Yaliyonikuta CAS ya TCU,Hisia zangu na Ushauri.

Yaliyonikuta CAS ya TCU,Hisia zangu na Ushauri.

Naisujaki Lekangai

JF-Expert Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
1,340
Reaction score
1,378
Wanajukwaa la elimu hamjambo?
Naandika haya yaliyonikuta kwenye mfumo wa cas ya tcu 2016/17 na sijui yaliyotokea huko nyuma ie 2015/2016 etc.
Yaliyonikuta.
Shemeji yangu alimaliza form4 2013 na form6 2016,akaniomba tuingie cas ili kuomba kozi ya degree.Tukaingia huko.

Tukaingiza index number ya form 4 pamoja na nywila tuliyounda.

Tulipobofya log in, jina lililotoka liliminywa herufi 4 za mwisho kwenye jina la tatu (surname) na option ya kusahihisha jina haikufanya kazi.

Hisia zangu.
Ninahisi kwamba programming ya cas kwenye field ya jina inaruhusu herufi +spacing isiyozidi character 29.Jina la shemeji +baba+surname + spacing ni character 33.

Bahati, shemeji kachaguliwa kusoma degree ila jina lake la ukoo (surname) limeminywa herufi nne ilihali kwenye vyeti vyake jina hilo liko full.Sasa je, chuoni watampokea kwa jina hilo la tofauti na vyeti vyake?

Ushauri kwa tcu
Kama hisia zangu za programming ni sahihi, ama tcu warekebishe haraka character zinazoruhusiwa kwenye field ya jina+spacing ziwe zaidi ya 30 kwa sababu majina ya baadhi ya jamii zetu hapa tanzania ni marefu sana.
au tcu wawasiliane na necta ili form4 wanapojiandikisha kwa mitihani ya taifa,majina yatakayoandikishwa yasiwe na herufi +spacing inayozidi character 29.
 
Hiyo haina tatizo mbona kozi mfumo na vyeti ni vitu viwili tofauti na ndiyo mana kila mtu anatumia namba badala ya jina ukiingiza namba jina lifajitokeza kama lilivyo kwenye cheti hivyo usiwe na waswas
 
kikubwa ni namba ya cheti mkuu.majina mnaweza mkawa mnafanana wengi tu.
 
vyeti ndo kila kitu chuo atapokelewa asijali
chuo chako kimepokea toka tcu jina la Eshinalavio Oshondumii Nduasi halafu anakuja mwanachuo mwenye cheti chenye jina Eshinalavio Oshondumii Nduasinde utampokea kwa roho moja bila kuuliza chochote siyo?
 
Hiyo haina tatizo mbona kozi mfumo na vyeti ni vitu viwili tofauti na ndiyo mana kila mtu anatumia namba badala ya jina ukiingiza namba jina lifajitokeza kama lilivyo kwenye cheti hivyo usiwe na waswas
Thread umeisoma na kuielewa lakini?
 
Heko mdau. Kumbe mambo ya programming unayamanya sana eh? Hilo tatizo la jina kwenye cheti kutofautiana na jina la tcu kwa herufi nne litasuluhishwa tu usiwe na wasi.
 
Back
Top Bottom