NAMTUMBA
JF-Expert Member
- Feb 20, 2014
- 1,939
- 600
Ifike mahali jeshi la polisi hasa kitengo cha usalama barabarani kianzishe utaratibu wakusindikiza mabasi yote ya abiria kwa kupokezana kama ile staili ya mwenge wa Uhuru. Askari wa DSM wasindikize hadi pwani. Pwani wasindikize hadi Moro, tanga etc. Kutoka hapo wapokee wengine kama ni iringa, Dodoma, singida na kwingineko. Kama kuna garama zozote kwa askari zilipwe na wenye mabasi, serikali isigaramie chochote zaidi yakujitolea askari wake. Askari hawa watawamonitor madereva kuanzia mwanzo wa safari hadi mwisho. Naamini hii itasaidia kupunguza ajali.