Yamenikuta: Mchepuko umetibua ndoa

Msanii

Platinum Member
Joined
Jul 4, 2007
Posts
26,362
Reaction score
39,842
Nilikuwa nakatiza maeneo ya Chang'ombe nikamwona mrembo anatembea juani alionekana amechoka, nikampa lifti kumsogeza mjini baada ya kumuuliza aendako,tulibadilishana anuani na tukawa tunawasiliana.

Binti mwenyewe ni mrembo na ameumbika kike haswaa. Sasa siku tuliyoonana tena nikajiona sana kumuachia hivyo nikaimba beti chache na hatimaye nikatusua mtoto. ikumbukwe hapo nimeoa.

Baada ya mchezo ule nilijuta kiasi ila nikanogewa tukawa tunabanjua amri ya sita kila mara bila kutambulika. Lakini hakuna marefu yasiyo na ncha, hatimaye nikagundulika na wife kwamba nakimbia mwenge nje ya chumba.

Moto uliowashwa daah sitausahau. Nahisi binti alikuwa ameniwekea kitu nijione nafanya jambo sahihi na baada ya kugundulika na wife ndo nikagundua upuuzi nilioufanya na almanusura ndoa ivunjike.

Ila nimemsihi sana wife anisamehe na sitarudia tena. Mke tunaendelea kuishi wote ila bado haniamini kwa hayo yaliyotokea.

Kiufupi ni kwamba nilitopea baada ya kuona nyumbani nakumbana na full stress na nakosa faraja, amani na upendo hivyo nikajiona nipo right kabisa kufanya dhambi ambayo leo naijutia.

Sharti alilonipa ni kwamba yeye ameandaa vijana wake hivyo nimlete yule binti ili abakwe mbele yake na kadhalika. Kitu hiko nimemwambia ni kinyume na utu na ni kuvunja sheria, ugomvi umeanza upyaaa.

Anasema kuwa namkwepesha huyo binti kwa kuwa nampenda. Naomba ushauri nifanyeje hapo maana ingawa najutia kosa langu lakini sipendi kutenda kosa la unyama kiasi hiki.



 
Tena fanya haraka mpeleke huyo bint kabla ya yote aliwe mbele yako na hasira yake iishe okoa ndoa mchepuko hauna maana ss fanya haraka
 
nabii mweusi

Binti akienda kushtaki polisi itakuwaje? Hapo ndo hofu yangu ilipo
 
Last edited by a moderator:
Aiseeee.......
Pole kwa masahibu Msanii
 
Last edited by a moderator:
Leo ahsubuhi ninampeleka kazini. anatoa machozi nikimuuliza hataki kusema, baadaye amenipigia anasema kuwa ninamkwepesha yule binti hivyo bado ana uhakika naendelea naye.

Kiufupi ni kwamba anayo namba yake na wameshawasiliana sana na ameshapafahamu kwao. Najiuliza kwa nini anihusishe mimi ktk mpango wa kijinai?
 
nenda wewe ukaliwe badala ya huyu mchepuko wako
 
Huo sio ubinadamu, kwani alikulazimisha kuwa nae? Halafu sisi wanawake huwa hatujiongezi tu, badala ya kudeal na tatizo ulilonalo ndani unakwenda kuparamia aliyetobgozwa.

Wewe mume ungekuwa na msimamo huyo dada angekulazimisha? Mkeo a napaswa akae nawewe akueleze madhara ya kutoka nje ya ndoa na akuulize sababu ya wewe kuamua hivyo.

Maana kama ni tabia yako utampeleka huyo binti wa watu atabakwa then utatafuta mwingine mwisho wa siku mtabakisha wangapi? Mwogopeni Mungu hiyo sio suluhu. Mnatakiwa muelezane kilichopungua badala ya kuadhibu wapita njia.
 
Nakushauri usifanye hivyo kwani huyu bnt hakukutongonga ni ww mwenyewe na matamanio yako cha msingi mwelee mkeo kuwa ulifanya vile kwa sababu hizo ambazo umetueleza so hakunahaja ya kumuhukumu binti wa watu wakat yeyekatongozwa kama ulivyomtongoza yeye hata kama kakukuta na kosa kuwa mkali sio akuendeshe na kwa ninavyokuona unaendeshwa kama gar bovu.
 
Nominomi

Nimejaribu kumsihi sana mke wangu kwamba pamoja na yote mimi ndiye mkosaji lakini yeye anashikilia msimamo kwamba kwa nini binti yule akubali kulala na mimi huku akijua kuwa nimeoa?

Nimejaribu kumwomba tukaombewe kanisani hasa mimi ili nisirejee upuuzi ule anasema huko hakuna jipya na msimamo wake ni ule ule. Ila ukweli nimemuudhi pamoja na kwamba ana hasira lakini utu wema ni silaha dhidi ya dhambi.
 
Last edited by a moderator:

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…