Wizara yafafanua taarifa ya kuonekana kwa FARU MWEUSI katika Hifadhi ya Taifa ya Nyerere

John Haramba

JF-Expert Member
Feb 4, 2022
365
1,373
Wizara ya Maliasili na Utalii inapenda kutoa ufafanuzi kwa umma kuhusu taarifa iliyotolewa na mtandao wa Tanzania Times, tarehe 3 Machi, 2022 ikieleza kuonekana kwa faru mweusi katika Hifadhi ya Taifa Nyerere.

Wizara imeeleza kuwa taarifa hiyo ambayo inaendelea kusambaa katika vyombo mbalimbali vya habari na mitandao ya kijamii siyo sahihi na wanaomba ipuuzwe. Ukweli ni kwamba hakuna Faru mweusi aliyeonekana katika hifadhi ya Taifa ya Nyerere kama ilivyoripotiwa na mtandao huo.

Aidha, Wizara imesisitiza kuwa Msemaji Mkuu wa masuala ya wanyampori hapa nchini ikiwemo utoaji wa takwimu na taarifa za wanyamapori kwa umma ni Wizara ya Maliasili na Utalii na si vinginevyo.

45f5fe27-bf21-42e5-ba1e-4c8c27428037.jpg
 
Kwani Faru mweusi ni Ishara gani!? Nuksi balaa au mkosi!? Au heri!?
 
Ana faida gani hasaa..!??
Ni kivutio kikubwa Cha utalii kwa Afrika inasemekana wapo kwetu tu na kenya. Kutokana na umaalum wake Kuna msanii amewahi kujiita "black rhino" kumaanisha hakuna Kama yeye duniani yupo Tanzania pekee. Kwahiyo kutokana na hili Ni kivutio kikubwa Cha watalii na wanalindwa Sana Kama ingekua serikalini tungesema ulinzi wao Ni Kama wa Rais.

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
Ni kivutio kikubwa Cha utalii kwa Afrika inasemekana wapo kwetu tu na kenya. Kutokana na umaalum wake Kuna msanii amewahi kujiita "black rhino" kumaanisha hakuna Kama yeye duniani yupo Tanzania pekee. Kwahiyo kutokana na hili Ni kivutio kikubwa Cha watalii na wanalindwa Sana Kama ingekua serikalini tungesema ulinzi wao Ni Kama wa Rais.

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
👍🏻👍🏻💯💯
 
Ukweli ni kwamba hakuna Faru mweusi aliyeonekana katika hifadhi ya Taifa ya Nyerere kama ilivyoripotiwa na mtandao huo.
Ili kuuthibitishia umma kuwa ni uzushi basi wafungulieni kesi mahakamani kama mlivyoofanya kwa wazushi wengine
 
Back
Top Bottom