Kiongozi Miongoni
Senior Member
- Feb 6, 2021
- 197
- 255
Wasalaam wana wa Jehova.
Kuna tatizo linaendelea kuwa sugu katika jamii yetu. Kuna kitu kinaitwa masega kwenye exhaust ya magari na hiki kitu kina kazi maalumu katika mfumo wa gari, sijui kazi yake kubwa ni nini kwa maana mimi siyo mtaalam wa mambo ya magari.
Last week gari yangu ilikuwa inapoteza nguvu na kutoa mlio mkubwa inapokuwa inatembea, niliamua kupeleka kwa fundi mmoja hapa mjini ninapoishi. Baada ya kufanya ukaguzi wa gari, fundi aliniambia kuwa gari tiyari imeibiwa masega.
Nilimuuliza fundi je yanaonekana kuibiwa lini, fundi akasema inaonekana yameibiwa kitambo na akaniambia kuwa wezi wa masega ni wengi na wayaiba kwa haraka sana.
Basi nikamwambia anitafutie masega mapya niweke, yule fundi alikataa kunitafutia masega kwa madai kwamba nisijaribu kuweka masega mapya maana nitagombana na watu, kwamba nikishaweka masega mapya ntakuwa simwamini mtu yoyote kumpa gari na kwamba hata nikipeleka gari garage itabidi kikae kwa sababu ntakuwa na wasi wasi kuwa yataibiwa tena.
Fundi anasema magari mengi yameibiwa masega ila wamiliki hawajui kwa sababu magari yao hayajasumbua.
Sasa najiuliza masega yanatumika kufanyia kazi gani na kwa nini yamekuwa ni deal kubwa kiasi hiki?.
Je, serikali haioni umuhimu wa kulifuatilia suala hili?
Wasalaam.
Kuna tatizo linaendelea kuwa sugu katika jamii yetu. Kuna kitu kinaitwa masega kwenye exhaust ya magari na hiki kitu kina kazi maalumu katika mfumo wa gari, sijui kazi yake kubwa ni nini kwa maana mimi siyo mtaalam wa mambo ya magari.
Last week gari yangu ilikuwa inapoteza nguvu na kutoa mlio mkubwa inapokuwa inatembea, niliamua kupeleka kwa fundi mmoja hapa mjini ninapoishi. Baada ya kufanya ukaguzi wa gari, fundi aliniambia kuwa gari tiyari imeibiwa masega.
Nilimuuliza fundi je yanaonekana kuibiwa lini, fundi akasema inaonekana yameibiwa kitambo na akaniambia kuwa wezi wa masega ni wengi na wayaiba kwa haraka sana.
Basi nikamwambia anitafutie masega mapya niweke, yule fundi alikataa kunitafutia masega kwa madai kwamba nisijaribu kuweka masega mapya maana nitagombana na watu, kwamba nikishaweka masega mapya ntakuwa simwamini mtu yoyote kumpa gari na kwamba hata nikipeleka gari garage itabidi kikae kwa sababu ntakuwa na wasi wasi kuwa yataibiwa tena.
Fundi anasema magari mengi yameibiwa masega ila wamiliki hawajui kwa sababu magari yao hayajasumbua.
Sasa najiuliza masega yanatumika kufanyia kazi gani na kwa nini yamekuwa ni deal kubwa kiasi hiki?.
Je, serikali haioni umuhimu wa kulifuatilia suala hili?
Wasalaam.