Naungana na wachangiaji wengi apo juu kulalama wizi wa kwenye atm,ila kiukweli kuiba kwenye atm ni ngumu hasa kwa benki zilizojipanga kitechnologia. Ila wateja pia tuweni macho,mtu asikupigie simu kuomba namba za kadi,muda ulioandikwa kwenye kadi,wala chochote kuhusu akaunti. Mwanzo wa kuibiwa ni apo tu. Ukitoa detail zako ovyo,mtu anaweza kuwa amekaa chumbani kwake urusi akavuta salio lako kwa detail ulizompa. Kuna jamaa anasema Crdb pia wanaibiwa,sikatai. Pia mwingne anasema wanaibiwa ila kulinda heshima ya kampun ukipiga kelele wanakurudshia. Kutoka wapi?-apa hamna cha heshima, ni kuwa IT ya hawa watu iko powa sana,yani ukiclaim/ukiripoti mapema wanao uwezo wa kutrace nani katoa,wapi katolewa pesa,device gani imetumika,muda tarehe,na hata picha za aliyetoa pesa,mwishowe ananaswa pesa inarudi. Naomba wanajf mtambue kuwa kama mtu hujaibiwa kwa uzembe wako,pesa ikiwa benki ikatolewa bila idhini yako,anayeibiwa ni benki wala si wewe mteja. Benki wanalo jukumu la kukutunzia pesa yako,ikipotea ni wao.