Elections 2010 Wito kwa wana mageuzi wote-ccm iliyogawanyika isitugawe

George Maige Nhigula Jr.

JF-Expert Member
Mar 14, 2008
470
149
Ndugu Wana JF,

Napenda kutoa wito kwa wapenda mabadiliko wote kuwa we are very close on the finishing line kuindoa ccm iliyogawanyika madarakani, ambayo ni adui wa wapenda mabadiliko na wanamageuzi wote nchini Tanzania bila kujali itikadi za dini zetu wala makabila yetu, sote kwa pamoja tunaweza kuandika historia na kuwa seehemu ya historia ya nchi hii,

Ni ukweli usiopingika kuwa kila zama na mashujaa wake, imetuchukua mda mrefu sana kufikia hatua hii tuliyofikia hivi sasa ya kuwa na mgombea kutoka kambi ya upinzani ambaye ametoa changamoto kubwa kwa ccm. Hivyo basi inabidi sote tujiulize swali moja Je tunataka kuwa sehemu ya hayo mabadilikoo tunayoyahitaji au tumekuwa consumed na propaganda za ccm zenye misingi ya kidini na ukabila ili waweze kutugawa na kuweza kutimiza ndoto yao yya kuendeleeza kulitawala taifa hili indefenetely?

Sote tunakubaliana na dhana ya FIERCE URGENCY OF NOW, kwamba mabadiliko hayawezi kusubili, kwani tunapokuwa hivi close to the finish line na tukakubali kumezwa na propaganda ambazo hazina msingi na maslahi kwa nchi na taifa letu bali kunufaisha chama cha mapinduzi basi tutakuwa tuna compromise our intellectual intergrity na kile tunacho kiamini to be true.

Nime amua kuyaandika haya kutokana na umakini wangu wa kufatilia maswala na ya kampeni na electrorate psychology kwa chaguzi nyingi za ndani ya Tanzania na nje ya nchi yetu, kwa nchi nyingi zilizo endelea huwa kunakuwa na issues za uchaguzi au agenda za uchaguzi huo, na agenda zenyewe zinakuwa influenced na electrorate yaani wananchi kutokana na mambo ambayo wao wanaona ni muhimu kuyapa kipaumbele. Lakini siasa za kiafrika vyama vya siasa ndo vina dictate agenda za uchaguzi kuwa ipi ina umuhimu kuliko nyingine, na Tanzania imekuwa best scenario.

Hivyo swala la msingi la kujiulizi what are the issues to be given high priority which affect millions of life ya watanzania, na watanzania watakapokwenda kupiga kura jumapili ya Tarehe 31, October 2010 basi wapige kura kutokana na vipaumbele vya agenda muhimu zinazo athiri maisha yao moja kwa moja na si vinginevyo.

Nadhani watanzania weengi watakubaliana nami kuwa uchumi wa Tanzania ni agenda muhimu ya kuzingatia wakati tunakwenda kupiga kura, kwani tumeshuhudia INFLATION ikiwa out of control ambayo imesababisha pesa yetu kushuka thamani sana na kusababisha bei ya bidhaa mbali mbali kupanda wakati kipato cha mtanzania kikiwa pale pale na hivyo basi kuwafanya watanzania wengi kuwa na hali nggumu ya kumudu maisha na kupelekea watanzania wengi kutupwa kwenye umaskini uliokithiri na maisha yasiyokuwa na uhakika.

Hali kadhalika wakati mwananchi wa kawaida ana pambana na hali ngumu ya maisha serikari ya ccm imekuwa iki mtwanga kodi mwananchi (indirect tax) kupitia bidhaa mbali mbali anazununua, wakati matajiri na wafanya biashara mashuuhuri wa ndani na nje wakikwepa au wakipata misamaha ya kodi! Je tulikwisha wahi sikia serikari ikitangaza punguzo la kodi kwwenye bidhaa za matumizi ya kila siku anazonunua mwananchi wa kawaida?

Ndugu watanzaania wenzangu, wakati tunaendelea kutaabika na uguu wa maisha serikarri ya ccm imeendelea kupatwa na kashfa nyingi za ufisadi na matumizi mabayya ya fedha tunazokamuliwa kupitia kodi mbali mbali, na bila kupata ufumbuzi wa kisheria au kiamaadili kwa viongozi wote wabadhilifuu kushugghulikiwa kwa mujibu wa sheria ya nchi. Sisi tunakkamuliwa then wajanja wachache wanatumbua kwa kujinafasi bila matatizo.

Hivyo basi kutokana na rekodi ya takribani miaka 50 ya CCM kuwa madarakani bila kuwa na rekodii nzuri ya kujivunia na wao pia wanajua kuwa ni vigumu kutetea rekodi yao, choguzi zote huwa wanajaribu ku dictate issue au agenda ambazo hazina maslahi kwa watanzania ili kuwatisha na kuweza kutugawa either kwa misingi ya imani zetu za dini au matabaka yetu ya kikabila, mkakati huo sio mgeni masikioni mwa watanzania wengi kwani hivi sasa CCM from nowhere wameibuka na agenda ya amani na utulivu baada ya kuona upepo mbaya wa mabadiliko unavuma kama kimbunga cha sunami, sasa nia ya kukabiliana na upepo huo ni kuwatisha watanzania kuwa wao eti ndo custodian wa amani na utulivu na kupuuza ukwelii kuwa amani na utulivu ni desturri ya mila ya watanzania wenyewe.

Halii kadhaliika CCM wameibuka na underground movement ambayo inapita kwenye misikiti na makanisa kuwanunua viongozi wa dini wasiokuwa na maadili ya kweli ili waweze kuwashawisshi waumini wao kuchagua ccm,sasa hawa watu mchana wanahubiri kutenganisha dini na siasa lakini usiku ndo wako mstari wa mbele kuchochea udini na ukabila ili waweze kucchaguliwa kurejea madarakani. sasa swali la msingi la kujiuliza ni kwamba je tutakubali sera ya ccm ya kuttugawa watanzania kwa misingi ya udini na ukabila, izime vugguvugu la mabadiliko? na kuwapa uwanja mpana wa kupata kiburi cha kuendelea kuongoza taifa hili kwa kueneza propaganda kuwa wananchi wengi wanakubaliana na sera zao? au nguvu ya kura yako itakuwa ni moja ya kura za mabadiliko na kuikataa ccm na sera zake zisizotekelezeka na kuandika historia ya taifa jipya?

Ndugu mtanzania, tumeshuhudia ccm ikiishiwa hoja za msingii na kutupeleka katika siasa za maji taka na kututaka tusahau kuzungumzia rekodi yao ya uwajibikaji kwa taifa letu, lakini hilo lilishindikana, walikuja na sera ya kutaka kumshambulia mgombea wa CHADEMA kuhusiana na historia yake ya kuwa kasisi wa kanisa katoliki huko nyuma kabla ya kuacha na kuishii maisha ya kawaida kama hoja ya kum disqualify na kupata kura nyingi za ghiliba toka kwa jamii ya ki islam, na kuendelea kutisha waislamu kuwa ame sign mkataba na baraza la maaskofu kwa nia ya kuwatisha waislamu na wao waweze kupata kura za waislamu! na hiyo chuki na uchochezi uliopandiikizwa kwenye jamii ya watanzania inaweza kuwafanya watu wengi sana ambao ni makini na wapenda mageuzi kuogopa kumpigia kura Dr Slaa kutokana na propaganda chafu za kuwatisha waislamu.

Lakini wakati ndugu mtanzania yoyote mwenye imani ya ki islamu lazima ukumbuke nii ccm hii hii ilikwisha wahi kutuhumu chama ccha wananchi CUF kuwa ni chama cha kidini ili kuwatisha wakristo wapenda mabadiliko, na ni ccm hiyo hiyo iliyojikuta inaliweka suala la kadhi mkuu kwenye ilani yao na kushindwa kulipatia ufumbuzi, hivyo basi ni ukweli usiopingika ccm wamekuwa wakituchezeaa vichwa vyetu kila uchaguzi unapo wadia na kucheza na propaganda chafu yenye misingi ya imani za watu. Sasa je tutawaruhusu ccm kwa kura zetu kutugawa kwa misingi ya imani za dini?

Tukiweza kuvuka mtego huu wa udini ambao ccm wametuwekea na kupiga kura za mabadiliko basi utakuwa mwanzo mzuri wa kuleta mabadiliko ya kweli, kwani ccm watatambua kuwa the only policy work well for them is divide and rule. Tusimame kwa nafasi zetu na tusimpigie kura mtu eti kwa sababu ni mwislamu mwenzetu ama mkristo mwenzetu, tuangalie issue au agenda muhimu za uchaguzi huu ni nini? na tupige kura kutokana na agenda hizo.

Ndugu watanzania wenanggu kuna sababu muhimu za kuchagua CHADEMA na Dr Slaa kama ffuatavyo:

Ndugu mtanzania Mwenzangu,

Ukitafakari kwa makini sana, utaona tofauti kubwa kati ya chadema na CCM.
Moja, Chadema recognizes that there are fundamental problems that are preventing us from achieving our full potential as a nation.
Pili. Chadema has identified a solution.
Tatu. Chadema has proven that it has the willingness, audacity and determination to fully implement the solutions, for the benefit of the nation. CCM mpaka leo hawataki kukiri kwamba kuna upungufu ndo maana swala la katiba is not their priority na halimo kwenye ilani yao ya uchaguzi wala sera zao, so longer it serve on their party interest and small group of people interest, ndo maana hii mandate ya CHANGE CCM hawaiwezi, na wala hawa relate nayo, and that is why mwaka hadi mwaka they keep coming up with half measures and solutions to tackle the problems we have

Ndugu Mtanzania Mzalendo

soma ilani ya chadema na ilani ya ccm. Kuna tofauti kubwa sana, Na Kubwa zaidi ambalo mimi na millions ya watanzania linawagusa, ni suala la kubadilisha katiba. Chadema wana mpango wa kufumua katiba nzima iandikwe upya. This is where CHANGE we desperately need begins kwenye katiba. Everything that is wrong with our country starts with the constitution. Katiba ya sasa, inalea a dysfunctional system of government, ndo maana ahadi nyingi na sera za ccm hazitekelezeki ipasavyo....that is one reason, there are many in CCMs case. Lakini muhimu ni kwamba, CHADEMA has the desire and determination to bring a new constitution to bring about a new system of government. System ambayo italeta ufanisi na uwajibikaji.

We know that without an efficient, transparent and accountable system, we will be unable to deliver any meaningful progress which touch a lot of issues affect most wananchi daily life

Hali kadhalika mgombea wetu, Slaa ana rekodi ya miaka kumi na tano, akitetea maslahi ya taifa hili. Miaka kumi na tano, aki simamia maendeleo ya karatu kupitia halamashauri, wananchi wameona matunda ya uwajibikaji wake, utumishi wake kwa wananchi ...wa jimbo lake, na utendaji wake wa kazi bungeni. Katika bunge liliopita, wabunge wa Chadema ingawa wachache, walitimiza kikamilifu kazi ya ya ubunge. Wananchi are witness to this and that is where their faith for the party. They,

CHADEMA have proved themselves to wananchi and millions of Tanzanians agree. It is because of their record CHADEMA have their CLOUT. Hawaja toka hewani hawa. Given their solid record they have every right to contest for the presidency, and bring CHANGE that we so desperately need. Millions of Tanzanians believe that chadema is the alternative, just like millions believed kikwete was the altenative, until when he let us down. Kama tulimjaribu kikwete, kwanini tusimjaribu DR. SLAA?

Time and time again CHADEMA ni chama makini kwani ukiangalia historia yake hakikuwahi kukurupuka na kugombea uraisi in the past ELECTIONS toka kilipo anzishwa, in 1995 hawakugombea walitoa support kwa chama cha NCCR-MAGEUZI, 2000 Hawakuweka mgombea uraisi walitoa support kwa chama cha wananchi CUF, na hata this election kwa upande wa Zanzibar wametoa support kwa chama cha wananchi CUF upande wa Zanzibar kwani kinatambua nguvu ya upinzani Zanzibar, hivyo basi hawajakurupuka hawa, Chadema wanastahili kupewa ridhaa ya wananchi tarehe 31-10.2010 kwa kupewa kura nyingi za mabadiliko na CCM wapate nafasi ya kukaa pembeni na to clean up uozo wao.


KAMA UNAONA BADO HUJASHAWISHIKA KUMPIGIA KURA DR. SLAA BORA UMPIGIE KURA PR0F. LIPUMBA NA CUF, KULIKO WEWE MPENDA MAGEUZI KUIPATIA KURA YAKO CCM, HILO NI KOSA AMBALO FUTURE GENERATION ITATULAUMU NA KUTUONA HATUKUSIMAMA VYEMA KATIKA NAFASI YETU! BORA UHARIBU KURA YAKO KULIKO KUIPA CCM KURA KAMA HUWEZI KUUMPIGIA HASHIM RUNGWE WA NCCR-MAGEUZI AU PPT-MAENDELEO AU TLP, TAFADHALI NAKUSIHI USIPIGE KURA YAKOO KWA MGOMBEA WA CCM.

WASHA MSHUMAA WA MATUMAINI YA TAIFA JIPYA KWA KUPIGA KURA YA MABADILIKO , CHAGUA CHADEMA-CHAGUA DR. SLAA
 
Back
Top Bottom