Candid Scope
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 11,883
- 6,884
Yah. kuondolewa thread zinazokiuka sheria, maadili, miongozo na taaluma
Nikiwa mdau mmojawapo wa hapa JF, kumekuwepo na malalamiko mengi kuhusu kuondolewa kwa baadhi ya mada zinazoletwa. Pengine ni kutokana na wengi wetu tunapoleta mada kutokuwa makini kwa kuangalia vigezo ambavyo ni muhimu kwa mtandao ambao ni public.
Nchi kama Marekani habari iliyoandikwa kuhusu Usalama wa Taifa kwa kudonoa majina ya wahusika, namba zao za simu, walikozaliwa na mengineyo lingekuwa kosa kubwa ambalo bila ajizi ni kufungiwa gazeti hilo for good na mhusika kupambana na mkono wa sheria kitu ambacho ni kuishia kifungoni. Ref: "Intelligence Identities Protection Act" ya US.
Hii mitandao inaongozwa na sheria za wanao-provide, ukivunja sheria zao tutakuja lalamika kukosa uhondo na hazina kubwa ambayo tunaifaidi kwa sasa hapa.
Uhuru nao ukizidi unashtukia umekiuka mambo mengi na kusababisha matatizo, tuwe na kiasi na tutafaidi tunachotaka.
Asante sana kwa mmiliki wa Mtandao huu na shukrani kwa uhuru aliotupa ambao kwa mapana na marefu hakuna mtandao mwingine Tanzania ambao unaweza kufikia uhuru huo hata kwa 50%. Vema tuutumie vema uhuru huu kwa manufaa yetu na nchi yetu.
Candid Scope
Nikiwa mdau mmojawapo wa hapa JF, kumekuwepo na malalamiko mengi kuhusu kuondolewa kwa baadhi ya mada zinazoletwa. Pengine ni kutokana na wengi wetu tunapoleta mada kutokuwa makini kwa kuangalia vigezo ambavyo ni muhimu kwa mtandao ambao ni public.
Nchi kama Marekani habari iliyoandikwa kuhusu Usalama wa Taifa kwa kudonoa majina ya wahusika, namba zao za simu, walikozaliwa na mengineyo lingekuwa kosa kubwa ambalo bila ajizi ni kufungiwa gazeti hilo for good na mhusika kupambana na mkono wa sheria kitu ambacho ni kuishia kifungoni. Ref: "Intelligence Identities Protection Act" ya US.
Hii mitandao inaongozwa na sheria za wanao-provide, ukivunja sheria zao tutakuja lalamika kukosa uhondo na hazina kubwa ambayo tunaifaidi kwa sasa hapa.
Uhuru nao ukizidi unashtukia umekiuka mambo mengi na kusababisha matatizo, tuwe na kiasi na tutafaidi tunachotaka.
Asante sana kwa mmiliki wa Mtandao huu na shukrani kwa uhuru aliotupa ambao kwa mapana na marefu hakuna mtandao mwingine Tanzania ambao unaweza kufikia uhuru huo hata kwa 50%. Vema tuutumie vema uhuru huu kwa manufaa yetu na nchi yetu.
Candid Scope