata moja walilofanikisha kwa asilimia 70 ?
 
Lema, Mbowe na Slaa hawakuahidi mtu yeyote maisha bora kwa kila mtanzania.. Msiwe wanafiki kwa kukwepa hoja kijinga jinga. Kikwete na wafuasi wake walikiri wenyewe kuwa wana uwezo kuwafanya watanzania waishi maisha bora. Je, wametimiza ahadi yao? Msilete longo longo.

Kwani kuleta zile ambulance kwa wana Arusha sio maisha bora! Na si ilikuwa ni moja ya ahadi zake kwenye kampeni! au kunya anye bata tu!!!
 
Sikuhitaji ahadi za CCM au chama chochote kujitengenezea maisha bora... yes nina maisha bora ukilinganisha na 2005, 2010 lakini kwa juhudi zangu... Na ukweli utaendelea kuwa hivyo daima.
Hata wauza unga,pembe za ndovu na watoto wa mafisadi wamefanikiwa sana kipindi hiki Uko sawa yawezekana Uko kundi hilo sishangai,kama deni LA Taifa limeongezeka, dawa hospital hakuna hiyo JUHUDI yako binafsi imetatuaje kuhusu Tanzania
 
Kama mlijua hivyo kwa nini hamkuwapiga wanafik walipowadanganya watanzania kuwa watawaletea maisha bora? Au nyie wenyewe ni vipofu kisiasa?

Mbona unafanya kila mtu mwanasiasa; Nyie mnadhani kuna chama kitaenda chakula kwenye meza yako... utakufa maskini!
 
Maisha bora hayaletwi na serikali mkuu. Ukisubiri serikali utajikuta unazeeka na mawazo kama wazee wa EA

Kwa nini serikali iliweka ahadi na hayaletwi na serikali? Mbona aliyoahidi Obama kwa serikali yake kwa watu wake karibu yote yamefikiwa?
 
Sikuhitaji ahadi za CCM au chama chochote kujitengenezea maisha bora... yes nina maisha bora ukilinganisha na 2005, 2010 lakini kwa juhudi zangu... Na ukweli utaendelea kuwa hivyo daima.

Kabisa, naona umejenga Shule yako, Hospitali yako, Unadhibiti thamani ya shilingi, umejenga barabara, na unapanga vizuri matumizi ya kodi zinazolipwa. Hakika huhitaji serikali ili jamii iwe na maisha bora.
 
Kabisa, naona umejenga Shule yako, Hospitali yako, Unadhibiti thamani ya shilingi, umejenga barabara, na unapanga vizuri matumizi ya kodi zinazolipwa. Hakika huhitaji serikali ili jamii iwe na maisha bora.
Source ya hela za Serikali ni kodi zetu!

na najivunia kwamba nalipa kodi nzuri; so I'm doing my job kuhakikisha maskini wazee na watoto wanapata hizo huduma; wengine fanyeni kazi... huduma za serikali ni basic services; maisha bora ni wewe mwenyewe!

Ndio maana pamoja na kuchangia serikaili kupitia kodi yangu; sitibiwi kwenye hospital zao, na sisomeshi watoto wangu kwenye shule zao... hope this make sense.
 
Back
Top Bottom