Uchaguzi 2020 Yaliyojiri Katika Mapokezi na Mkutano Mkubwa wa hadhara wa Tundu Lissu Mjini Bukoba

View attachment 1576775
Mgombea Urais kupitia Chadema Tundu Lissu leo anatarajiwa kuingia kwa kishindo kikubwa mjini Bukoba.

Mji wa Bukoba ambao ni ngome Kuu ya Chadema unatarajiwa kuzizima Leo wakati shujaa huyo atakapokanyaga viunga vya mji huo.

Mgombea Ubunge wa Bukoba Mjini mwenye ushawishi mkubwa Chief Kalumuna amewaalika wananchi wote wa Bukoba kumlaki na kumsindikiza kwa maandamano makubwa mgombea huyo wa Urais atakapowasili Hadi katika viwanja vya Gymkhana.

Wachunguzi wa siasa za Bukoba wanasema huenda Leo mji wa Bukoba ukavunja Rekodi ya Mapokezi iliyowekwa na miji ya Tunduma, Mbeya na Mwanza.

Mpaka Sasa kila dalili zinaonyesha mgombea Urais kupitia Chadema Tundu Lissu ana Uhakika wa kushinda kwa zaidi ya asilimia 60%

Kabla ya kuingia Bukoba Mjini Lissu atahutubia mikutano katika miji ya Karagwe na Misenyi
Tunafuatilia kwa karibu sana mkuu , Naona Molemo Media iko kazini , safi sana kamanda
 
Tunahitaji mabadiliko sisi sera za wana ccm zimesha chosha watu.watu wanatawala kwa kukariri
Kweli kabisa, maana tumechoka watoto wetu kupata elimu bila malipo, tumechoka kutembea kwenye barabara za lami, tumechoka kukarabatiwa MV Bukoba na kutengenezwa meli mpya, tumechoka Serikali ya awamu ya tano ku-control mfumuko wa bei, tumechoka umeme kusambaziwa umeme vijijini, yaani tumechoka watanzania
 
Lissu anakamilisha ratiba huko kanda ya ziwa hana chake, mdomo wake umemponza. Anachukia meli,treni,daraja la busisi nk. kwa kifupi ngoja akatembee na uwepo wake unawaponza wagombea ubunge na udiwani kupitia chadema.
Hahah...bahati nzuri ni kwamba unayesema haya ni zombie la lumumba
 
inaelekea somo analowapa Tundu Lissu haliwakolei.

nitakukumbusha.

1. meli, treni, madaraja, ni wajibu wa kila serekali kwani kodi za wananchi ndizo zinazotumika. pesa hazitoki kwa rais wala chama tawala

2. hata mkoloni alijenga vyote hivi lakini bado Mwalimu JKN (RIP mzee wetu) alipigania uhuru bila kujali misukosuko ya wakoloni

3. vitu hivyo kutekelezwa na serekali ni kama ATM (serekali) inavyotumika kuchukua pesa zako (kodi yako) benki

4. kutekeleza vitu hivyo pasipokuwa na uhuru na haki katika jamii ni sawa na kujenga nyumba bila msingi juu ya mchanga, nyumba hii itabomoka kabla ya hata kupaua

5. Tundu Lissu anasema anataka kujenga miundombinu na kuinua uchumi katikati ya uhuru na haki. hii ni sawa na kujenga nyumba juu ya msingi imara wa zege, nyumba hii itadumu milele!
Thank you sir!
😅
👊 ✌️✌️✌️💥
 
Ndg Mayalla, nyie wa vyombo vya habari mnaogopa kufanya live coverage ya mikutano ya Lissu kwa sababu mnazozijua wenyewe. Hata magazeti, almost yote yanakuwa na title moja tu ya Magufuli, na kapicha KADOGOOOOO ka vyama vya upinzani. Hatujawahi kushuhudia uoga wa wanahabari kwa tawala za huko nyuma kama huu tunaoushuhudia sasa. Kweli tunajua mna watoto wa kulea, mnaogopa kufungiwa, lakini mmezidi mno.

Mayalla maana yake njaa haaaaa tangu tupoambiwa maana ya jina lake sisumbuki tena.
 
Hapa Missenyi Mh.Tundu Lisu amesubuliwa watu wamekesha uwanja wa mashujaa chakaza...bendera za chama zinapepea Kila upande
Niyeye2020
Huko ndo kahawa zenu mlizuiwa kuuza kwa bei nzuri, mkalazimishwa kukopwa kwa bei ya chini?.......msifanye makosa tena mmeona ukatili wa magufuli, apigwe chini hayupo na sisi kwenye maendeleo yetu. Ana ajenda zake ambazo si rafiki kwa ustawi wetu!. Piga chini CCM!.
 
Mkuu Molemo asante kwa taarifa hiyo, tunamtakia kila la heri Rais wetu huyu ajaye awe na afya njema, naomba akisahau kuwapa pole wananchi wa Bukoba kwa natural disaster iliyowakumba miaka iliyopita umkumbushe asisahau pia kile walichofanya wale watani wetu walivyopiga kibindoni rambirambi za waliofikwa na maafa yale...

Mkubwa punguza sauti aisee
 
Kama tunavyotawaliwa rais wa ajabu haijawahi tokea

Huyu huyu ndio Aliyekuwa anamkandia Nyerere, Mwinyi,Mkapa na Kikwete, Leo hii ana wasifia, na kumponda Magufuli wakati Magufuli anayafanya yale waliokuwa wanayapigia Debe .
Kuhusu Chakula sijasikia mtanzania aliyekufa u kwa ajili ya njaa.
Kuhusu kuagiza tani 90,000 inategemea upungufu ni kiasi gani, na hata huo uagizaji upungufu mbona haukuleta shida yeyote.
Anti ongea kama mtu mzima.
 
Bukoba wamejipanga wanataka kuvunja rekodi
Ni kweli Tunduma na Mbeya town tulitisha...

Ila guys, mlikiona kilichofanywa na watu wa Kyerwa Jana? Hili naona linapewa uzito kidogo, lakini yale mapokezi ya pale kati binafsi yaani- inspire sanaa, kwanza kulikuwa kama kijijini hivi, uwanja wenyewe ulikuwa katikati ya msitu hukoo... barabara ya kuufikia ule uwanja ni full mivumbi... bila shaka angekuwa mwaflan afike pale na kile "kiberiti" chake angelazwa wiki nzima akitibiaa..!!

Jamaa walitisha sana...vibe kama lote, mzuka kama katelemka nani sijui... Yaani daah.. jana, mpaka nilimwogopa Lissu.!!

BACK TANGANYIKA
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom