samurai
JF-Expert Member
- Oct 16, 2010
- 11,478
- 24,250
Sijui unaishi wapi mwenzetu,,, labda masaki au msasani kule kwa wazungu,, huku uswazi hakufai, hivi unajua uchaguzi kule tarime inakuwaje?? Pale mwanza, musoma,mbeya wale vijana wasiojitambua baada ya kupiga kura hufanyeje?? Wenzio hata wakikuona tu nakigari chako unaenda kupiga kura wanataka wakusachi au wanajua wewe CCM!!! huu uchaguzi kazi ipo sio masihara haya unayofikiria na hakuna wakati vyombo vya usalama vinatakiwa kuwa makini kama huu..wakizembea tu basi wengi wasio na hatia wataumizwa au kufa...