Yaliyonikuta Tabora

Yaliyonikuta Tabora

Mkuu achana naye huyo anastress za kulipishwa gharama za mlango.

Kwa sisi tunaoijua Tabora ya miaka hiyo ghorofa ni ofisi ya mkuu wa mkoa tu mpaka sasa hivi, mabadiliko ya kimaendeleo tunayaona.

msamehe huyo malyenge(makengeza) amevurugwa

Si ndo hivyo ulivosema? Ina maana mpaka sasa ghorofa ni la mkuu wa mkoa tu. Au mpaka tulete mtu wa PhD ya interpretation?
 
Mkuu upo sawa.

Kwa sisi tunaoishi nje, ukifika tu Dar, unataka kulia maana kila kitu kinafanywa tofauti.

Sasa ukifika Tabora wala hushangai tena maana ulishabwaga moyo Dar.

Ila nakubaliana kuwa kutukana mkoa mzima kwa sababu ya Mjinga fulani, ni makosa.

Hii hotel ambayo mhudumu amelewa, mlinzi hajali na mwenye hotel hana habari kwa nini mhudumu hayupo ni kasheshe.

Sasa moto ukiokea ndani na milango imefungwa itakuwaje? Mwisho unasema kazi ya Mungu......

Ukilala hotel na asubuhi sana unaondoka, basi uliza kama usiku wanafunga au utaweza kutoka.....



Wewe ni muongo, mimi pia ni mzaliwa na nimekulia Tabora mjini. Usitegemee ulale guest za buku halafu upate matatizo uje ututukane humu. Karibu na stand kuna hoteli nyingi sana tu za maana kama GOLDEN EAGLE na FRANKMAN sijawahi kupata huduma mbaya toka kwao.

Huwezi kusema vibaya mkoa mzima kwasababu ya huyo mlevi na polisi njaa ambao wapo nchi nzima.
 
Customer service mbovu kabisa huyo mhudumu alitaakiwa ataifishwe kazi hapo hapo!Na hao mapolisi kiboko doh walitaka wakudhulumu mara 20 ya pesa ulolipa kwaajili ya mlango ambao umeharibika kwa kosa la mhudumu!

Ni kweli mkuu. Polisi walisema hakuna ushahidi ninaoweza kuthitisha kuwa muhudumu alivunja kioo cha mlango mwenyewe. na wao nikawauliza hakuna ushahidi anaoweza kuthibitisha kuwa mimi nilivunja kioo cha mlango. Wakasema uthibitisho upo kwa sababu yeye ndo amekwenda polisi kushitaki.
Ni hoja ambayo nikaamua kuipuuza maana niliiona kuwa ni ya kipumbavu.
 
Sipati picha ungezuka moto humo ndani ingekuwaje maana mumefungiwa kama mbuzi zizini na mhudumu hayupo. Mngeungua hadi majivu. Asante kwa taarifa ili tukifika tabora tuwe makini.
 
Ni kweli mkuu. Polisi walisema hakuna ushahidi ninaoweza kuthitisha kuwa muhudumu alivunja kioo cha mlango mwenyewe. na wao nikawauliza hakuna ushahidi anaoweza kuthibitisha kuwa mimi nilivunja kioo cha mlango. Wakasema uthibitisho upo kwa sababu yeye ndo amekwenda polisi kushitaki.
Ni hoja ambayo nikaamua kuipuuza maana niliiona kuwa ni ya kipumbavu.

Ila na wewe ulizidi udhaifu tena mbele ya mkeo yaani kijana mdogo wa gest anakubambikia kesi pamoja na mgambo wake unafungiwa mpaka polisi wanakuja ivi kweli ulikosa cha kufanya au vipi? Siku nyingine piga vibao wote wawili mi kesi kama hizo ndo nazipenda vibaya sana niliwah kudhurumiwa na mhudumu mmoja kama elfu 20 ivi alafu kaniletea janja ya nyani nikaona ngoja nilete polisi wanisaidie kuja polisi demu anasema alinipa k so tumemalizana na polisi wakakubaliana nae nilichukia kilichotokea pale ni fundisho kwa yule demu kufanyia uhuni vijana tusiokua na kazi nilipiga mbele ya polisi na nikabeba simu yake polisi nikawapa line tu.
 
Ila na wewe ulizidi udhaifu tena mbele ya mkeo yaani kijana mdogo wa gest anakubambikia kesi pamoja na mgambo wake unafungiwa mpaka polisi wanakuja ivi kweli ulikosa cha kufanya au vipi? Siku nyingine piga vibao wote wawili mi kesi kama hizo ndo nazipenda vibaya sana niliwah kudhurumiwa na mhudumu mmoja kama elfu 20 ivi alafu kaniletea janja ya nyani nikaona ngoja nilete polisi wanisaidie kuja polisi demu anasema alinipa k so tumemalizana na polisi wakakubaliana nae nilichukia kilichotokea pale ni fundisho kwa yule demu kufanyia uhuni vijana tusiokua na kazi nilipiga mbele ya polisi na nikabeba simu yake polisi nikawapa line tu.

Unajua mkuu si suala la udhaifu......ni suala la muda na rasilimali. Kijana mwenyewe hata mkononi hajai sema ukifanya jambo lingine lolote Tabora utabambikiziwa kesi ya ujambazi. Na ikizingatia mlango umevunjwa si ndio wangepata ushahidi kamili mkuu? Kama kumshighulika huyo kijana ni siku nyingine lakini si katika mazingira yale. Nakubali yawezekana kuna udhaifu lakini sitakuwa dhaifu siku zote.
 
pole sana ndugu!!
wahudumu mikundu sample ya huyo dogo wapo sana mahotelini,magestini,mawizarani,maofisini,mabasini,madukani,n.k
 
Back
Top Bottom