trudie
JF-Expert Member
- Jan 15, 2014
- 4,546
- 11,136
Habari wanajukwaa,
Kuna aina ya wizi unaendelea mkoani Mwanza unaweza kuwa wa kitambo sana lakini umeshamiri katika wiki hii hivyo naomba muwe makini sana.
Kuna kijana mmoja mtanashati tena ukimwona ana heshima zake anatembelea kwenye maduka ya jumla, rejareja na pia deport za bia na soda kufanya utapeli wake kwa mtandao.Ninasimulia kifupi alivyonipata ili muwe makini nae kama ana wenzie pia.
Jana mida ya asubuhi kijana mmoja alikuja dukani kwangu nauza bia za jumla na pombe kali akauliza bei ya Zanzi kubwa nikamtajia akaomba kupunguziwa sababu hakuwa nayo.
Wakati tunaelewana bei akatoa simu yake akampigia mtu kumjulisha kwamba bei ya Zanzi sio kama waliyotegemea ila simu ikazima kabla hawajaelewana.
Akaniomba dada naazima simu yako nimjulishe mwenzangu nikamjibu sina dakika akasema hata meseji tu nitume nikampa.Akatuma meseji akarudisha simu akaaga ngoja nitoe hela hapo narudi.
Baada ya kama nusu saa simu yangu ikaita namba imeseviwa jina la Mamamkwe wangu nikapokea lakini hatukuelewana simu ikakatika akatuma meseji una laki 5 hapo nikamjibu hapana sina kwa sasa.
Akaniuliza kiwango nilicho nacho nikamjibu nina laki 2 akaomba naomba nitumie 195000 kuna mtu anasubiri na namba akaituma ya kumtumia mtu huyo na jina litakalotokea baada ya kutuma. Sababu mamakwe wangu ni mtu wa biashara hapa Mwanza sikusita nikamtumia akashukuru tukaagana kwa meseji.
Baada ya masaa kama 5 akatuma meseji tena anauliza una shilingi ngapi sasa hivi hapo ndio nikastuka sio kawaida mama aulizie mauzo yangu basi nikampigia mwenzangu amuulize mama ni anakosea meseji anamtumia mfanyakazi wake au ni vipi.
Baada ya hapo ndio tukajua tumetapeliwa ila sikuelewa kivipi namba ninayo kwenye simu na imeseviwa kabisa.
Kumbe anachofanya ukimpa simu anaangalia Call log ile namba uliyowasiliana nayo karibuni anaandika namba yake anaisave kwa jina hilo hilo ndio anatumia kutapeli akijua mtu mpaka ugundue ni ngumu sana.
Jana ametapeli maduka mengi sana maeneo ya Mkuyuni na ataendelea kutapeli kwa hiyo muwe makini nae sana.Ni wizi wa kizamani lakini mtu huwezi jua siku wala saa.
Poleni kwa waraka mrefu najua utawasaidia wakazi wenzangu wa Mwanza kwa mwizi huyu.
Kuna aina ya wizi unaendelea mkoani Mwanza unaweza kuwa wa kitambo sana lakini umeshamiri katika wiki hii hivyo naomba muwe makini sana.
Kuna kijana mmoja mtanashati tena ukimwona ana heshima zake anatembelea kwenye maduka ya jumla, rejareja na pia deport za bia na soda kufanya utapeli wake kwa mtandao.Ninasimulia kifupi alivyonipata ili muwe makini nae kama ana wenzie pia.
Jana mida ya asubuhi kijana mmoja alikuja dukani kwangu nauza bia za jumla na pombe kali akauliza bei ya Zanzi kubwa nikamtajia akaomba kupunguziwa sababu hakuwa nayo.
Wakati tunaelewana bei akatoa simu yake akampigia mtu kumjulisha kwamba bei ya Zanzi sio kama waliyotegemea ila simu ikazima kabla hawajaelewana.
Akaniomba dada naazima simu yako nimjulishe mwenzangu nikamjibu sina dakika akasema hata meseji tu nitume nikampa.Akatuma meseji akarudisha simu akaaga ngoja nitoe hela hapo narudi.
Baada ya kama nusu saa simu yangu ikaita namba imeseviwa jina la Mamamkwe wangu nikapokea lakini hatukuelewana simu ikakatika akatuma meseji una laki 5 hapo nikamjibu hapana sina kwa sasa.
Akaniuliza kiwango nilicho nacho nikamjibu nina laki 2 akaomba naomba nitumie 195000 kuna mtu anasubiri na namba akaituma ya kumtumia mtu huyo na jina litakalotokea baada ya kutuma. Sababu mamakwe wangu ni mtu wa biashara hapa Mwanza sikusita nikamtumia akashukuru tukaagana kwa meseji.
Baada ya masaa kama 5 akatuma meseji tena anauliza una shilingi ngapi sasa hivi hapo ndio nikastuka sio kawaida mama aulizie mauzo yangu basi nikampigia mwenzangu amuulize mama ni anakosea meseji anamtumia mfanyakazi wake au ni vipi.
Baada ya hapo ndio tukajua tumetapeliwa ila sikuelewa kivipi namba ninayo kwenye simu na imeseviwa kabisa.
Kumbe anachofanya ukimpa simu anaangalia Call log ile namba uliyowasiliana nayo karibuni anaandika namba yake anaisave kwa jina hilo hilo ndio anatumia kutapeli akijua mtu mpaka ugundue ni ngumu sana.
Jana ametapeli maduka mengi sana maeneo ya Mkuyuni na ataendelea kutapeli kwa hiyo muwe makini nae sana.Ni wizi wa kizamani lakini mtu huwezi jua siku wala saa.
Poleni kwa waraka mrefu najua utawasaidia wakazi wenzangu wa Mwanza kwa mwizi huyu.