Ya Ruto na Odinga Kuwagharimu Mbowe/Dr Slaa/Shibuda

Ya Ruto na Odinga Kuwagharimu Mbowe/Dr Slaa/Shibuda

Naona tunajaribu kufananisha vitu ambavyo havina hata chembe ya kufanana.
 
Anatengwa kwasababu ni muongeaji mno..kuna mambo ambayo ni "inside" issues huwezi kumwambia kila mtu, busara ndogo tu huwa inahitajika, huhitaji kuwa rocket scientist kujua kuwa you don't share inside info with the "other side".. Sometimes the most trivial info could be very compromising..!! Sasa huwezi kuweka close mtu anaye-behave kwa namna hiyo!! Hao Shonza na wenzake are simply pathetic!!!!! Lakini yote uliyoshauri kwa ujumla wake yanaleta maana!

Nahisi kama unataka kutueleza kuwa katika siasa kuna siri nzito, Si kweli.Walichotofautiana na viongozi waCDM na Shibuda na kukataa kumsusa Kikwete wakati wabunge wa CDM walipotoka nje ya bunge. This is a very trivial matter ndio maana baadaye wote waliotoka nje ya bunge walienda Ikulu kwa Kikwete huyo huyo na baadaye wakamwagia sifa kemkem wakati wa uzinduzi wa barabara na miradi mingine ya maendeleo katika majimbo yao.

Ushauri wa mtoa mada ni muafaka sana.
 
Huko kanda ya Ziwa wameshasema asiposimama Zitto Chadema haipati kitu!

Nilikuwa Shinyanga juzi juzi naongea na wakereketwa wa Chadema mitaa ya majengo wamenipa hii habari.
 
Lakini swali langu linabaki pale pale: je, Shibuda anaweza kuvutia kura zote za Wasukuma ambao ni karibu 25% ya Watanzania? Jibu ni hapana. Kwa sababu Tanzania hatuchagui viongozi kufuatana na dini zao.

Umechanganya habari ya dini na kabila.
 
Sabau hatokei kaskazini ndio maana wanamtenga na pia wanahisi mbio za urais atawapita

----!!! Umetimiza wajibu wako kwa leo, wahi Lumumba ukavute mkwanja!!!!!

Tiba
 
Huko kanda ya Ziwa wameshasema asiposimama Zitto Chadema haipati kitu!

Nilikuwa Shinyanga juzi juzi naongea na wakereketwa wa Chadema mitaa ya majengo wamenipa hii habari.

Mkuu tumuombe mwenyezi Mungu muumba Mbingu na Nchi atupe uhai kwa ujumla wetu tushuhudie uchaguzi mkuu unao tarajiwa kufanyika nchini mwaka 2015.

Huwa napata taabu sana, je masalia mtachangia nini hapa JF mara tu baada ya uchaguzi wa 2015?
 
Hakuna chama kisicho na mamluki na dawa ya mamluki si kimfukuza na kulumbana nae bali kumnyima tu information muhimu za chama

Na ndiyo sababu ya Shibuda kulalamika kutengwa.Na hapohapo unashauri apewe uwaziri kivuli.Nikuulize bado huna uhakika kuwa Shibuda ni pandikizi na ana mkono wake mkubwa tu hata kwenye sakata la hawa watoto wanaopiga kelele kila siku gazeti la mtanzania?
 
Nahisi kama unataka kutueleza kuwa katika siasa kuna siri nzito, Si kweli.Walichotofautiana na viongozi waCDM na Shibuda na kukataa kumsusa Kikwete wakati wabunge wa CDM walipotoka nje ya bunge. This is a very trivial matter ndio maana baadaye wote waliotoka nje ya bunge walienda Ikulu kwa Kikwete huyo huyo na baadaye wakamwagia sifa kemkem wakati wa uzinduzi wa barabara na miradi mingine ya maendeleo katika majimbo yao.


Ushauri wa mtoa mada ni muafaka sana.[/QUOTE)

Sijasema lazima iwe siri nzito, ndio maana ukisoma vizuri nimesema "the most trivial of info can be very compromising!!!!!" Hilo unaloliongelea ni moja tu kati ya mengi usiyoyajua...!! He is not lethal, simply negligent, in my views...
 
Umechanganya habari ya dini na kabila.

Hivi hizi statistics za idadi ya makabila watu uwaga wanazitoa wapi? au sielewe wanakuwa wanamaanisha nini?, manake sijawahi kusikia watu wa kihesabiwa kwa makabila yao.
 
Hivi hizi statistics za idadi ya makabila watu uwaga wanazitoa wapi? au sielewe wanakuwa wanamaanisha nini?, manake sijawahi kusikia watu wa kihesabiwa kwa makabila yao.
Hizo statistics mbona zipo tangu enzi za ukoloni?
 
Japo mimi simpendi Shibuda ila analysis ya mtoa uzi naikubali. Huwezi ukatupa wavu baharini na ukavua samaki tu, never, lazima uvue na makokolo. Sasa Shibuda ni kokolo la lazima kwa idadi ya samaki tunaotakiwa kuwavua ndani ya usiku mmoja.
 
Moi alikua Mkikuyu? Uchaguzi wa 2007 ilikua wazi RAO aliibiwa hata idadi ya wabunge alikuokua nao ni kubwa ndio maana Spika na Naibu Spika wote walitoka ODM. Mwaka huu mambo yalikua tofauti kabisa, suala la Ruto limamuathili sana RAO katika uchaguzi huu hilo liko wazi.

Moi ni kwasababu alikuwa Makamu wa RAIS... haukumbuki JINSI JOMO KENYATTA alivyosafirishwa Usiku usiku kufia MOMBASA, MOI alikuwa hakui isipokuwa Wakikuyu kina SAITOTI na JAJI MKUU walikuwa upande wake... Walikuwa hawamtaki CHARLES NJONJO awe Rais wa KENYA... ndipo hapo MOI akasalimika lakini angalia Makamu wake wote ni Wakikuyu na alimpa kanu UHURU KENYATTA... ndio yeye aliyemuingiza kwenye SIASA akiwa na Miaka 32... PAY BACK is HEALTHY eh!!!
 
Ni bora kuzikosa kura za mtu huyu kwani ni msaliti.Cdm songa mbele usirudi nyuma.
Napenda kueleza kuwa mimi ni mfuatiliaji sana wa siasa za Kenya. Namshangaa Odinga kulalamika kuwa amedhulumiwa kwenye uchaguzi, anabishana na ukweli. Ukweli ni kwamba siku alipogombana na Ruto ndipo siku alipopoteza urais. Ruto ni mwanasiasa mwenye ushawishi mkubwa kule bonde la ufa ambalo linakaribia wapiga kura asilimia 30. Huwezi kupoteza rift valley ukawa rais kenya. Odinga alishindwa kumvumilia Ruto ambaye ni a very controversial politician.

Hali hii ya kushindwa kuwavumilia wanasiasa 'controversial" ndani ya chadema itakigharimu sana chama kama ilivyoigharimu ODM. Nimesomo mahali eti chadema bado wanakazania kumfukuza Shibuda. Nina ushahidi pamoja na kwamba hardliners watanipuuza kuwa Shibuda ana ushawishi sana usukumani ambayo inawapiga kura wengi. Hii inatokana na ujasiri wake wa kuwatetea wakulima wa pamba na wafugaji kwa muda mrefu. Lakini Shibuda anazifahamu sana fitna za kisiasa hasa za usukumani. Waulize CCM wanamfahamu, maana hata pamoja na kumfanyia visa vingi, alishinda Maswa kwa kishindo na kupata pia madiwani wengi. Ni ukweli pia kuwa baada ya Chadema kukosana na Shibuda ushawishi wa Chadema kwa Wasukuma umepungua, nina ushahidi, fuatilia hata uchaguzi wa madiwani uliopita.

Ushauri. Shibuda ni mtu "controversial" lakini muhimu. Gharama ya kumvumilia ni ndogo kuliko kumfukuza. Ukimfukuza leo kwanza ataenda mahakamani na ataendelea kuwa mbunge lakini pia atalitumia jukwaa vibaya litakiumiza sana chama. Mimi naamini, kiongozi mzuri ni yule ambaye anaweza pia kuwaongoza watu wanaotofautiana nae kimawazo na pia watu controversial. Namshauri Mh Mbowe ajaribu kukaa na Shibuda na amuulize anataka nini. Nimeshawahi kukaa nae mara nyingi, anacholalamikia ni kwamba chama kimemtenga. Mchawi mpe mwanao, ningekuwa mimi Mbowe ningemteuwa kuwa waziri kivuli wa kilimo na mifugo. Acha akawatetee wasukuma wenzake lakini chama kijengeke kuliko kuhangaika nae. Hata nilikuwa na Mbunge mwenzake wa Maswa Magharibi siku moja anakiri Shibuda anaushawishi mkubwa. Naomba mkumbuke maneno yangu, Chadema will never be the same without Shibuda, Zitto et al. Chama kijenge uvumilivu ambapo CCM ndipo walipoizidi Chadema. Wao wanauvumilivu hata kwa wale wanaoitukana CCM. Nadhani tunakubali, akina Mwampamba na Shonza kelele zao si kwamba hazina madhara, tungekaa nao tangia mwanzo mambo yangemalizwa vizuri.

Mwisho namshauri Rais wangu Dr Slaa ambaye nampenda sana, ajifunze kutofautisha mamlaka ya dola na uongozi wa siasa. Ukiwa rais wa nchi unakuwa na mamlaka ya dola, unaweza kumfukuza mtu yeyote wakati wowote. Ila kwenye siasa hili haliwezekani, ni lazima kuwavumilia watu, kikubwa kutana nao, wasikilize shida zao, washauri na kuwa nao karibu. Siasa ni hiari, mamlaka ya dola hayahitaji kuwa na watu wenye hiari.

Long live Chadema!
 
Japo mimi simpendi Shibuda ila analysis ya mtoa uzi naikubali. Huwezi ukatupa wavu baharini na ukavua samaki tu, never, lazima uvue na makokolo. Sasa Shibuda ni kokolo la lazima kwa idadi ya samaki tunaotakiwa kuwavua ndani ya usiku mmoja.
Yeah,hata ukiangalia USA, POWEL ALIMUUNGA MKONO OBOMA REP HAWAKUMKEMEA. TUKUBALI WATU KAMA SHIBUDA WAPO TUWAVUMILIE
 
Napenda kueleza kuwa mimi ni mfuatiliaji sana wa siasa za Kenya. Namshangaa Odinga kulalamika kuwa amedhulumiwa kwenye uchaguzi, anabishana na ukweli. Ukweli ni kwamba siku alipogombana na Ruto ndipo siku alipopoteza urais. Ruto ni mwanasiasa mwenye ushawishi mkubwa kule bonde la ufa ambalo linakaribia wapiga kura asilimia 30. Huwezi kupoteza rift valley ukawa rais kenya. Odinga alishindwa kumvumilia Ruto ambaye ni a very controversial politician.

Hali hii ya kushindwa kuwavumilia wanasiasa 'controversial" ndani ya chadema itakigharimu sana chama kama ilivyoigharimu ODM. Nimesomo mahali eti chadema bado wanakazania kumfukuza Shibuda. Nina ushahidi pamoja na kwamba hardliners watanipuuza kuwa Shibuda ana ushawishi sana usukumani ambayo inawapiga kura wengi. Hii inatokana na ujasiri wake wa kuwatetea wakulima wa pamba na wafugaji kwa muda mrefu. Lakini Shibuda anazifahamu sana fitna za kisiasa hasa za usukumani. Waulize CCM wanamfahamu, maana hata pamoja na kumfanyia visa vingi, alishinda Maswa kwa kishindo na kupata pia madiwani wengi. Ni ukweli pia kuwa baada ya Chadema kukosana na Shibuda ushawishi wa Chadema kwa Wasukuma umepungua, nina ushahidi, fuatilia hata uchaguzi wa madiwani uliopita.

Ushauri. Shibuda ni mtu "controversial" lakini muhimu. Gharama ya kumvumilia ni ndogo kuliko kumfukuza. Ukimfukuza leo kwanza ataenda mahakamani na ataendelea kuwa mbunge lakini pia atalitumia jukwaa vibaya litakiumiza sana chama. Mimi naamini, kiongozi mzuri ni yule ambaye anaweza pia kuwaongoza watu wanaotofautiana nae kimawazo na pia watu controversial. Namshauri Mh Mbowe ajaribu kukaa na Shibuda na amuulize anataka nini. Nimeshawahi kukaa nae mara nyingi, anacholalamikia ni kwamba chama kimemtenga. Mchawi mpe mwanao, ningekuwa mimi Mbowe ningemteuwa kuwa waziri kivuli wa kilimo na mifugo. Acha akawatetee wasukuma wenzake lakini chama kijengeke kuliko kuhangaika nae. Hata nilikuwa na Mbunge mwenzake wa Maswa Magharibi siku moja anakiri Shibuda anaushawishi mkubwa. Naomba mkumbuke maneno yangu, Chadema will never be the same without Shibuda, Zitto et al. Chama kijenge uvumilivu ambapo CCM ndipo walipoizidi Chadema. Wao wanauvumilivu hata kwa wale wanaoitukana CCM. Nadhani tunakubali, akina Mwampamba na Shonza kelele zao si kwamba hazina madhara, tungekaa nao tangia mwanzo mambo yangemalizwa vizuri.

Mwisho namshauri Rais wangu Dr Slaa ambaye nampenda sana, ajifunze kutofautisha mamlaka ya dola na uongozi wa siasa. Ukiwa rais wa nchi unakuwa na mamlaka ya dola, unaweza kumfukuza mtu yeyote wakati wowote. Ila kwenye siasa hili haliwezekani, ni lazima kuwavumilia watu, kikubwa kutana nao, wasikilize shida zao, washauri na kuwa nao karibu. Siasa ni hiari, mamlaka ya dola hayahitaji kuwa na watu wenye hiari.

Long live Chadema!

hapo red panaonesha jinsi ulivyo popo, kimsingi uko too low, hakuna namna ambapo siasa za kenya zinaendana na za bongo, kenya ni ukabila na umaskini wa kutupwa wa watu wa kawaida
 
Napenda kueleza kuwa mimi ni mfuatiliaji sana wa siasa za Kenya. Namshangaa Odinga kulalamika kuwa amedhulumiwa kwenye uchaguzi, anabishana na ukweli. Ukweli ni kwamba siku alipogombana na Ruto ndipo siku alipopoteza urais. Ruto ni mwanasiasa mwenye ushawishi mkubwa kule bonde la ufa ambalo linakaribia wapiga kura asilimia 30. Huwezi kupoteza rift valley ukawa rais kenya. Odinga alishindwa kumvumilia Ruto ambaye ni a very controversial politician.Hali hii ya kushindwa kuwavumilia wanasiasa 'controversial" ndani ya chadema itakigharimu sana chama kama ilivyoigharimu ODM. Nimesomo mahali eti chadema bado wanakazania kumfukuza Shibuda. Nina ushahidi pamoja na kwamba hardliners watanipuuza kuwa Shibuda ana ushawishi sana usukumani ambayo inawapiga kura wengi. Hii inatokana na ujasiri wake wa kuwatetea wakulima wa pamba na wafugaji kwa muda mrefu. Lakini Shibuda anazifahamu sana fitna za kisiasa hasa za usukumani. Waulize CCM wanamfahamu, maana hata pamoja na kumfanyia visa vingi, alishinda Maswa kwa kishindo na kupata pia madiwani wengi. Ni ukweli pia kuwa baada ya Chadema kukosana na Shibuda ushawishi wa Chadema kwa Wasukuma umepungua, nina ushahidi, fuatilia hata uchaguzi wa madiwani uliopita.Ushauri. Shibuda ni mtu "controversial" lakini muhimu. Gharama ya kumvumilia ni ndogo kuliko kumfukuza. Ukimfukuza leo kwanza ataenda mahakamani na ataendelea kuwa mbunge lakini pia atalitumia jukwaa vibaya litakiumiza sana chama. Mimi naamini, kiongozi mzuri ni yule ambaye anaweza pia kuwaongoza watu wanaotofautiana nae kimawazo na pia watu controversial. Namshauri Mh Mbowe ajaribu kukaa na Shibuda na amuulize anataka nini. Nimeshawahi kukaa nae mara nyingi, anacholalamikia ni kwamba chama kimemtenga. Mchawi mpe mwanao, ningekuwa mimi Mbowe ningemteuwa kuwa waziri kivuli wa kilimo na mifugo. Acha akawatetee wasukuma wenzake lakini chama kijengeke kuliko kuhangaika nae. Hata nilikuwa na Mbunge mwenzake wa Maswa Magharibi siku moja anakiri Shibuda anaushawishi mkubwa. Naomba mkumbuke maneno yangu, Chadema will never be the same without Shibuda, Zitto et al. Chama kijenge uvumilivu ambapo CCM ndipo walipoizidi Chadema. Wao wanauvumilivu hata kwa wale wanaoitukana CCM. Nadhani tunakubali, akina Mwampamba na Shonza kelele zao si kwamba hazina madhara, tungekaa nao tangia mwanzo mambo yangemalizwa vizuri.Mwisho namshauri Rais wangu Dr Slaa ambaye nampenda sana, ajifunze kutofautisha mamlaka ya dola na uongozi wa siasa. Ukiwa rais wa nchi unakuwa na mamlaka ya dola, unaweza kumfukuza mtu yeyote wakati wowote. Ila kwenye siasa hili haliwezekani, ni lazima kuwavumilia watu, kikubwa kutana nao, wasikilize shida zao, washauri na kuwa nao karibu. Siasa ni hiari, mamlaka ya dola hayahitaji kuwa na watu wenye hiari. Long live Chadema!
Shibuda haaminiki na anafahamu hilo . Ukiona kansa mkononi dawa ni kukata mkono mapema ukifikiria faida ya mkono baadaye utajuta kansa itakapoenea . Shibuda ni mjanja lakini cdm ni wajanja zaidi ndo maana hawana haraka na shibuda
 
Back
Top Bottom