Ww unakumbuka ulianza na simu ipi????

Ww unakumbuka ulianza na simu ipi????

cement

JF-Expert Member
Joined
May 5, 2012
Posts
581
Reaction score
221
simu.jpg

me ya kwanza ni ya 1 ilikuwa
 
mi ya kwangu haiko hapo nilianza na nokia 3210
 
Mimi kwangu haipo hapo niliiokota 2007 nikiwa form 5 natoka shule
 
Mm nianza kumiliki line kwanza mwaka 2004,, baadae 2005 nikamiliki no 2 leo namiliki no 4.
 
Siemens c25 nimeitundika kiunoni hahahahaaaa umenikumbusha kuna jamaaa nilimuomba nim-bipu kaka ili anipigie jamaa akanijibu kuwa simu yake haina button ya kubipia.....I can not forget this till i die
 
Sijaona yangu, ilikuwa siemens C 25, ina kidole kama inataka kujibu swali, that was back in 2001, kipindi hicho miongoni mwa vigezo vya simu kali ni kuwa na vibration, nakumbuka phillips savvy ilikuwa inanunulika kisa ilikuwa na vibration
 
3310 aka jeneza enzi hizo nko f2 mwaka 2001

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Siemens c28 aka twanga pepeta ndo likuwa simu yangu ya mwanzo, hahaha huwezi amini ilipotea mitaa ya Posta nikiwa na sweet heart wangu ambye sasa ndo shemeji yenu tumetoka Sinza naenda chukua mpunga Standard chartered wa kula bata siku hiyo, hee si ikateleza mfukoni ikadondokea kwenye kiti mwenyewe sina habari, ndo ikawa mwisho wa Twanga yangu.

Hiyo Namba nne alikuwa nayo late bro wangu, mwenyewe alikuwa anaiweka kwenye kipochi chake anachomeka kwenye mkanda kiunoni utampenda. alipofariki nikawa naitumia, tatizo kubwa ya simu za Ericsson zina matatizo sana ya network, siku moja na shemeji yenu wakati wa uchumba, mie bado naishi na bro wangu mkubwa km kawaida yetu tukapanga tukutane pale Sinza Kamanyola hotel flani matata hivi, mzee nimewahi niko inside km dk ishirini kumbe na yeye kaja ananipigia hanipati, mie simu yangu ukiiangalia inaoneka iko vizuri tu muda unakwenda nikaanza kulaani, kumbe na yeye yupo nje ananilaani, nikatoka nje wapi simu inaonekana iko fiti, baada ya ssaa nzima si nikatoka zangu na hasira vibaya mnoo, kumbe na yeye ana hasiza zaidi ya kwangu. baada ya km nusu saa nipo migomigo si sms zikaanza kuingia ni matusi mtindo mmoja. nampigia alipopokea simu tu na lawama juu wewe ulikuwa na baamedi kwani sijui hahahahaha dah iliniletea msala hiyo simu sisahau!!
 
namba 3,wakati nikiwa mwaka wa kwanza udsm 2004!then ikaibwa na rum mate wakati nimejilaza zangu hall 5!Sikukaa nayo hata mwezi!you remind me back to that time.
 
Nilianza na Trium, hiyo ilikuwa na vibration kiasi kwamba hata ukiwa kwenye Lecture kule ATLB, hutasemwa vibaya na Nshomile Prof. Rugumamu au Ngwale kama itaita kwa sauti kubwa !!!
 
Duh hii inanikumbusha jinsi watu walivyokuwa wakifikiria mimi ni afisa usala wa taifa nilikuwa naheshimika mitaani nikienda maali lazima niiweke mezani kumiliki simu enzi hizo ilikuwa raha sio siku hizi mtu huna kazi unamili simu unapiga mizinga ya vocha kwa watu
Nilikuja na hii simu Tanzania mwaka huo wa 1992, wakati huo hapakuwa na mitandao ya simu . Siku moja kwa udadisi wangu tu nikapiga namba 999. Kwa mshangao mkubwa nilijibiwa kuwa 'hapa ni Polisi Chuo kikuu, tukusaidie nini?'. Ghafla nilikata na kushangaa kuwa kumbe hata kama mtandao wa mobile phones ulikuwa bado kutangazwa rasmi, lakini simu yangu iliweza kupokelewa nikipiga hiyo namba ya emergency!
 
Back
Top Bottom