Wizi kimtandao mchana kweupe VODACOM

Wizi kimtandao mchana kweupe VODACOM

VODACOM wakiishiwa kwa tulio na simu na line zao wanaiba mchana kweupee..!
Hebu ona ujumbe nimetumiwa..

"Umetozwa Sh 100.0 TSH kwa ajili ya hadithi BABA NISAMEHE. Piga 0901767676 kuweza kusikiliza simulizi nzuri. Kujitoa tuma neno ONDOA kwenda 15460"

Hapo nipende nisipende nimekatwa shs 100 toka akaunti yangu ya m-pesa.
Halafu ukituma neno ONDOA kwenye namba waliyokupa, ujumbe hauendi maana wsmeublock, na wanaendelea kukukata pesa.

VODACOM wana wateja zaidi ya milioni 10. Hivyo kwa click moja wamekwapua bilioni moja toka kwa wateja wao.

Hata tukilalamika TCRA huwa hakuna action yoyote ya kurudisha hiyo 1b kwa wateja.

Kuna wana sheria humu, twawezaje kishitaki VODACOM kwa wizi huu?
UPDATE

Kulingana na mtandao na toleo la VODACOM, ina jumla ya wateja
Approximately 33.4 million
As of December 2025, Vodacom Tanzania has approximately 33.4 million total subscribers. This includes 19.0 million mobile data customers and 31.5 million M-Pesa subscribers.
Vodacom Tanzania
Wateja wa M -Pesa ni Milioni 31.5
Kwa hiyo kimsingi kwa kuwatoza Tshs 100 kila mmoja, wana kwapua kwa wakati mmoja Bilioni 3.15...!!!!
Huu ni wizi wa kutisha.
 
VODACOM wakiishiwa kwa tulio na simu na line zao wanaiba mchana kweupee..!
Hebu ona ujumbe nimetumiwa..

"Umetozwa Sh 100.0 TSH kwa ajili ya hadithi BABA NISAMEHE. Piga 0901767676 kuweza kusikiliza simulizi nzuri. Kujitoa tuma neno ONDOA kwenda 15460"

Hapo nipende nisipende nimekatwa shs 100 toka akaunti yangu ya m-pesa.
Halafu ukituma neno ONDOA kwenye namba waliyokupa, ujumbe hauendi maana wsmeublock, na wanaendelea kukukata pesa.

VODACOM wana wateja zaidi ya milioni 10. Hivyo kwa click moja wamekwapua bilioni moja toka kwa wateja wao.

Hata tukilalamika TCRA huwa hakuna action yoyote ya kurudisha hiyo 1b kwa wateja.

Kuna wana sheria humu, twawezaje kishitaki VODACOM kwa wizi huu?

UPDATE
Wateja wa M-Pesa Vodacom ni Milioni 31.5.
Hivyo kwa kutozwa Tshs 100 kila mmoja , VODACOM wanaiba Tshs Bilioni 3.13 kwa mpigo.
Tuna TCRA HEWA, Wabunge HEWA, Wizara ya Mawasiliano HEWA, na je tuna Serikali HEWA?
 
Namna gani palee😅mtf
Screenshot_20260722_084827_Messages.jpg
 
Hivi unaamini mtu mzima aliyejiunga JamiiForums since 2014 anaweza akajiunga kwa hela yake kusikiliza hadithi inayoitwa “BABA NISAMEHE”?Kukuonyesha ushahidi haikufanyi kuwa ni wewe ulijiunga kumbuka wanatumia system na system huamrishwa na walio ndani ifanye kipi na ukiuliza wanakujibu juu juu huku wakiijua michezo yao.

OK tuseme alijiunga,kwanini kila mtu hapa awalalamikie hao vodacom kwa kesi moja hii hii ya kutuunganishia wateja huduma tusizozitaka?wamekuja na mtindo mpya kugawa namba zetu kwa kampuni za betting,store za nguo etc simu yangu siku haiishi sijapata ujumbe kutoka “LCWAKIKI” na “AWALHOME” ni kwa ridhaa ya nani mpaka nisumbuliwe na text za huduma nisizozihitaji?
Mkuu nilijaribu tu kuweka sawa kutokana na experience niliyopitia, so kama unatumiwa text ambazo hukujiunga nazo unaweza kuwashitaki mtandao husika mkuu.
 
Back
Top Bottom