Yaliyonikuta Tabora

Yaliyonikuta Tabora

Sample size yangu ni kubwa mkuu huku ni kwetu napajua. Nimeshalala hoteli nyingi sana hapo Tabora lakini huduma ziko chini sana. Tatizo unataka kufananisha tukio hilo na hoteli zote. kwamba nikienda kulala hoteli nyingine muhudumu atanibamiza na mlango uvunjike kama ulivyovunjika wa Goodley Hotel. Sivyo! Ukilala hotel zingine utakumbana na kero ya aina nyingine.....siyo kwamba kero zinakuwa zan namna moja. naomba unielewe mkuu.
Kwa mfano unaingia hotelini unakuta toileti pepa hamna wakati ni hoteli kubwa kabisa napo utasemaje? Na kitu kama toileti pepa kuigundua haipo ni mpaka uende toileti na uwe na shida nayo. Ukiomba toileti pepa utaambia zimeisha na wewe unataka kujisaidi asubuhi uwahi. hiyo siyo kero?

Wewe ni muongo, mimi pia ni mzaliwa na nimekulia Tabora mjini. Usitegemee ulale guest za buku halafu upate matatizo uje ututukane humu. Karibu na stand kuna hoteli nyingi sana tu za maana kama GOLDEN EAGLE na FRANKMAN sijawahi kupata huduma mbaya toka kwao.

Huwezi kusema vibaya mkoa mzima kwasababu ya huyo mlevi na polisi njaa ambao wapo nchi nzima.
 
Sehemu yoyote walopita waarabu sijajua ni kwa nini,nilienda kufacilitate semina Mtwara wahudumu wa hotel hawajali wateja similar kesi Lindi napo ni hivo hivo lakini nilienda Mwanza,Mbeya,Kilimanjaro huduma safi sijui waliwapa dawa gani hawa waarabu.


Hiyo ya Mtwara ilikuwa mwaka gani na ilikuwa ni Hotel gani?,sitegemei kusikia hivyo kwa mtu aliyefikia Naf Blue hotel lakini kama ulijichanganya uswazi basi hapo utaendelea sana kuwalaumu waarabu.
 
Tabora ipo hovyo kabisa hata kiusalama,nilikwenda kikazi kule kuna hotel maarufu nilifikia, sasa nikawa nimetoka nje kuna bar sehemu nikapata moja moto na ili nipate kujua habari za pale, ndipo jamaa wakawa wanaongelea hotel nilipofikia nanukuu 'hii hotel Bwana imezidi kwa ujambazi Juzi wamevamia na kila room wakawa wanaingia na kuiba,muda si mrefu itakosa wateja'. Na mimi ndio nimekaa Pembeni nawasikiliza, asubuhi nikahama ile hotel
 
🏃🏃🏃🏃🏃🏃🏃🏃🏃🏃🏃🏃🏃🏃🏃🏃🏃
 
Wewe ni muongo, mimi pia ni mzaliwa na nimekulia Tabora mjini. Usitegemee ulale guest za buku halafu upate matatizo uje ututukane humu. Karibu na stand kuna hoteli nyingi sana tu za maana kama GOLDEN EAGLE na FRANKMAN sijawahi kupata huduma mbaya toka kwao.

Huwezi kusema vibaya mkoa mzima kwasababu ya huyo mlevi na polisi njaa ambao wapo nchi nzima.

Mkuu kumbuka huduma nzuri ulizopata na tabia za watu wa Tabora....Kwanza wakipata kazi huwa wanajionesha kwa watu wa kwao kwamba wao sasa wana ajira. Hii ndiyo tabia ya Wanyamwezi. Badala ya kutoa huduma huwa wanajionesha wamepata. Kwa kuwa umesema ulipata huduma nzuri Franline na Golden Eagle basi na wewe isiwe ndo sample ya kwamba hoteli zote ni nzuri.
 
Polisi wa Tanzania akili zao kama misukuke vile...

Hii ni kwa sababu imejaa vilaza waliokosa nafasi za kuendelea kimasomo...
Pole Polisi wa TZ ni watafuta hela. Atafanya kitu chochote mpaka ipate hela yako. Kama huna kosa atasingizia umemtukana
 
Hapana mkuu......ni katika hali ya kuwa karibu na eneo la stendi.......Kwa taarifa tu kwa tabora hata hoteli iwe kubwa kiasi gani uelewa wa watu wa Tabora unafanana.
usifikiri kwa kutumia hasira hautaeleweka, mbona hata mimi nilicheleweshwa ubungo mhudumu analiwa chumbani?
 
Mkuu unatuporomoshea matusi yote hayo wanyamwezi kwasababu ya muhuni mmoja tu?

Hututendei haki kabisa mkuu

Wao hawakunitendea haki mbona hausemi? Thamani halisi ya kioo cha mlango na matengenezo ilikuwa ni sh elfu thelathini tu (angalia hiyo picha). Sasa kwa nini wao walitaka nitoe laki saba? Mbona hilo haulioni kuwa si sahihi?
 
Miafrika banah sijui ikoje!..huo ni umaskini au we ni le mbebez mwalimu.

Tatizo mnalala gest za maskini. Nenda lodge ya maana afu lala presidential suite uone kama utapata hayo majangazi!!

Ckila mtu anauwezo wakulala sehemu hizo unazosema Tunatofautiana uwezo....unataka kuniambia anapolala Riz1 nisawa na anapolala mwendesha Bodaboda?
 
Wakuu natumaini hamjambo,

Leo napenda niwaeleze jinsi baadhi ya mikoa yetu ilivyo nyuma kimaendelo na tulikuwa hatujui sababu ya mikoa hiyo kuwa nyuma kimaendeleo. Lakini kwa safari yangu ya Tabora mjini nimegundua ni kutokana na upeo mdogo wa wananchi wa mikoa hiyo iliyo nyuma kimaendelo.

Ni kwamba nilikuwa likizo ya mwaka haki ambayo kila mtumishi anapaswa kupewa. Nilipomaliza likizo yangu usiku wa kuamkia tarehe 15 Mwezi huu nililala kwenye hoteli moja mjini Tabora karibu na stendi kwa ajili ya kujidamkia mabasi yanayokuja Dar Es Salaam ambayo saa ya kuripoti ni saa kumi na moja na nusu alfajiri. Nilifuata taratibu zote za kihoteli na ilipofika saa kumi na moja na robo alfajiri nilikuwa tayari (mimi na mke wangu) kwa safari.

Kufika mapokezi hatukukuta muhudumu yeyote. Nilijaribu kuita kwa sauti kumwita mhudumu atufungulie mlango tuondoke lakini hakuna dalili ya kuitikiwa. Bahati nzuri kuna mteja mwingine naye alikuwa akisafiri alfajiri hiyo naye akaja tukaungana kumtafuta muhudumu bila mafanikio.

Ndipo kwa kutumia maarifa mengine nikajaribu kumwita mlinzi wa nje huko getini aje atusaidie kutufungulia ama kumtafuta muhudumu atufungulie. Lakini tulishindwa kwa sababu getini ni mbali sauti zetu hazikumfikia mlinzi. Ndipo nikapata wazo la kumpigia simu jamaa yangu mmoja aliyepo Tabora mjini aje amgongee mlinzi kisha amfahamishe kuna watu ndani wanahitaji kutoka hotelini lakini hawamwoni muhudumu.

Wazo langu lilifanikiwa maana jamaa akaja akamgongea mlinzi wa hoteli na kumfahamisha ya kuwa muhudumu haonekani na kuna watu wanahitaji kutoka hotelini. Ndipo mlinzi alipomtafuta muhudumu akampata (sijui alimpata wapi hilo sijui). Muhudumu akaja kutufungulia lakini akiwa katika hali ya ulevi.

Baada ya kutufungulia (yule mteja mwingine amekasirika kupita maelezo) ndipo nikamwambia muhudumu nikiwa nimesimama mlangoni kuwa wasilalamike kutopata wateja maana moja ya sababu yawezekana ikawa ni hii aliyotufanyia leo.

Muhudumu akanijibu ".......hata usipokuja tena kwani mteja ni wewe peke yako? Nipishe nifunge mlango......." Huku akinisukumiza na mlango nitoke mlango ukabamiza mabegi niliyokuwa nimeshika mkononi na matairi ya mabegi yakavunja vioo vya mlango huo.

Kilichofuatia akaamuru mlinzi afunge geti tusitoke mpaka hapo polisi watakapokuja. Nikafungiwa ndani ya geti la hoteli kuanzia saa 11 dk 29 alfajiri mpaka polisi walipokuja saa 1 dk 40 asubuhi. Wakaja wakanikamata kwa tuhuma ya kuingia hotelini kwa nia ya kuharibu mali!

Kwa hiyo basi likaniacha na safari ikawa imekufa!

Nikawekwa mahabusu mpaka saa 5 na nusu asubuhi yule jamaa yangu alipotafuta watu wa kuja kunitolea dhamana. Kesi ikaamuliwa nilipe mlango wa hoteli shilingi LAKI SABA ili nisipelekwea mahakamani. Nikawaomba badala ya kulipa pesa mimi nitafute fundi aje atathmini gharama kisha atengeneze nimlipe.

Suala ni kutengeneza mlango....Nilipata upinzani mkali sana polisi kwamba nawafundisha kazi. Nikawaambia sheria za nchi yetu siyo nzuri,mlalamikaji anaaminiwa sana kuliko mshitakiwa.

Wao walikuwa na uthibitisho gani kuwa mimi niliingia hotelini kwa nia ya kuharibu mali? Aliyevunja ni muhudumu siyo mimi!!

Hatimaye ikakubalika nitafute fundi. Nikampata fundi gharama ya kioo ikawa ni shilingi elfu ishirini na ufundi ni shilingi elfu kumi tu. Mlango ukawa umekamilika kutengenezwa saa 7 dk 36 mchana.

Hayo ndiyo yaliyonikuta Tabora. Mlango wenyewe ni huu nilio u atach na muhudumu mwenyewe ni huyo dogo mwenye shati jekundu. Ameniboa sana........!!!!!

View attachment 246879

Uongo huu
 
Yule jamaa mteja mwingine alitangulia kutoka sasa mimi nilipobaki kumweleza aliyotufanyia ndipo yakatokea hayo. Tukabaki wawtatu mimi, mke wangu na jamaa aliyekuja kumgongea mlinzi. Tulishindwa kutok maana geti lilifungwa na jamaa yangu aliyekuja aliingiza gari ndani Tusingeweza kutoka........
Na Tabora unavyopajua saa 11 alfajiri uanzishe varangati si utaambiwa jambazi!!! Polisi walivyokuja kwa suala la kioo tu walitoa pingu wanifunge sembuse ufanye fujo? Mkuu Tabora mimi ni kwetu napajua sana. Uelewa ni ziro! Hata ukiwa mwalimu ukapangiwa Tabora ukiacha tabora boys, Milambo na Tabora girls Tabora ni matatizo....!!!!!!!

Umesahau na Itaga Seminary
 
Hapana mkuu......ni katika hali ya kuwa karibu na eneo la stendi.......Kwa taarifa tu kwa tabora hata hoteli iwe kubwa kiasi gani uelewa wa watu wa Tabora unafanana.
watu wa tabora wanafanana uelewa??unaonekana ww n mjuaji saana,na ulilala hotel ya bei rahis,teheee tabora hakuna maendeleo ww ulienda wap na wap?
 
watu wa tabora wanafanana uelewa??unaonekana ww n mjuaji saana,na ulilala hotel ya bei rahis,teheee tabora hakuna maendeleo ww ulienda wap na wap?

Mkuu achana naye huyo anastress za kulipishwa gharama za mlango.

Kwa sisi tunaoijua Tabora ya miaka hiyo ghorofa ni ofisi ya mkuu wa mkoa tu mpaka sasa hivi, mabadiliko ya kimaendeleo tunayaona.

msamehe huyo malyenge(makengeza) amevurugwa
 
Mkuu achana naye huyo anastress za kulipishwa gharama za mlango.

Kwa sisi tunaoijua Tabora ya miaka hiyo ghorofa ni ofisi ya mkuu wa mkoa tu mpaka sasa hivi, mabadiliko ya kimaendeleo tunayaona.

msamehe huyo malyenge(makengeza) amevurugwa
maendeleo gani Tbr,punguzeni uchawi na uswahili watu tuje kuwekeza
 
Mkuu achana naye huyo anastress za kulipishwa gharama za mlango.

Kwa sisi tunaoijua Tabora ya miaka hiyo ghorofa ni ofisi ya mkuu wa mkoa tu mpaka sasa hivi, mabadiliko ya kimaendeleo tunayaona.

msamehe huyo malyenge(makengeza) amevurugwa

Sasa wewe ndo umeanza dharau....................................Mbona kuna maghorofa kibao tu yamejengwa Tabora? Hivi wewe ni mnyamwezi wa Urambo ama ni mkimbizi wa Urambo? Maana kama Tabora ni kwenu usingeshindwa kuyaona maghorofa yaliyojengwa.....matokeo yake unakumbukumbu ya tabora ya miaka kibao..... Maghorofa yapo mengi siku hizi si kama zamani. Acha kudharau wanyamwezi. Tunazungumzia huduma mbovu Tabora na si kubeza maghorofa. Usitoke nje ya mada........
 
Customer service mbovu kabisa huyo mhudumu alitaakiwa ataifishwe kazi hapo hapo!Na hao mapolisi kiboko doh walitaka wakudhulumu mara 20 ya pesa ulolipa kwaajili ya mlango ambao umeharibika kwa kosa la mhudumu!
 
Mkuu OKW BOBAN SUNZU umewatajia sababu za kutoendelea Tabora! Hongera sana mkuu. Kuna watu walikuwa wanashindwa kupata corolation ya huduma mbovu na maendeleo. Umeshawatajia mkuu. Mojawapo ni uchawi na Uswahili......
Sasa kitendo walichonifanya Goodley Hotel ni uswahili.......!!!!!!
Mkuu wewe ni genius.......!!!!!
 
Last edited by a moderator:
Sasa wewe ndo umeanza dharau....................................Mbona kuna maghorofa kibao tu yamejengwa Tabora? Hivi wewe ni mnyamwezi wa Urambo ama ni mkimbizi wa Urambo? Maana kama Tabora ni kwenu usingeshindwa kuyaona maghorofa yaliyojengwa.....matokeo yake unakumbukumbu ya tabora ya miaka kibao..... Maghorofa yapo mengi siku hizi si kama zamani. Acha kudharau wanyamwezi. Tunazungumzia huduma mbovu Tabora na si kubeza maghorofa. Usitoke nje ya mada........

Soma vizuri uielewe hiyo statement ya kuhusu maghorofa usiwe na haraka kucomment
 
Back
Top Bottom