- Thread starter
- #41
Maisha bora ni mipango na jitihada zako.
Kwa hiyo, Ilani za Uchaguzi za CCM kwa kila uchaguzi ni changa la macho?
Kwa hiyo, mawaziri, viongozi wa CCM wanaopita huku na huko kukagua utekelezaji wa ilani ya chama ni wazushi?
Kwa hiyo, bajeti za maendeleo za kila wizara kila mwaka ni changa la macho na wizi mtupu wa viongozi wa serikali ya CCM?
Kwa hiyo, kodi tunatozwa na kulipishwa kodi kwa kila bidhaa na huduma ni kwa ajili ya mafisadi CCM na sio kwa maendeleo ya wananchi?
Kwa hiyo, unataka kusema, hospitali na vifaa tiba vyake vitaendelezwa na kila mwananchi kwa mpango wake?
Kwa hiyo, Tanzania chini ya mafisadi CCM ni nchi ya pekee ulimwenguni ambayo serikali yake haijihusishi na kuwaletea maendeleo wananchi wake?
Huyo Chikwete, CCM no.1, huo uvasco da gama anaoufanya haujamwezesha kujifunza kuona kwamba maendeleo ya CHINA na Vietnam alikotoka yametokana na serikali!
Ama kweli! CCM janga la kitaifa! Ndio maana kumbe elimu inabomoka kila uchao, hospitali hazina dawa wala vifaa tiba. Umasikini miongoni mwa watanzania unapaa kila siku!