Yahoo imeanza kusumbua sana miezi ya karibuni tangu walipoanza kutambulisha system yao mpya ya 'Yahoo mail beta'
Kwenye software development 'beta' ni final stage kabla software haijawa released kwa matumizi, kwa hiyo mara nyingi 'beta' versions huwa zina faults.
Ushauri wangu usitumie 'Yahoo mail Beta', tumia 'Yahoo mail Classic' au all new yahoo, not 'beta'
Kama bado inasumbua, hamia Gmail, unaweza ukafungua email mpya ya Gmail na ukaredirect mail zako za yahoo ziwe zinaingia kwenye email yako mpya ya gmail kuondoa usumbufu wa kumtaarifu kila mtu kuwa umebadili email address
Yahoo ilinisumbua sana wiki 3 zilizopita, nilikuwa siwezi kulogin kwenye mail account, ila naweza kulogin kwenye messenger. Nilitafuta msaada kwenye 'yahoo service chat' ambayo waliniweka kwenye queue zaidi ya masaa matatu, nilipofanikiwa kulogin, nkamodify settings mail zote nkazidirect kwenye Gmail, sijawah pata usumbufu kwenye Gmail.