Mojawapo ya mambo ambayo baadhi ya vigogo ndani ya chama wanajilaumu sana kuwa yalichangia CCM kufanya vibaya ni "uhuru wa vyombo vya habari". Kuna imani kuwa miaka mitano iliyopita vyombo vya habari vimeachwa vikiichafua serikali na CCM na matokeo yake yameonekana kwenye sanduku la kura. Waraka mmoja ambao uliangukia miguuni mwangu unadokeza kuwa jambo hilo haliwezi na halipaswi kuachwa tena.
Ni maoni yangu kuwa tathmini hiyo ya CCM ni sahihi na kimkakati wa vita ni kuwa unamuweka jenerali mzuri mahali ambapo mnataka madhara makubwa yatokeaa. Jenerali ambaye anajua mbinu vizuri, ana uwezo wa kuthubutu kuleta nidhamu kwenye tasnia ya habari.
Hivyo basi, tuangalie kwa makini ni nani/kina nani watapewa kuiongozi wizara hii ambao ninaamini itakuwa ni propaganda mashine ya hali ya juu lakini wakati huo huo itatumiwa vizuri kuwaleta wahariri wa vyombo kadhaa vya habari kwenye mstari na hata baadhi ya waandishi wa habari. Lengo liko wazi sana - not again vyombo vya habari havitaachwa viwe kama vilivyokuwa. The next battleground itakuwa kwenye Habari.
Binafsi naamini kwa asilimia 100 akitangazwa Waziri wa Habari itathibitisha mtazamo wangu huu - wengine watashangaa mimi nitasema Naam, lets the show begin!
Mzee Mwanakijiji, mtazamo wako unaweza kuwa sahihi ki CCM tuu lakini kiserikali, utakuwa umekuja too lillte too late kwa sababu moja ya majukumu ya lazima kabisa kwa wizara ya habari ya wamu hii, ni kupitisha ile sheria mpya ya habari, ambayo kwa mara ya kwanza nchini Tanzania, haki ya kupata habari, itatambulika kisheria, yaani the right to information.
Hata kama serikali haaipendi sheria hii, uitaingizwa kwenye mbinyo mpaka waipitishe, kama tulivyopitisha shria ya ugaidi na juzi juzi sheria ya kuwahukumu maharamia watekameli wa Kisomali, huku tukiwa hatuna hili wala lile tulijualo, hata licha ya kuona jirani Kenya wakinyolewa na kukubali kwao, sisi kichwa chetu bado hutukitii maji!.
Mwanzo zilikuwa ziletwe sheria mbili, the Media Services Bill na the Right to Information, sasa italetwa sheria moja. Tena ilikuwa iletwe tangu mwaka jana, walipoona ni mwaka wa uchaguzi, serikali kupitia kwa Mkuchika, ika fanya dilly dallying na hatimaye kuichelewesha.
Sheria hiyo ikipita, lile suala la kutafuta habari fulani, unaambiwa fulani hayupo, sasa linakwisha na watendaji wanalazimika kutoa habari pale zinapotakiwa na sio kutoa tuu pale wanapoamua wao. Kwa shria hiyo, sasa unapata uwezo hata wa kuhoji, hivi ile bajeti ya vitafunwa vya Ikulu, imetumikaje na kuweza kuona mzabuni wa kusupply hivyo vitafunwa Ikulu ni nani na amequote bei gani, utashangaa macho yako kumbe kikombe cha chai Ikulu ni 2,000 soda pia 2,000, bia 5,000! etc. Kwa sasa huwezi.
Kuna baadhi ya sheria sisi kama nchi huwa hatusitaki ili waWatanzania waendelee kukosa habari, au kulishwa habari fulani zenye maslahi kwa watawala, that time is over, sasa tuko kwenye information age, hata huu ushindi wa tsunani ya Chadema nau attribute kwenye free flow of information.