Msanii
Platinum Member
- Jul 4, 2007
- 25,946
- 38,665
Nilikuwa nakatiza maeneo ya Chang'ombe nikamwona mrembo anatembea juani alionekana amechoka, nikampa lifti kumsogeza mjini baada ya kumuuliza aendako,tulibadilishana anuani na tukawa tunawasiliana.
Binti mwenyewe ni mrembo na ameumbika kike haswaa. Sasa siku tuliyoonana tena nikajiona sana kumuachia hivyo nikaimba beti chache na hatimaye nikatusua mtoto. ikumbukwe hapo nimeoa.
Baada ya mchezo ule nilijuta kiasi ila nikanogewa tukawa tunabanjua amri ya sita kila mara bila kutambulika. Lakini hakuna marefu yasiyo na ncha, hatimaye nikagundulika na wife kwamba nakimbia mwenge nje ya chumba.
Moto uliowashwa daah sitausahau. Nahisi binti alikuwa ameniwekea kitu nijione nafanya jambo sahihi na baada ya kugundulika na wife ndo nikagundua upuuzi nilioufanya na almanusura ndoa ivunjike.
Ila nimemsihi sana wife anisamehe na sitarudia tena. Mke tunaendelea kuishi wote ila bado haniamini kwa hayo yaliyotokea.
Kiufupi ni kwamba nilitopea baada ya kuona nyumbani nakumbana na full stress na nakosa faraja, amani na upendo hivyo nikajiona nipo right kabisa kufanya dhambi ambayo leo naijutia.
Sharti alilonipa ni kwamba yeye ameandaa vijana wake hivyo nimlete yule binti ili abakwe mbele yake na kadhalika. Kitu hiko nimemwambia ni kinyume na utu na ni kuvunja sheria, ugomvi umeanza upyaaa.
Anasema kuwa namkwepesha huyo binti kwa kuwa nampenda. Naomba ushauri nifanyeje hapo maana ingawa najutia kosa langu lakini sipendi kutenda kosa la unyama kiasi hiki.
Binti mwenyewe ni mrembo na ameumbika kike haswaa. Sasa siku tuliyoonana tena nikajiona sana kumuachia hivyo nikaimba beti chache na hatimaye nikatusua mtoto. ikumbukwe hapo nimeoa.
Baada ya mchezo ule nilijuta kiasi ila nikanogewa tukawa tunabanjua amri ya sita kila mara bila kutambulika. Lakini hakuna marefu yasiyo na ncha, hatimaye nikagundulika na wife kwamba nakimbia mwenge nje ya chumba.
Moto uliowashwa daah sitausahau. Nahisi binti alikuwa ameniwekea kitu nijione nafanya jambo sahihi na baada ya kugundulika na wife ndo nikagundua upuuzi nilioufanya na almanusura ndoa ivunjike.
Ila nimemsihi sana wife anisamehe na sitarudia tena. Mke tunaendelea kuishi wote ila bado haniamini kwa hayo yaliyotokea.
Kiufupi ni kwamba nilitopea baada ya kuona nyumbani nakumbana na full stress na nakosa faraja, amani na upendo hivyo nikajiona nipo right kabisa kufanya dhambi ambayo leo naijutia.
Sharti alilonipa ni kwamba yeye ameandaa vijana wake hivyo nimlete yule binti ili abakwe mbele yake na kadhalika. Kitu hiko nimemwambia ni kinyume na utu na ni kuvunja sheria, ugomvi umeanza upyaaa.
Anasema kuwa namkwepesha huyo binti kwa kuwa nampenda. Naomba ushauri nifanyeje hapo maana ingawa najutia kosa langu lakini sipendi kutenda kosa la unyama kiasi hiki.
MREJESHO
Baada ya kuweka kesi yangu hapa nilipata mawazo mengi yanayojenga na hatimaye niliongezeka ujasiri. Ingawa mkosaji ni mimi lakini sikuona maana yeyote ya kutekeleza matakwa ya wifey as collateral ya umaluuni wangu.
Namshukuru sana Mwana JF mmoja aliyenijenga kifikra, dada huyu sitamsahau maishani kwani aliamua kubeba jukumu yeye mwenyewe na akawa ananishauri bila kuchoka na hata nilishare naye vitu vingi vya msingi ambavyo hata yeye alishangaa kuwepo na hayo mambo. Unajua mostly inaonekana WANAUME tuna makosa sana kutoka nje ila kuna slightly errors ambazo wake zetu wanafanya ambazo zinakupeleka moja kwa moja nje ya mipaka ya viapo vya ndoa.
Hivi sasa ninavyoongea mke wangu amepoa na ameacha vitisho vyake na hakuna tena kuvurugana ingawa hali inatulia kwa muda na kulipuka tena lakini kadiri siku zinavyokwenda ndivyo anazidi kuwa mpole. Ameelewa hatari ya kufanya kosa kama ngazi ya kurekebisha kosa la awali.
Nawashukuru sana JF mmenisaidia kisaikolojia na kuokoa ndoa yangu isisambaratike...