Malyenge
JF-Expert Member
- Jan 16, 2012
- 6,658
- 3,662
Wakuu natumaini hamjambo,
Leo napenda niwaeleze jinsi baadhi ya mikoa yetu ilivyo nyuma kimaendelo na tulikuwa hatujui sababu ya mikoa hiyo kuwa nyuma kimaendeleo. Lakini kwa safari yangu ya Tabora mjini nimegundua ni kutokana na upeo mdogo wa wananchi wa mikoa hiyo iliyo nyuma kimaendelo.
Ni kwamba nilikuwa likizo ya mwaka haki ambayo kila mtumishi anapaswa kupewa. Nilipomaliza likizo yangu usiku wa kuamkia tarehe 15 Mwezi huu nililala kwenye hoteli moja mjini Tabora karibu na stendi kwa ajili ya kujidamkia mabasi yanayokuja Dar Es Salaam ambayo saa ya kuripoti ni saa kumi na moja na nusu alfajiri. Nilifuata taratibu zote za kihoteli na ilipofika saa kumi na moja na robo alfajiri nilikuwa tayari (mimi na mke wangu) kwa safari.
Kufika mapokezi hatukukuta muhudumu yeyote. Nilijaribu kuita kwa sauti kumwita mhudumu atufungulie mlango tuondoke lakini hakuna dalili ya kuitikiwa. Bahati nzuri kuna mteja mwingine naye alikuwa akisafiri alfajiri hiyo naye akaja tukaungana kumtafuta muhudumu bila mafanikio.
Ndipo kwa kutumia maarifa mengine nikajaribu kumwita mlinzi wa nje huko getini aje atusaidie kutufungulia ama kumtafuta muhudumu atufungulie. Lakini tulishindwa kwa sababu getini ni mbali sauti zetu hazikumfikia mlinzi. Ndipo nikapata wazo la kumpigia simu jamaa yangu mmoja aliyepo Tabora mjini aje amgongee mlinzi kisha amfahamishe kuna watu ndani wanahitaji kutoka hotelini lakini hawamwoni muhudumu.
Wazo langu lilifanikiwa maana jamaa akaja akamgongea mlinzi wa hoteli na kumfahamisha ya kuwa muhudumu haonekani na kuna watu wanahitaji kutoka hotelini. Ndipo mlinzi alipomtafuta muhudumu akampata (sijui alimpata wapi hilo sijui). Muhudumu akaja kutufungulia lakini akiwa katika hali ya ulevi.
Baada ya kutufungulia (yule mteja mwingine amekasirika kupita maelezo) ndipo nikamwambia muhudumu nikiwa nimesimama mlangoni kuwa wasilalamike kutopata wateja maana moja ya sababu yawezekana ikawa ni hii aliyotufanyia leo.
Muhudumu akanijibu ".......hata usipokuja tena kwani mteja ni wewe peke yako? Nipishe nifunge mlango......." Huku akinisukumiza na mlango nitoke mlango ukabamiza mabegi niliyokuwa nimeshika mkononi na matairi ya mabegi yakavunja vioo vya mlango huo.
Kilichofuatia akaamuru mlinzi afunge geti tusitoke mpaka hapo polisi watakapokuja. Nikafungiwa ndani ya geti la hoteli kuanzia saa 11 dk 29 alfajiri mpaka polisi walipokuja saa 1 dk 40 asubuhi. Wakaja wakanikamata kwa tuhuma ya kuingia hotelini kwa nia ya kuharibu mali!
Kwa hiyo basi likaniacha na safari ikawa imekufa!
Nikawekwa mahabusu mpaka saa 5 na nusu asubuhi yule jamaa yangu alipotafuta watu wa kuja kunitolea dhamana. Kesi ikaamuliwa nilipe mlango wa hoteli shilingi LAKI SABA ili nisipelekwea mahakamani. Nikawaomba badala ya kulipa pesa mimi nitafute fundi aje atathmini gharama kisha atengeneze nimlipe.
Suala ni kutengeneza mlango....Nilipata upinzani mkali sana polisi kwamba nawafundisha kazi. Nikawaambia sheria za nchi yetu siyo nzuri,mlalamikaji anaaminiwa sana kuliko mshitakiwa.
Wao walikuwa na uthibitisho gani kuwa mimi niliingia hotelini kwa nia ya kuharibu mali? Aliyevunja ni muhudumu siyo mimi!!
Hatimaye ikakubalika nitafute fundi. Nikampata fundi gharama ya kioo ikawa ni shilingi elfu ishirini na ufundi ni shilingi elfu kumi tu. Mlango ukawa umekamilika kutengenezwa saa 7 dk 36 mchana.
Hayo ndiyo yaliyonikuta Tabora. Mlango wenyewe ni huu nilio u atach na muhudumu mwenyewe ni huyo dogo mwenye shati jekundu. Ameniboa sana........!!!!!
Leo napenda niwaeleze jinsi baadhi ya mikoa yetu ilivyo nyuma kimaendelo na tulikuwa hatujui sababu ya mikoa hiyo kuwa nyuma kimaendeleo. Lakini kwa safari yangu ya Tabora mjini nimegundua ni kutokana na upeo mdogo wa wananchi wa mikoa hiyo iliyo nyuma kimaendelo.
Ni kwamba nilikuwa likizo ya mwaka haki ambayo kila mtumishi anapaswa kupewa. Nilipomaliza likizo yangu usiku wa kuamkia tarehe 15 Mwezi huu nililala kwenye hoteli moja mjini Tabora karibu na stendi kwa ajili ya kujidamkia mabasi yanayokuja Dar Es Salaam ambayo saa ya kuripoti ni saa kumi na moja na nusu alfajiri. Nilifuata taratibu zote za kihoteli na ilipofika saa kumi na moja na robo alfajiri nilikuwa tayari (mimi na mke wangu) kwa safari.
Kufika mapokezi hatukukuta muhudumu yeyote. Nilijaribu kuita kwa sauti kumwita mhudumu atufungulie mlango tuondoke lakini hakuna dalili ya kuitikiwa. Bahati nzuri kuna mteja mwingine naye alikuwa akisafiri alfajiri hiyo naye akaja tukaungana kumtafuta muhudumu bila mafanikio.
Ndipo kwa kutumia maarifa mengine nikajaribu kumwita mlinzi wa nje huko getini aje atusaidie kutufungulia ama kumtafuta muhudumu atufungulie. Lakini tulishindwa kwa sababu getini ni mbali sauti zetu hazikumfikia mlinzi. Ndipo nikapata wazo la kumpigia simu jamaa yangu mmoja aliyepo Tabora mjini aje amgongee mlinzi kisha amfahamishe kuna watu ndani wanahitaji kutoka hotelini lakini hawamwoni muhudumu.
Wazo langu lilifanikiwa maana jamaa akaja akamgongea mlinzi wa hoteli na kumfahamisha ya kuwa muhudumu haonekani na kuna watu wanahitaji kutoka hotelini. Ndipo mlinzi alipomtafuta muhudumu akampata (sijui alimpata wapi hilo sijui). Muhudumu akaja kutufungulia lakini akiwa katika hali ya ulevi.
Baada ya kutufungulia (yule mteja mwingine amekasirika kupita maelezo) ndipo nikamwambia muhudumu nikiwa nimesimama mlangoni kuwa wasilalamike kutopata wateja maana moja ya sababu yawezekana ikawa ni hii aliyotufanyia leo.
Muhudumu akanijibu ".......hata usipokuja tena kwani mteja ni wewe peke yako? Nipishe nifunge mlango......." Huku akinisukumiza na mlango nitoke mlango ukabamiza mabegi niliyokuwa nimeshika mkononi na matairi ya mabegi yakavunja vioo vya mlango huo.
Kilichofuatia akaamuru mlinzi afunge geti tusitoke mpaka hapo polisi watakapokuja. Nikafungiwa ndani ya geti la hoteli kuanzia saa 11 dk 29 alfajiri mpaka polisi walipokuja saa 1 dk 40 asubuhi. Wakaja wakanikamata kwa tuhuma ya kuingia hotelini kwa nia ya kuharibu mali!
Kwa hiyo basi likaniacha na safari ikawa imekufa!
Nikawekwa mahabusu mpaka saa 5 na nusu asubuhi yule jamaa yangu alipotafuta watu wa kuja kunitolea dhamana. Kesi ikaamuliwa nilipe mlango wa hoteli shilingi LAKI SABA ili nisipelekwea mahakamani. Nikawaomba badala ya kulipa pesa mimi nitafute fundi aje atathmini gharama kisha atengeneze nimlipe.
Suala ni kutengeneza mlango....Nilipata upinzani mkali sana polisi kwamba nawafundisha kazi. Nikawaambia sheria za nchi yetu siyo nzuri,mlalamikaji anaaminiwa sana kuliko mshitakiwa.
Wao walikuwa na uthibitisho gani kuwa mimi niliingia hotelini kwa nia ya kuharibu mali? Aliyevunja ni muhudumu siyo mimi!!
Hatimaye ikakubalika nitafute fundi. Nikampata fundi gharama ya kioo ikawa ni shilingi elfu ishirini na ufundi ni shilingi elfu kumi tu. Mlango ukawa umekamilika kutengenezwa saa 7 dk 36 mchana.
Hayo ndiyo yaliyonikuta Tabora. Mlango wenyewe ni huu nilio u atach na muhudumu mwenyewe ni huyo dogo mwenye shati jekundu. Ameniboa sana........!!!!!