YEHODAYA
JF-Expert Member
- Aug 9, 2015
- 36,908
- 51,904
Tayari msafara umeshajipanga kuondoka Ikulu Chamwino kuelekea bungeni kuagwa kisha utapelekwa uwanja wa Jamhuri
=========
DODOMA: WABUNGE WATOA HESHIMA ZA MWISHO KWA DKT. MAGUFULI
Spika wa Bunge Job Ndugai akiwaongoza Wabunge na Viongozi wengine mbalimbali kwenye shughuli za kuuaga mwili wa Hayati Magufuli
Wabunge wa Bunge la Tanzania wametoa heshima zao za mwisho kwa Hayati Dkt. John Magufuli aliyekuwa Rais wa Awamu ya Tano aliyefariki dunia Machi 17, 2021
Wabunge wameuaga mwili wa Dkt. Magufuli katika Viwanja vya Bunge Jijini Dodoma na baada ya zoezi hilo kukamilika, mwili huo utapelekwa Uwanja wa Jamhuri kwa ajili ya shughuli ya kitaifa ya kutoa heshima za mwisho ambao itahudhuriwa na Viongozi mbalimbali wa Kimataifa
NAIBU SPIKA: WENGI WAMEONA MEMA YA DKT. MAGUFULI. WATU WENGINE KUTOONA WEMA NI KAWAIDA
Mwili wa Hayati Dkt. John Magufuli aliyekuwa Rais wa Tanzania umewasili Viwanja vya Bunge Dodoma kisha atapelekwa Uwanja wa Jamhuri kwa shughuli ya kumuaga Kitaifa
Akizungumza katika Viwanja vya Bunge, Naibu Spika wa Bunge la Tanzania, Dkt. Tulia Ackson ameeleza walio wengi wameona mema aliyofanya Dkt. Magufuli, akisema watu wengine kutoona wema ni jambo la kawaida
RATIBA YA KUMUAGA DKT. MAGUFULI DODOMA YABADILISHWA
Kutokana na wingi wa watu waliojitokeza Uwanja wa Jamhuri kumuaga Hayati Dkt. John Magufuli, ratiba imebadilishwa ambapo imeelezwa mwili utaagwa na watu wachache uwanjani
Imeelezwa mabadiliko hayo yamefanyika ili kutoa nafasi kwa wananchi kuaga kwenye mitaa ili watu wote waweze kutoa heshima zao za mwisho
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Dkt. Binilith Mahenge amesema baada ya watu wachache kuaga, mwili wa Dkt. Magufuli utatolewa Uwanjani na kupitishwa round about ya Jamhuri na kisha katika Barabara ya Iringa na kisha ya Polisi
Ametaja Barabara nyingine ambazo mwili utapita kuwa ni Jamatini, Bunge, Morena, Emaus kuzungushia Barabara ya Waziri Mkuu hadi African Dreams na kutokea Barabara ya Arusha hadi Uwanja wa Ndege.
WAZIRI MKUU: NAMNA NZURI YA KUMUENZI DKT. MAGUFULI NI KUUISHI UTUMISHI WAKE
Waziri Mkuu wa Tanzania, Kassim Majaliwa, amesema namna nzuri ya kumuenzi Hayati Dkt. John Magufuli ni kwa Watu kuuishi utumishi wake uliojaa ujasiri, maono na mapenzi makubwa kwa Nchi
Akizungumza katika Uwanja wa Jamhuri amesema, "Wengi tulitamani aendelee kuwa nasi kimwili, hata hivyo kifo ni suala lisiloepukika"
Ameungana na kauli iliyotolewa na Rais Samia Suluhu Hassan kuhusu Watanzania kuendelea kushirikiana na kuzidisha umoja na mshikamano.
-
Ameongeza pia Hayati Magufuli aliifanya Afrika iheshimike tena na pia ametimiza ndoto za waasisi wa nchi barani Afrika.
RAIS KENYATTA: DKT. MAGUFULI AMEONESHA WAAFRIKA TUNA UWEZO WA KUSIMAMIA UCHUMI WETU
Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta amesema katika miaka michache, Dkt. John Magufuli aliyekuwa Rais wa Tanzania ameonesha kuwa Waafrika wana uwezo wa kujitoa katika utegemezi wa watu na vitu vya nje
Amesema, "Kwa muda mfupi tumeona kazi ya barabara, ujenzi wa Uwanja wa Ndege na mambo mengine mengi ambayo yatakuwa na manufaa kwa Watanzania na wana Afrika Mashariki"
Rais Kenyatta amemuelezea Hayati Dkt. Magufuli kama Rafiki wa karibu ambaye walikuwa wanaongea mara kwa mara. Amesema kifo chake ni pigo kwasababu alikuwa mtu wa heshima
Ameongeza, "Nawahakikishia tutaendelea kufanya kazi pamoja, tutaendelea kushirikiana na kuhakikisha tunaleta pamoja Jumuiya ya Afrika Mashariki"
RAIS RAMAPHOSA WA AFRIKA KUSINI AMSHUKURU DKT. MAGUFULI KWA MAMBO MATATU
Katika hotuba yake Uwanja wa Jamhuri Dodoma, Rais Cyril Ramaphosa amesema Hayati Dkt. Magufuli alisimama kama shujaa dhidi ya Rushwa na ubadhirifu, akimuelezea kama Kiongozi aliyepinga vitendo hivyo akiamini Viongozi wanapaswa kutumikia wananchi wao
Amemshukuru Dkt. Magufuli kwa kuelekeza nguvu katika maendeleo ya Kiuchumi wa Taifa la Tanzania, Ukanda na Bara la Afrika kwa ujumla
Vilevile, Rais Ramaphosa amemshukuru Hayati Dkt. Magufuli kwa kuwa Mwana wa Afrika aliyeona umuhimu wa tamaduni kukumbukwa na kufundishwa, akisema alikuwa Kiongozi aliyetaka watu kujivunia Lugha za Kiafrika
Amesema Tanzania ilipata bahati kuwa na Kiongozi kama Hayati Dkt. John Magufuli
RAIS SAMIA: MATOKEO NDIO JIBU PEKEE ALILOPENDA KUSIKIA DKT. MAGUFULI. SIO VISINGIZIO NA LAWAMA
Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amesema Hayati Rais Magufuli alipenda kusikia matokeo kutoka kwao na wala sio visingizio na lawama
Amesema, "Alitukumbusha kuwa amejitolea maisha yake kuwa sadaka kwa Watanzania hivyo hakuwa na budi kufanya kazi usiku na mchana kuwaletea Maendeleo. Sote tulihofia sana iwapo alipata muda wa kutosha wa kupumzika"
Amesema katika Uongozi wa Dkt. Magufuli, wamejifunza mengi akisisitiza "Tupo vizuri, tumeiva sawasawa"
MWILI WA DKT. MAGUFULI WAZUNGUSHWA MARA TANO UWANJA WA JAMHURI
Mwili wa Hayati Dkt. John Magufuli umezungushwa mara katika Uwanja wa Jamhuri ili kutoa fursa kwa wananchi kutoa heshima zao za mwisho
Hilo limefanyika baada ya Viongozi, Wakuu wa Nchi mbalimbali pamoja na Familia ya Dkt. John Magufuli kutoa heshima zao za mwisho katika Uwanja huo ambapo shughuli ya Kitaifa imefanyika
Baada ya kuzungushwa katika uwanja huo, mwili wa Dkt. Magufuli utazungushwa kupita maeneo kadhaa ili wakazi wa Dodoma waweze kumuaga Kiongozi huyo
=========
DODOMA: WABUNGE WATOA HESHIMA ZA MWISHO KWA DKT. MAGUFULI
Wabunge wa Bunge la Tanzania wametoa heshima zao za mwisho kwa Hayati Dkt. John Magufuli aliyekuwa Rais wa Awamu ya Tano aliyefariki dunia Machi 17, 2021
Wabunge wameuaga mwili wa Dkt. Magufuli katika Viwanja vya Bunge Jijini Dodoma na baada ya zoezi hilo kukamilika, mwili huo utapelekwa Uwanja wa Jamhuri kwa ajili ya shughuli ya kitaifa ya kutoa heshima za mwisho ambao itahudhuriwa na Viongozi mbalimbali wa Kimataifa
NAIBU SPIKA: WENGI WAMEONA MEMA YA DKT. MAGUFULI. WATU WENGINE KUTOONA WEMA NI KAWAIDA
Mwili wa Hayati Dkt. John Magufuli aliyekuwa Rais wa Tanzania umewasili Viwanja vya Bunge Dodoma kisha atapelekwa Uwanja wa Jamhuri kwa shughuli ya kumuaga Kitaifa
Akizungumza katika Viwanja vya Bunge, Naibu Spika wa Bunge la Tanzania, Dkt. Tulia Ackson ameeleza walio wengi wameona mema aliyofanya Dkt. Magufuli, akisema watu wengine kutoona wema ni jambo la kawaida
RATIBA YA KUMUAGA DKT. MAGUFULI DODOMA YABADILISHWA
Kutokana na wingi wa watu waliojitokeza Uwanja wa Jamhuri kumuaga Hayati Dkt. John Magufuli, ratiba imebadilishwa ambapo imeelezwa mwili utaagwa na watu wachache uwanjani
Imeelezwa mabadiliko hayo yamefanyika ili kutoa nafasi kwa wananchi kuaga kwenye mitaa ili watu wote waweze kutoa heshima zao za mwisho
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Dkt. Binilith Mahenge amesema baada ya watu wachache kuaga, mwili wa Dkt. Magufuli utatolewa Uwanjani na kupitishwa round about ya Jamhuri na kisha katika Barabara ya Iringa na kisha ya Polisi
Ametaja Barabara nyingine ambazo mwili utapita kuwa ni Jamatini, Bunge, Morena, Emaus kuzungushia Barabara ya Waziri Mkuu hadi African Dreams na kutokea Barabara ya Arusha hadi Uwanja wa Ndege.
WAZIRI MKUU: NAMNA NZURI YA KUMUENZI DKT. MAGUFULI NI KUUISHI UTUMISHI WAKE
Waziri Mkuu wa Tanzania, Kassim Majaliwa, amesema namna nzuri ya kumuenzi Hayati Dkt. John Magufuli ni kwa Watu kuuishi utumishi wake uliojaa ujasiri, maono na mapenzi makubwa kwa Nchi
Akizungumza katika Uwanja wa Jamhuri amesema, "Wengi tulitamani aendelee kuwa nasi kimwili, hata hivyo kifo ni suala lisiloepukika"
Ameungana na kauli iliyotolewa na Rais Samia Suluhu Hassan kuhusu Watanzania kuendelea kushirikiana na kuzidisha umoja na mshikamano.
-
Umoja wa Afrika: Magufuli alikuwa mkombozi wa Afrika katika Utawala na Uchumi.
Rais wa DR Congo ambaye ni Mwenyekiti wa Umoja wa nchi za Afrika ameyasema haya alipokuwa akitoa salamu za rambirambi leo Dodoma.Ameongeza pia Hayati Magufuli aliifanya Afrika iheshimike tena na pia ametimiza ndoto za waasisi wa nchi barani Afrika.
RAIS KENYATTA: DKT. MAGUFULI AMEONESHA WAAFRIKA TUNA UWEZO WA KUSIMAMIA UCHUMI WETU
Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta amesema katika miaka michache, Dkt. John Magufuli aliyekuwa Rais wa Tanzania ameonesha kuwa Waafrika wana uwezo wa kujitoa katika utegemezi wa watu na vitu vya nje
Amesema, "Kwa muda mfupi tumeona kazi ya barabara, ujenzi wa Uwanja wa Ndege na mambo mengine mengi ambayo yatakuwa na manufaa kwa Watanzania na wana Afrika Mashariki"
Rais Kenyatta amemuelezea Hayati Dkt. Magufuli kama Rafiki wa karibu ambaye walikuwa wanaongea mara kwa mara. Amesema kifo chake ni pigo kwasababu alikuwa mtu wa heshima
Ameongeza, "Nawahakikishia tutaendelea kufanya kazi pamoja, tutaendelea kushirikiana na kuhakikisha tunaleta pamoja Jumuiya ya Afrika Mashariki"
RAIS RAMAPHOSA WA AFRIKA KUSINI AMSHUKURU DKT. MAGUFULI KWA MAMBO MATATU
Katika hotuba yake Uwanja wa Jamhuri Dodoma, Rais Cyril Ramaphosa amesema Hayati Dkt. Magufuli alisimama kama shujaa dhidi ya Rushwa na ubadhirifu, akimuelezea kama Kiongozi aliyepinga vitendo hivyo akiamini Viongozi wanapaswa kutumikia wananchi wao
Amemshukuru Dkt. Magufuli kwa kuelekeza nguvu katika maendeleo ya Kiuchumi wa Taifa la Tanzania, Ukanda na Bara la Afrika kwa ujumla
Vilevile, Rais Ramaphosa amemshukuru Hayati Dkt. Magufuli kwa kuwa Mwana wa Afrika aliyeona umuhimu wa tamaduni kukumbukwa na kufundishwa, akisema alikuwa Kiongozi aliyetaka watu kujivunia Lugha za Kiafrika
Amesema Tanzania ilipata bahati kuwa na Kiongozi kama Hayati Dkt. John Magufuli
RAIS SAMIA: MATOKEO NDIO JIBU PEKEE ALILOPENDA KUSIKIA DKT. MAGUFULI. SIO VISINGIZIO NA LAWAMA
Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amesema Hayati Rais Magufuli alipenda kusikia matokeo kutoka kwao na wala sio visingizio na lawama
Amesema, "Alitukumbusha kuwa amejitolea maisha yake kuwa sadaka kwa Watanzania hivyo hakuwa na budi kufanya kazi usiku na mchana kuwaletea Maendeleo. Sote tulihofia sana iwapo alipata muda wa kutosha wa kupumzika"
Amesema katika Uongozi wa Dkt. Magufuli, wamejifunza mengi akisisitiza "Tupo vizuri, tumeiva sawasawa"
MWILI WA DKT. MAGUFULI WAZUNGUSHWA MARA TANO UWANJA WA JAMHURI
Mwili wa Hayati Dkt. John Magufuli umezungushwa mara katika Uwanja wa Jamhuri ili kutoa fursa kwa wananchi kutoa heshima zao za mwisho
Hilo limefanyika baada ya Viongozi, Wakuu wa Nchi mbalimbali pamoja na Familia ya Dkt. John Magufuli kutoa heshima zao za mwisho katika Uwanja huo ambapo shughuli ya Kitaifa imefanyika
Baada ya kuzungushwa katika uwanja huo, mwili wa Dkt. Magufuli utazungushwa kupita maeneo kadhaa ili wakazi wa Dodoma waweze kumuaga Kiongozi huyo