Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 371,548
- 860,642
ni wimbo mzuri wenye mdundo mzuri na ujumbe unaotia. simanzi lakini uliokosa uhalisia na unaitwa ni wimbo wa dini lakini kimsingi asilimia tisini haujakaa kidini bali ni hadithi ya maisha
Tuangalie uhalisia unapokosekana
1.Baaada ya kupata masaibu ya mme wake anahangaika kutafuta msaada wa mawifi na rafiki wa mumewe lakini kila mtu anakuwa na udhuru, ina maana kati ya wote hakuna hata mmoja mwenye msaada?basi kama ni hivyo una matatizo wewe
2.Anajaribu bank lakini akounti zote anakuta zina shida hivyo hawezi kutoa pesa ,,,katika dunia hii ya utandawazi ni kitu ambacho hakiwezekani na ikitokea hivyo una bonge la nuksi
3.Unafika hospitali daktari anakataa kumtibu mgonjwa kwakuwa huna pesa lakini unamiliki vogue .jamani tuwe wakweli ina maana unamiliki vogue lakini huna hata bima ya afya yenu? na hiyo ni hospital au ni kidispensari? kwakuwa hospital kubwa ya hadhi yake hawatangulizi hela bali matibabu kwanza malipo baadae
4.Daktari anakataa kuchukua gari kama bond kwakuwa inakula sana mafuta, hv unaweka bond au unampa dokta aitumie? na hicho ni kidispensari cha mtu binafsi na si hospital .hospital ya kweli ni taasisi ambayo kuna utaratibu wake hivyo huwezi kwenda kuongea na dokta kuhusu malipo
5.una miliki vogue lakini nyumbani huna hata hakiba ya laki5? au huna biashara au huna rafiki binafsi wa kuweza kumkopa ?au hujui wale wanaochukua mali na wakatoza riba ukachukua kiasi unachohitaji?
Tatizo la Bukuku ni tatizo la waimbaji wengi hawana watu mahiri wa kuhariri kazi zao wanatunga wanapeleka studio produser anaweka beat ngoma inaenda hewani matokeo yake ni kutoa sub standards
Tuangalie uhalisia unapokosekana
1.Baaada ya kupata masaibu ya mme wake anahangaika kutafuta msaada wa mawifi na rafiki wa mumewe lakini kila mtu anakuwa na udhuru, ina maana kati ya wote hakuna hata mmoja mwenye msaada?basi kama ni hivyo una matatizo wewe
2.Anajaribu bank lakini akounti zote anakuta zina shida hivyo hawezi kutoa pesa ,,,katika dunia hii ya utandawazi ni kitu ambacho hakiwezekani na ikitokea hivyo una bonge la nuksi
3.Unafika hospitali daktari anakataa kumtibu mgonjwa kwakuwa huna pesa lakini unamiliki vogue .jamani tuwe wakweli ina maana unamiliki vogue lakini huna hata bima ya afya yenu? na hiyo ni hospital au ni kidispensari? kwakuwa hospital kubwa ya hadhi yake hawatangulizi hela bali matibabu kwanza malipo baadae
4.Daktari anakataa kuchukua gari kama bond kwakuwa inakula sana mafuta, hv unaweka bond au unampa dokta aitumie? na hicho ni kidispensari cha mtu binafsi na si hospital .hospital ya kweli ni taasisi ambayo kuna utaratibu wake hivyo huwezi kwenda kuongea na dokta kuhusu malipo
5.una miliki vogue lakini nyumbani huna hata hakiba ya laki5? au huna biashara au huna rafiki binafsi wa kuweza kumkopa ?au hujui wale wanaochukua mali na wakatoza riba ukachukua kiasi unachohitaji?
Tatizo la Bukuku ni tatizo la waimbaji wengi hawana watu mahiri wa kuhariri kazi zao wanatunga wanapeleka studio produser anaweka beat ngoma inaenda hewani matokeo yake ni kutoa sub standards