Ng'wamapalala
JF-Expert Member
- Jun 9, 2011
- 6,811
- 6,506
Ni ukweli kabisa katika dunia hii kila tatizo huwa lina solution yake.Unauliza alienda kumkinga Mbowe akiwa kama nani!, OK, akiwa kama mbunge wa CHADEMA, na sio mbunge wa CHADEMA tu bali kila mbunge wa bunge la JMT anawajibu wa kuhakikisha kanuni zinafuatwa.
Ina maana unataka kuhalalisha kuwa alichofanyiwa ni sawa tu kisa kamkinga Mbowe?, Hata hivyo naomba nikusahihishe, hakuwa peke yake kwenye kumkinga Mbowe, ni karibu wabunge wote wa CDM walimzinga Mbowe asitolewe, picha na clips zipo humuhumu zitafute ujiridhishe.
Lakini kwa nini yeye zaidi ndio aliandamwa?, wapo wanaojaribu kuhusianisha tukio hili na tukio la Sugu kudaiwa kumtukana Pinda japo mahakama ilitupilia mbali, wanajenga hoja kwamba uongozi wa bunge ulikuwa na hasira nae.
Kama huo ndiyo msingi wako wa hoja. Unataka kuniambia kama kanuni hazifuatwi ndani ya bunge alichofanya Mh. Mbilinyi ndiyo solution iliyopo katika kanuni hizo?.
Sitaki kumjadili Naibu Spika na matamshi yake kwa sababu hajadiriki kwa maana kuwa hakuzitendea haki kanuni za bunge na kikubwa zaidi, hakutumia hata tone dogo la hekima na busara.