Pascal Mayalla
Platinum Member
- Sep 22, 2008
- 50,655
- 113,881
Mkuu Molemo , japo kwa sasa mimi ni kada wa Chama cha Mapinduzi, CCM, ni muumini wa ukweli, uwazi na kufanya siasa safi, za kupingana bila kutukanana, sio muumini wa siasa za majitaka.Mkuu Fahamu TV zote zimekatazwa kurusha Live mikutano ya Chadema.
Tulikuwa tunarusha kupitia Chadema Media You Tube Platform yetu wiki iliyopita kijana wetu aliyekuwa anafanya kazi hiyo kakamatwa na kufunguliwa mashtaka na TCRA kwanini anarusha mikutano ya Chadema
Kama ni kweli TV zote zimekatazwa kurusha live mikutano ya Chadema, nawapa pole!, ila nakuomba kuwa mkweli, ni nani aliyezikataza TV zote zisirushe live mikutano ya Chadema?. Jee mnao ushahidi wowote wa hili?. Kama ni kweli na ushahidi mnao, what did you do, wakati, sheria zipo, taratibu za kufuatwa zipo na mnazijua, kanuni za TCRA za utangazaji uchaguzi mkuu ziko wazi, mmefanya nini?.
Hilo la kijana wenu kukamatwa, hapa Mkuu mwenzangu ni kuwa mkweli tuu, hakukamatwa kwasababu anarusha live mkutano wa Chadema kupitia Chadema Media You Tube Platform yenu, naomba soma vizuri charge sheet!. Kosa lake ni kurusha maudhui mtandaoni kupitia online TV bila kusajiliwa na TCRA!.
Kiukweli kabisa mkubali mkatae, katika moja ya maeneo ambayo Chadema mna matatizo ni eneo la mass mobilization na doing the right thing!.
Niliwashauri siku nyingi toka ile 2015!. Kurusha kwenye YouTube ni bure, TCRA imeweka sheria ya kujisajili na kulipia just TZS 1,000,000 kwa miaka 2, juzi juzi wamepunguza ada ya usajili hadi just TZS 500,000 tuu!. Hivi kweli Chadema ni watu wa kurusha online TV bila kusajiliwa na wakati sheria, taratibu na kanuni mbazijua!. You are not serious!.
Sasa vitu vidogo vidogo kama hivi, vinawafanya watu wenye integrity kujiuliza, maswali kama haya
Je, CHADEMA inaweza kushinda 2020? Is it serious, credible & mature enough opposition?
Kuwa mkweli Mkuu mwenzangu Molemo, kweli nyie Chadema are you really serious?, sasa kama vitu vidogo vidogo tuu hivi kama kujisajili TCRA kupata leseni ya kurusha maudhui mtandaoni mnashindwa!, Ikulu mtaiweza?.
Hili la media, nimewashauri sana tangu yule "jamaa yangu" alipojiunga kwenu
Elections 2015 - Mabadiliko Chanya ya Ujio wa Lowassa: CHADEMA Kuhama Ufipa!, Kuwa Makao Yake, Kituo cha TV na Redio!
Nilisema
Wanabodi,
Ukipiga hesabu ya jumla ya ruzuku yote ambayo Chadema imekuwa ikipokea, na kulinganisha ruzuku hiyo imefanyia nini, utakubaliana na mimi, kuwa fedha hiyo, ingetosha kabisa kujenga jengo jingine kwenye eneo la kutosha. Hali hii imetokana na upangaji mbovu wa vipaumbele vyake, hali iliyopelekea matumizi mabovu ya ruzuku, kama yalivyofafanuliwa kwenye ripoti ya CAG.
Mabadiliko hayo chanya sio tuu kwa Chadema kumiliki jengo lake lenyewe, pia Chadema itamiliki kituo chake cha Redio na Televisheni pamoja na magazeti yake yenyewe, kwa sababu Lawassa hapo alipo tayari ni mmiliki by proxy wa familia kubwa ya media, yenye vituo vya Redio, TV na magazeti lukuki!, hivyo sasa pia vitatumiwa kuisupport Chadema kwa kuanzia tuu, wakati mchakato wa umiliki rasmi wa vyombo vyake yenyewe ukiendelea!.
Paskali
Wakati tukijiandaa kwa uchaguzi huu, kuna kitu niliuliza humu,
Uchaguzi wa 2020, Kukumbuka shuka kumekucha, is it too little too late kwa CHADEMA or better late than never?
Better late than never, mlipieni kijana wenu ile standard fine ya TZS 5.M, sajilini TCRA mpige kazi.
P