Napenda kueleza kuwa mimi ni mfuatiliaji sana wa siasa za Kenya. Namshangaa Odinga kulalamika kuwa amedhulumiwa kwenye uchaguzi, anabishana na ukweli. Ukweli ni kwamba siku alipogombana na Ruto ndipo siku alipopoteza urais. Ruto ni mwanasiasa mwenye ushawishi mkubwa kule bonde la ufa ambalo linakaribia wapiga kura asilimia 30. Huwezi kupoteza rift valley ukawa rais kenya. Odinga alishindwa kumvumilia Ruto ambaye ni a very controversial politician.
Hali hii ya kushindwa kuwavumilia wanasiasa 'controversial" ndani ya chadema itakigharimu sana chama kama ilivyoigharimu ODM. Nimesomo mahali eti chadema bado wanakazania kumfukuza Shibuda. Nina ushahidi pamoja na kwamba hardliners watanipuuza kuwa Shibuda ana ushawishi sana usukumani ambayo inawapiga kura wengi. Hii inatokana na ujasiri wake wa kuwatetea wakulima wa pamba na wafugaji kwa muda mrefu. Lakini Shibuda anazifahamu sana fitna za kisiasa hasa za usukumani. Waulize CCM wanamfahamu, maana hata pamoja na kumfanyia visa vingi, alishinda Maswa kwa kishindo na kupata pia madiwani wengi. Ni ukweli pia kuwa baada ya Chadema kukosana na Shibuda ushawishi wa Chadema kwa Wasukuma umepungua, nina ushahidi, fuatilia hata uchaguzi wa madiwani uliopita.
Ushauri. Shibuda ni mtu "controversial" lakini muhimu. Gharama ya kumvumilia ni ndogo kuliko kumfukuza. Ukimfukuza leo kwanza ataenda mahakamani na ataendelea kuwa mbunge lakini pia atalitumia jukwaa vibaya litakiumiza sana chama. Mimi naamini, kiongozi mzuri ni yule ambaye anaweza pia kuwaongoza watu wanaotofautiana nae kimawazo na pia watu controversial. Namshauri Mh Mbowe ajaribu kukaa na Shibuda na amuulize anataka nini. Nimeshawahi kukaa nae mara nyingi, anacholalamikia ni kwamba chama kimemtenga. Mchawi mpe mwanao, ningekuwa mimi Mbowe ningemteuwa kuwa waziri kivuli wa kilimo na mifugo. Acha akawatetee wasukuma wenzake lakini chama kijengeke kuliko kuhangaika nae. Hata nilikuwa na Mbunge mwenzake wa Maswa Magharibi siku moja anakiri Shibuda anaushawishi mkubwa. Naomba mkumbuke maneno yangu, Chadema will never be the same without Shibuda, Zitto et al. Chama kijenge uvumilivu ambapo CCM ndipo walipoizidi Chadema. Wao wanauvumilivu hata kwa wale wanaoitukana CCM. Nadhani tunakubali, akina Mwampamba na Shonza kelele zao si kwamba hazina madhara, tungekaa nao tangia mwanzo mambo yangemalizwa vizuri.
Mwisho namshauri Rais wangu Dr Slaa ambaye nampenda sana, ajifunze kutofautisha mamlaka ya dola na uongozi wa siasa. Ukiwa rais wa nchi unakuwa na mamlaka ya dola, unaweza kumfukuza mtu yeyote wakati wowote. Ila kwenye siasa hili haliwezekani, ni lazima kuwavumilia watu, kikubwa kutana nao, wasikilize shida zao, washauri na kuwa nao karibu. Siasa ni hiari, mamlaka ya dola hayahitaji kuwa na watu wenye hiari.
Long live Chadema!
Hali hii ya kushindwa kuwavumilia wanasiasa 'controversial" ndani ya chadema itakigharimu sana chama kama ilivyoigharimu ODM. Nimesomo mahali eti chadema bado wanakazania kumfukuza Shibuda. Nina ushahidi pamoja na kwamba hardliners watanipuuza kuwa Shibuda ana ushawishi sana usukumani ambayo inawapiga kura wengi. Hii inatokana na ujasiri wake wa kuwatetea wakulima wa pamba na wafugaji kwa muda mrefu. Lakini Shibuda anazifahamu sana fitna za kisiasa hasa za usukumani. Waulize CCM wanamfahamu, maana hata pamoja na kumfanyia visa vingi, alishinda Maswa kwa kishindo na kupata pia madiwani wengi. Ni ukweli pia kuwa baada ya Chadema kukosana na Shibuda ushawishi wa Chadema kwa Wasukuma umepungua, nina ushahidi, fuatilia hata uchaguzi wa madiwani uliopita.
Ushauri. Shibuda ni mtu "controversial" lakini muhimu. Gharama ya kumvumilia ni ndogo kuliko kumfukuza. Ukimfukuza leo kwanza ataenda mahakamani na ataendelea kuwa mbunge lakini pia atalitumia jukwaa vibaya litakiumiza sana chama. Mimi naamini, kiongozi mzuri ni yule ambaye anaweza pia kuwaongoza watu wanaotofautiana nae kimawazo na pia watu controversial. Namshauri Mh Mbowe ajaribu kukaa na Shibuda na amuulize anataka nini. Nimeshawahi kukaa nae mara nyingi, anacholalamikia ni kwamba chama kimemtenga. Mchawi mpe mwanao, ningekuwa mimi Mbowe ningemteuwa kuwa waziri kivuli wa kilimo na mifugo. Acha akawatetee wasukuma wenzake lakini chama kijengeke kuliko kuhangaika nae. Hata nilikuwa na Mbunge mwenzake wa Maswa Magharibi siku moja anakiri Shibuda anaushawishi mkubwa. Naomba mkumbuke maneno yangu, Chadema will never be the same without Shibuda, Zitto et al. Chama kijenge uvumilivu ambapo CCM ndipo walipoizidi Chadema. Wao wanauvumilivu hata kwa wale wanaoitukana CCM. Nadhani tunakubali, akina Mwampamba na Shonza kelele zao si kwamba hazina madhara, tungekaa nao tangia mwanzo mambo yangemalizwa vizuri.
Mwisho namshauri Rais wangu Dr Slaa ambaye nampenda sana, ajifunze kutofautisha mamlaka ya dola na uongozi wa siasa. Ukiwa rais wa nchi unakuwa na mamlaka ya dola, unaweza kumfukuza mtu yeyote wakati wowote. Ila kwenye siasa hili haliwezekani, ni lazima kuwavumilia watu, kikubwa kutana nao, wasikilize shida zao, washauri na kuwa nao karibu. Siasa ni hiari, mamlaka ya dola hayahitaji kuwa na watu wenye hiari.
Long live Chadema!