PreGE2025 Kesi ya Uhaini inayomkabili Tundu Lissu yaahirishwa hadi Juni 16

PreGE2025 Kesi ya Uhaini inayomkabili Tundu Lissu yaahirishwa hadi Juni 16

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla)

Blessed Tajiri

JF-Expert Member
Joined
Dec 16, 2023
Posts
221
Reaction score
659
1000192774.jpg

Leo ni wakati mwingine tena wa kusikiliza kesi zinanzomkabilo Tundu Lissu.

Nini kitajiri, tutarajie kusikia habari mpya ya Lissu kuachiwa?

Wacha tuone nini kitajiri.



====================================

Mwenyekiti wa CHADEMA, Tundu Lissu amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kwa ajili ya kusikilizwa kwa kesi za jinai zinazomkabili ikiwemo kuchapisha taarifa za uongo mtandaoni.

Lissu ambaye hivi karibuni amechaguliwa kuwa Makamu Mwenyekiti wa International Democrat Union (IDU) anakabiliwa na kesi mbili mbele ya Mahakimu wawili tofauti.

Makama Mwenyekiti wa CHADEMA, John Heche alivyotinga kwenye Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kusikiliza kesi inayomkabili Mwenyekiti wa Chadema, Tundu Lissu.

Aliyewahi kuwa Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na MaendeleoCHADEMA. Wilbroad Slaa akiingia katika viunga vya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar Es Salaam kwa ajili ya kufuatilia kesi zinazomhusu Mwenyekiti wa chama hicho Tundu Lissu


Godbless Lema awasili ndani ya chumba cha Mahakama, ulinzi waimarishwa.


Ulinzi mkali umetawala katika eneo la Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu wakati wa kusikiliza kesi inayomkabili Mwenyekiti wa Chadema, Tundu Lissu

Askofu Mwamakula akiongoza maombi ndani ya chumba cha Mahakama



Dakika 11 za wakili Peter Kibatala akijibu hoja za mawakili wa serikali waliosema lissu ametukana ndani ya mahakama kwa kusema 'No reforms No election'

==========================================

Kesi ya Mwenyekiti wa CHADEMA, Tundu Lissu, imeahirishwa hadi Juni 16, 2025 katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu. Mahakama imempa onyo kali kwa kutamka kauli ya "No reform, no election" bila ruhusa akiwa ukumbini, ikitafsiriwa kama dharau kwa Mahakama.

Lissu anadaiwa kutoa maneno ya uchochezi Aprili 3, 2025 jijini Dar es Salaam, akihamasisha kuzuia Uchaguzi Mkuu wa 2025 na kumshinikiza kiongozi wa serikali.






 

Attachments

  • snapins-ai_3645907474704470932.mp4
    8.3 MB
Tunamshukuru Mungu hata katika haya magumu wanayotutendea watawala mawakala wa shetani. Kama Mungu wetu wa haki amependa ukombozi wa Taifa upitie njia hii, tutaendelea kumshukuru, maana tumeaswa kuwa tushukuru kwa kila jambo.

Labda Mungu ametaka kabla ya ukombozi, awaoneshe wananchi wote ili wapate kujua walikuwawanatawaliwa na mashetani ya kiwango kikubwa.

Anayeitafuta haki ni mtumishi wa Mungu, anayedhulumu haki ni mtumishi wa shetani.

Tukatae Samialization, maana samialization ni kuishi katika ushetani wa kudhulumu haki za binadamu.

Mungu wetu, tunaomba neema za pekee kwaajili ya mtumishi wako Tundu Lisu, na laana kuu kwaajili ya waumini wa samialization.
 
Back
Top Bottom