Juma lililopita nilisafiri kupitia JNIA. Kitu cha kwanza baada ya kucheck-in pamoja na mizigo yangu nililakiwa na kijana (Security personnel) akaniuliza kama tiketi yangu ilinunuliwa mwezi huu (July 2012) au kabla. Nilimwuliza, kulikoni? Akanieleza kama nilinunua kabla ya July 2012 basi ni lazima nilipie kiasi cha $10 kwani kodi imepanda kutoka $20 hadi $40. Nikamweleza yule kijana kuwa tkt yangu ilinunuliwa June 2012 na hilo ongezeko silipi.
Nilipofika kwenye meza ya kupata boarding pass walinipa boarding pass yangu halafu yule dada akaniambia nimwone mtu wa kodi. Nilikwenda kwa yule dada na kumweleza kuwa mimi sitembei na pesa na kama anataka pesa yangu basi achukue kutoka kwenye credit card yangu. Akanywea, nikaondoka zangu. Wakati wote nikiwa kwenye mstari nilikuwa naangalia kinachoendelea pale kwenye desk la "kodi". Watu walikuwa wanatoa pesa lakini lakini hakuna risiti iliyokuwa inatolewa kwa pesa iliyopokelewa bali kugonga mhuri kwenye boarding pass. Huu ni wizi wa waziwazi. Cha kusikitisha ni kuwa wengi waliokuwa wanatoa pesa walikuwa ni Watanzania kwani wageni, hasa wazungu walikuwa wanaogopwa.
Licha ya tukio hili la jana pale JNIA kuna uswahili na ulaghai kwelikweli. Security personnel wa pale kazi yao ni kubughudhi wasafiri. Mara kadhaa wameniambia kuwa wanauza Kadi za Chanjo, n.k.
Nilipofika kwenye meza ya kupata boarding pass walinipa boarding pass yangu halafu yule dada akaniambia nimwone mtu wa kodi. Nilikwenda kwa yule dada na kumweleza kuwa mimi sitembei na pesa na kama anataka pesa yangu basi achukue kutoka kwenye credit card yangu. Akanywea, nikaondoka zangu. Wakati wote nikiwa kwenye mstari nilikuwa naangalia kinachoendelea pale kwenye desk la "kodi". Watu walikuwa wanatoa pesa lakini lakini hakuna risiti iliyokuwa inatolewa kwa pesa iliyopokelewa bali kugonga mhuri kwenye boarding pass. Huu ni wizi wa waziwazi. Cha kusikitisha ni kuwa wengi waliokuwa wanatoa pesa walikuwa ni Watanzania kwani wageni, hasa wazungu walikuwa wanaogopwa.
Licha ya tukio hili la jana pale JNIA kuna uswahili na ulaghai kwelikweli. Security personnel wa pale kazi yao ni kubughudhi wasafiri. Mara kadhaa wameniambia kuwa wanauza Kadi za Chanjo, n.k.